Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nichukue nafasi hii nikushukuru sana kwa kunipa nafasi kuchangia kwenye Wizara nyeti, kipekee nimshukuru sana Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi ambayo anaendelea kuifanya hususan katika ku-promote utalii wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Waziri wetu Mheshimiwa Jenista pamoja na ndugu yao Deo Ndejembi kwa Wizara ambayo wamepewa, hatuna mashaka kabisa na hawa wawili, Mheshimiwa Jenista tunamfahamu, tunafahamu utendaji wako tunaamini kabisa upele umepata mkunaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina hoja kubwa mbili, hoja ya kwanza nataka nitoe uhalisia wa upungufu wa watumishi na nita-site mfano wa Manyoni DC, hoja ya pili vilevile nitoe ushauri kwa Serikali juu ya maboresho ya ile program yetu ya ya Maboresho ya Utumishi wa Umma (Public Services Reform Program). (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wenzangu wote wamesema kwamba tunao upungufu mkubwa sana wa Watumishi wa Umma kwenye kada mbalimbali. Nitatolea mfano kwenye Halmashauri yangu ya Manyoni, kwa upande wa Manyoni upande wa walimu wa shule za msingi, tunao upungufu wa zaidi ya asilimia 60 hadi sasa na ukizingatia tunazo shule 20 mpya za UVIKO ambazo zimejengwa nadhani hili Waziri wa TAMISEMI atakuwa amelichukua, kwamba kuna shule mpya ambazo Mama Samia ametujengea mpya ambazo tunategemea mwakani zianze kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Manyoni upande wa shule za msingi tuna zaidi ya upungufu wa asilimia 60 wa walimu wa shule za msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa Sekondari tuna upungufu wa zaidi ya asilimia 33 wa Walimu wa Shule za Sekondari. Jambo la kusikitisha ajira zilizotoka mwaka juzi au mwaka jana, tulipata walimu 11 tu ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, nadhani utaona sasa tuna upungufu wa zaidi ya Walimu 600 lakini rate ya kuajiri ni Walimu 11.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tuna very serious problem upande wa watendaji wa vijiji kati ya vijiji 58 nilivyonavyo ni vijiji 39 ambayo ni sawa na asilimia 67 vina Watendaji wa Vijiji. Tuna Vijiji 19 ambavyo vimekaa zaidi ya miezi Sita ambayo ni sawa sawa asilimia 33 havina Watendaji wa Vijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii maana yake ni nini? Mama Samia amepeleka fedha nyingi sana za miradi vijijini, tunategemea hawa Watendaji wa Vijiji ndiyo wasimamie hii miradi, hatuna watendaji wa vijiji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa afya tuna upungufu zaidi ya asilimia 60 ya watumishi wa afya, (Human Resource for Health), hili ni tatizo kubwa na waliopo ni kama asilimia 38.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu upande wa utumishi ni kwanza, nadhani tunahitaji kuhuhisha mfumo wa ajira za Watendaji wa Vijiji. Huko nyuma Watendaji wa Vijiji wengi walikuwa wanatoka kwenye maeneo husika sasa hivi tunamchukua Mtendaji wa Vijiji Kigoma anakwenda kufanya kazi Bagamoyo, ndiyo ndugu yangu Mheshimiwa Tabasamu ameeleza pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeshauri Mheshimiwa Waziri uangalie upya, kama inawezekana Watendaji wa Vijiji watoke kwenye maeneo ya karibu na ile halmashauri husika. Hii itapunguza hulka ya Watendaji wa Kijiji kuhama pia tuta- improve retention.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni kuhusu utoaji wa vibali mbadala replacement. Wakati Waziri anakuja ku- windup nitapenda kujua standard operating procedure ukomo, hivi kwa mfano, samahani labda mtumishi amefariki replacement yake inatakiwa ichukue muda gani policy maxmum ni vizuri tukalijua hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ni kuhusu ile program yetu ya kuboresha utumishi wa umma. Tulikuwa na program nzuri sana ilianza 2002 awamu ya kwanza, ikaenda 2007 awamu ya pili, kutoka 2007 ikenda 2012 ikaisha, kuna maboresho makubwa sana yalifanyika katika utumishi wa umma. Swali langu la msingi ile program tangu ife nini mpango wa Serikali kuja na uendelevu wa Interventions ambazo zilifanywa na program ya kwanza na ya pili? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wadau mbalimbali ambao wamekuwa na interest kubwa sana ya kusaidia Serikali, wakiwemo World Bank, USAID, GIZ, EU na wengine, ni nini mkakakati wa Serikali wa kuwa-engaged hawa wadau ili tuje na a new program ambayo itasaidia kuendeleza intervention za program one na program two.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni maeneo nyeti sana, tumeona ripoti ya CAG bado kunachangomoto nyingi sana kwenye utumishi wa umma. Suala la accountability lakini kuna suala la ethical issues, suala la utendaji, suala la performance management, haya mambo yanahitaji kuboreshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila siku kuna uteuzi unaendelea, kwenye upande wa leadership viongozi wanatakiwa wanolewe, hii program ndiyo itakuwa muarobaini wa kuboresha utumishi wetu na utumishi wa umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya nakushukuru na ninaunga mkono hoja. (Makofi)