Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi, na mimi naungana na wenzangu kumpongeza Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya. Nampongeza kwa dhati kwa sababu najua hii Wizara aliyoipata ambayo anaifanyia kazi mara nyingi amekuwa anaifanyia kwa vitendo. Nimemshuhudia mwenyewe Mheshimiwa Nape akipiga gitaa, nimemshuhudia mwenyewe Mheshimiwa Nape akiimba, nimemshuhudia mwenyewe Mheshimiwa Nape akicheza kiduku, nimemshuhudia Mheshimiwa Nape akicheza sindimba, nimemshuhudia Mheshimiwa Nape akicheza mayonjo, ina maana yuko kwenye fani. Nakupongeza sana Mheshimiwa Nape pamoja na Naibu Waziri wako. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu utaenda kwa vifungu, kwanza nianze kidogo kwa mkwara tuliopigwa kwamba tukienda kucheza kwa King Kiki tutakuwa tumekula rushwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Afya wakati anawasilisha Bajeti yake alikuja na wanakijiji hapa akatuambia kijiji kile kina miaka mitano hakuna mama aliyefariki kutokana na uzazi, tukapiga makofi. Alipokuja Waziri wa Muungano na Mazingira alikuja na Waasisi wa Muungano akatuonesha tukapiga makofi, lakini pia, akatuonesha mwanafunzi Getrude Clement ambaye alituwakilisha Marekani kwenye masuala ya mazingira, tukapiga makofi. (Makofi)
Lakini pia alipokuja Waziri wa Biashara, Viwanda na Uwekezaji alituambia pale nje kuna wafanyabiashara wa magari wanaotaka kwenda kununua yako pale, tukapiga makofi. Pia Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wakati anawasilisha mada yake hapo tuliwaona maafande wamejaa huku tele wa kila Idara tukapiga makofi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tuko Wizara ya Habari, Utamaduni, Michezo na Sanaa, Waziri anaonesha wadau wake, tunaambiwa tukienda kucheza kwa King Kiki tunakula rushwa, hiyo haki kweli?
Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi King Kiki nimemjua nikisoma shule ya msingi, nikasoma sekondari, nikaolewa, nikacheza muziki kwa raha yangu, nimeingia Bungeni King Kiki yupo na akipiga ninaingia. Kwa sababu hiyo imeonesha jinsi gani wanamuziki wakongwe waliokaa hapa nchini na kufanya kazi zao bila kutetereka, sasa kama mtu amefanya shughuli ya muziki kwa kipindi kirefu, leo anakuja hapa kuonesha ujuzi wake na kuwafurahisha Wabunge, mnasema ni rushwa. Hivi mambo mangapi yanayofanyika humu ndani, mbona hamyasemi? Mmeona tu ya King Kiki kuja hapa kuwaburudisha Wabunge ndiyo imekuwa nongwa? Tubadilike! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaendelea kuzungumzia sekta ya habari. Kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza wamiliki wote wa vyombo vya habari hapa nchini bila kuwasahau wenzetu wa Gazeti la Uhuru na Mzalendo, pamoja na redio Uhuru. Pamoja na pongezi hizo kwa wanahabari na wamiliki wa vyombo vya habari nizungumzie maslahi ya wanahabari.
Mheshimiwa Mwenyekiit, wanahabari wengi mapato yao yako chini, wanahabari wanaweza wakapewa sehemu wakafuatilie kazi bila usafiri. Lakini wanahabari hawa pia bado tuna matatizo nao kwamba wana utaalamu wa kuandika pia habari potofu. Unaweza ukakuta taarifa ile ile kwenye gazeti hili unaambiwa sita wamekufa, hili saba wamekufa, lingine 10 wamekufa, na lingine watatu wamekufa, ajali ni ile ile moja, hilo pia ni tatizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna tatizo la kutoa habari kwa upendeleo. tatizo hili tumeliona hasa kipindi cha uchaguzi na kipindi cha kampeni. Ni vizuri basi, zile taasisi za habari zijielekeze moja kwa moja kwamba tuko hivi, kama walivyofanya redio Uhuru na magazeti ya Uhuru kwamba, ukienda kule unajua wewe ni Chama cha Mapinduzi, vingine vimekaa kimya huku vinatoa habari kwa upendeleo. Tumeviona, tunavijua na tutavifanyia kazi maana Serikali ni yetu, Mheshimiwa Nape ni wetu na tutapambana. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, siamini kabisa kama Mbunge utakaa ndani ya Bunge kwa miaka mitano, toka asubuhi mpaka jioni wanakuona kwenye tv kwenye Jimbo lako utapata maji, utapata zahanati, utapata shule, utapata barabara, utapata umeme hiyo siamini! Ninachoamini ni kwamba utakapokuja kwenye Bunge na kutoa hoja zako na kurudi kwenye Jimbo lako kwenda kutekeleza yale ya wananchi waliyokutuma ndipo utakapopata maendeleo na ndipo watakapokuchagua. Hawakuchagui kwa kuangaliwa kwenye tv. Ingekuwa kuangaliwa kwenye tv tunachaguliwa tusingeenda Majimboni kuomba kura. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu gani kinachong‟ang‟ania sana tu kwenda kwenye tv. Mmemzomea Rais hapa na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi tumenyamaza, mkatuona wajinga. Mkaendelea akaja Waziri Mkuu hapa mkakataa kusikiliza hotuba yake wala kuichambua, tukanyamaza kimya mkasusa mkatoka hatujawasemesha, lakini pia uchaguzi wa Zanzibar mmenuna, sisi tumepiga kura tumemalizika.
MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ni kwamba, siku zote ninyi mkinuna wenzenu wanakula. Kununa mnanuna wenyewe halafu mnalalamika! Hakuna kitu chochote ambacho hakina mwanzo. Tuliingia kwenye Bunge vizuri, tulikuwa tunaonekana kwenye televisheni na kila mtu alikuwa anaona raha kuonekana kwenye televisheni, lakini haya mmeyataka ninyi wenzetu. Televisheni mmefanya ndiyo kituo cha kutukania viongozi wakubwa Serikalini, kutukania Marais, kukashifia Serikali iliyoko madarakani, hatuwezi kukubali. Kuna watu hawapendi ugomvi, kuna watu wameamua kujiweka sawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wameamua kujiweka sawa kwa maana kwamba, kitu kingine kama mtu hataki…
MWENYEKITI: Waheshimiwa naomba utulivu jamani tumsikilize Mbunge. Naomba nidhamu ndani ya Bunge, upande huu nimewasikia.
MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Kama mtu hataki siyo lazima apambane na wewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usiwe na wasiwasi mimi nilishasema daktari aje apime watu akili. Kwa hiyo, usiwe na wasiwasi waache wazomee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani mtu toka asubuhi anatoka nyumbani anamuaga mke wake anakuja hapa kwa kazi ya kuzomea. Halafu analalamikia tv! Tv ya nini?
MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi mimi nitakubali kweli mzazi wangu anatukanwa humu halafu nakubali. Hicho kitu hakiwezi kukubalika. Binafsi kama Mheshimiwa Malembeka siwezi kukubali kiongozi wangu anatukanwa humu televisheni na wote wanamuangalia, siwezi kukubali. Kwa sababu hata mzazi wako kama anatukanwa, ukihadithiwa tu unataka kupigana sembuse kuangalia. Hicho hatuwezi kukubali.
Taarifa....
MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei hiyo taarifa kwa sababu zifuatazo; Kwanza nina uhakika humu ndani kuna watu wameoana bila taratibu, wake zao nyumbani hawajui lakini hapa wanajifanya mke na mume, hilo la kwanza. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hiyo ninaikataa kwa sababu mimi ninajua ndoa ya mkristo ni moja, siyo mbili wala tatu, lakini kuna watu humu wana wake, ambao wake zao hawajui, mbona hawaoneshi kwenye televisheni?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea, wasinipotezee muda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nirudi kuhusu suala la michezo. Kwanza nizungumzie suala la vifaa vya michezo, ninaomba bei zipungunzwe kwa sababu sasa hivi vijana wengi wamejikita kwenye michezo lakini vifaa bei iko juu. Ndiyo maana utakuta wakati mwingine wanacheza mpira bila viatu, kwa hiyo ni vizuri bei ya vifaa vya michezo zipunguzwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda nizungumzie Kijiji cha Michezo kilichopo Mvuti katika Kata ya Msongola, eneo lile limetengwa heka 10 kwa ajili viwanja vya michezo…
MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.