Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuipongeza Serikali kwa bajeti nzuri yenye matumaini makubwa kwa nchi yetu. Nina mapendekezo yafuatayo nikianza na ujenzi wa vituo vya afya. Jimbo la Mbinga Vijijini mpaka sasa lina kituo kimoja cha Mapera kinachofanya kazi. Ikiwa jimbo hili lina Kata 29 na Tarafa tano. Nashukuru kupata vituo viwili vya kimkakati katika Kata ya Mkumbi na Muungano ambavyo vinajengwa lakini bado kuna vituo vya kimkakati vya Mbuji, Ukata na Litumbandyosi naomba vianze kujengwa.

Pia naiomba Serikali iunge mkono juhudi za Wanambinga Vijijini ya kukamilisha maboma ya zahanati, shule ya msingi na ofisi za vijiji na kata ambapo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wananchi wameitikia wito wa ujenzi wa miundombinu hii, ombi lao ni kuwaunga mkono!

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu TARURA; napendekeza mgao wa fedha uendane na hali halisi ya maeneo yetu. Mfano Jimbo la Mbinga Vijijini lina mtandao mkubwa wa barabara wenye sura ya nchi ya milima na mabonde na mvua nyingi, kiasi cha kuhitaji maraja na mifereji. Hali hii inahitaji bajeti kubwa tofauti na ya ujenzi wa barabara tu. Hivyo napendekeza kwa majimbo ya aina hii yapewe bajeti ya ziada ili kukabilina na mazingira hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utawala; Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga pamoja ukubwa wa kijiografia ikiwa na umbo la mwezi ina kata 29 zenye uwezo wa kuzaa kata nyingine na tarafa tano, tayari tumekamilisha mchakato katika ngazi ya Wilaya na mkoa la kugawa Halmashauri hii na kata, maombi haya yapewe kipaumbele muda ukifika ili kusogeza huduma kwa wananchi tofauti na ilivyo sasa mwananchi wa upande mmoja ili kupata huduma analazimika kupita Halmashauri nyingine ndipo azifikie ofisi za Halmashauri.

Kuhusu Mfuko wa Jimbo, napendekeza utolewe zaidi ya mara moja tofauti na ilivyo sasa kwa miaka hii miwili umetolewa mara moja kwa mwaka kiasi cha kuchelewa kuchochea baadhi ya shughuli za maendeleo za wananchi hususani za msimu.