Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwapongeza sana kwa mchanganuo mzuri wa bajeti unajieleza kwa kila sekta. Pia napenda kuwapongeza viongozi wote, Waheshimiwa Mawaziri wote kuanzia Waziri Bashungwa, Mheshimiwa Silinde na Mheshimiwa Dkt. Dugange nawapongeza hasa kwa prompt action kila ambapo kuna suala la kushughulikia. Ninawiwa pia kuwapongeza Watendaji Wakuu na wa chini, wako very cooperative. Kwa kweli katika hali ya kawaida huwezi kutarajia Katibu Mkuu au Naibu Katibu Mkuu umuandikie message na akujibu, lakini kwa hakika kuanzia Profesa Shemdoe, Dkt. Grace, Dkt. Mkama na Ndugu Gerald Mweli na Mzee Cheyo kwa kweli binafsi ninapata ushirikiano mkubwa sana. Nimewiwa kuwapongeza na muendelee hivyo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Wizara kwa mwaka wa fedha 2021/2022 mlitoa maelekezo kwa LGAs zote kuwa na mradi mmoja wa kimkakati, kwa mfano Mafinga tunaendelea na ujenzi wa Kituo cha Afya Ifingo, ni jambo jema ambalo linawafanya wananchi kunufaika na own source. Nashauri pamoja na kuwa tunaanzia mipango katika vikao vyetu vya Kamaka, Kamati ya Fedha hadi Baraza la Madiwani, nimebaini kuwa kama Wizara iki-set lengo LGAs zinabanwa kutekeleza, kwa mwendo huu kila baada ya miaka mitano ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo unapokamilika tutakuwa na miradi ambayo sio tu ina tija kwa wananchi lakini ambayo inaonekana kwa macho ya kawaida. Kwa sababu hiyo, nashauri na mwaka huu wa fedha Wizara itoe maelekezo mahsusi kwa kila LGAs zenye mapato ya kiwango fulani kutekeleza mradi mmoja wa kimkakati usiopungua shilingi milioni 400.

Kuhusu wamachinga, imekuwepo dhana kwamba ni maeneo ya Majiji na Manispaa tu ndizo zina changamoto ya wamachinga, kumbe hata TCs kama Mafinga TC au Makambako TC au Korogwe TC na kadhalika. Nimeona katika mipango ya Serikali kiasi fulani cha fedha kitapelekwa katika baadhi ya Majiji kama Dodoma kwa ajili ya miundombinu ya wamachinga, nashauri fedha hizi hata kwa kiwango kidogo, LGAs ambazo ni Town Council pia ziweze kutazamwa. Kwa mfano Mafinga TC ni Mji ambao upo kando ya highway ya Dar - Malawi/Zambia mpaka South Africa, ni mji wa kibiashara kutokana pia na sekta ya mazao ya misitu, hivyo changamoto ya miundombinu ya wamachinga ni kubwa hivyo ni muhimu kupewa fedha kwa ajili ya jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu TARURA/Tactic; kwanza napongeza utararibu ambao ni shirikishi, hususani kutujulisha fedha za ujenzi wa barabara, lakini pia semina ya Wabunge kuhusu ambavyo TARURA imejipanga kuanza kutangaza zabuni mapema kusudi miradi kuanza kabla mvua hazijaanza. Pili napongeza watendaji wa TARURA kuanzia CEO wao Engineer Seif na watendaji wake mkoani Iringa na Mufindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti,ushauri wangu na maombi; wakati tunapewa fedha za barabara, Mafinga tumepata bilioni moja kwa sababu ya maelezo kuwa tupo kwenye Mradi wa Tactic, ninavyoona mradi huu wa Tactic utatekelezwa kwa awamu na kwamba sasa katika miji 12 tayari wataalam wameshaenda kufanya kazi za awali, ninaomba na kushauri kwanza wakati ambao bado mradi wa TACTIC haujaanza tutengewe fedha kama maeneo mengine ambako walipata shilingi bilioni 1.5; pili, nashauri kama ambavyo Serikali ilijenga heshima na kuchochea ukuaji wa shughuli za uzalishaji katika mradi wa TSCP, mradi huu wa Tactic ni vema ukianza kwa pamoja kwa sababu kwa maelezo utatekelezwa kwa awamu, tukianza pamoja tutaokoa baadhi ya gharama hasa kwa sababu gharama ya vifaa vya ujenzi zinapanda kila kukicha, mradi utakaotekelezwa mwaka 2022 gharama zake sio sawa na wale ambao tutaanza miaka ijayo na tatu, Dromas nashauri TARURA watusaidie kuharakisha mchakato wa kuingiza barabara katika mfumo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano Mafinga mimi binafsi kwa kushirikiana na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa/ Vijiji, Madiwani na TARURA tulitembea jimbo zima kubaini barabara ambazo zinapaswa kufunguliwa na ambazo zinapaswa kuingia katika mfumo. Ilikuwa ni kazi ngumu ya wiki mbili, baadhi ya maeneo tuliwashirikisha mpaka Mabalozi. Naomba kwa msisitizo mtusaidie barabara za Mafinga ziingie katika Dromas, na hii itasaidia sana kuendana na zoezi zima la anuani za makazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uharaka katika maombi ya kubadilisha matumizi ya fedha; ninashauri, Halmashauri tukiwasilisha maombi ya kubadilisha matumizi ya fedha basi tupate mrejesho kwa wakati. Ninao mfano hai, Mafinga TC kwa mujibu wa utaratibu tuliwasilisha maombi ya kubadilisha matumizi ya fedha kwa kuandika kwa RAS na baadae RAS akawasilisha Wizarani, lakini imetuchukua miezi almost sita maana kutoka Septemba mpaka Machi na hii baada ya mimi Mbunge kuanza kufuatilia in personal kwa sababu Madiwani katika vikao walianza kuhoji na kuniomba nifuatilie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu, alimradi taxation zote na sababu za kubadilisha matumizi tunakuwa tumekidhi basi tujibiwe kwa wakati na kama kuna maelekezo tofauti basi pia tujulishwe. Nadhani katika jambo hili hakuna ambaye sikumtafuta kuanzia Mheshimiwa Waziri mpaka Mzee Cheyo na ndio maana pale mwanzo nimewapongeza kwa sababu wote walikuwa wana-respond kwa haraka mpaka likafanikiwa, lakini it took too long.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.