Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kupongeza sana siku ya leo pia ni siku nyingine kubwa ambapo Bunge limefanya kazi kubwa likijadili taarifa za Kamati ambazo zina majukumu mengi na nimpongeze sana Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria, Mheshimiwa Joseph Kizito Mhagama pamoja na Makamu wake na Wajumbe wa Kamati hiyo, lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Rweikiza pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Sheria Ndogo wamefanya kazi kubwa sana, taarifa zao kama mmeona zinatofautiana maazimio mathalani ya Kamati ya Katiba na Sheria ni maazimio 22 ni maazimio mengi sana, na kwa hiyo niwapongeze sana Kamati hii kwa kazi kubwa ambayo wanafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo ni mengi siwezi kuchambua yote, lakini niseme sisi tumepokea kama Serikali na kazi yetu sisi kwa Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na uratibu lakini yapo ambayo tuna husika na Kamati hii kwa sababu na sisi tunawajishwa na hii Kamati ya Katiba na Sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamegusia maeneo kadhaa lakini moja hili la Ofisi ya Mpigachapa Mkuu wa Serikali nataka niwapongeze sana Kamati namna ambavyo wameliweka azimio hili, sisi kwetu ni kazi kwa sababu Ofisi ya Mpigachapa Mkuu wa Serikali ni ofisi ambayo kwa kweli inahitaji kuangaliwa sana na Serikali tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba tunaijengea uwezo ili iweze kutekeleza majukumu yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanza tu nataka niwahakikishie Wajumbe wa Kamati na Bunge lako tukufu kwamba Serikali ina mpango wa kuifanya Idara ya Mpigachapa Mkuu wa Serikali kuwa Wakala wa Serikali. Tunataka kuifanya hivyo ili iwe na uwezo wa kufanya shughuli zake kibiahsara, kufanya shughuli zake kwa kufanya maamuzi yenyewe ya ndani kuliko ambavyo ilivyo sasa ambapo mambo mengi wanakuwa hawawezi kuyaamua kwa hiyo kasi ya utendaji wao inapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo Serikali inajenga kiwanda kikubwa cha kisasa hapa Dodoma ambacho kitafungwa mitambo ya kisasa na kutakuwa kuna uwezo wa hela kuanzia kununua vitendea kazi maana yake pia eneo la vitendea kazi kama makaratasi yanakuwa ni changamoto kwao na wanashindwa kupata kazi na kuzifanya kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwahakikishie kwamba hili tumelipokea kwa mikono miwili na tunaenda kulifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamezungumzia pia utoaji wa maeneo ya ujenzi wa Mji Mkuu wa Serikali kule Mtumba hadi sasa tumetwaa ekari 2030.88 na tumelipa fidia na fidia hii imeenda vizuri, nataka tuwahakikishie tu kwamba kama kutakuwa kuna haja ya kutwaa eneo lingine hakuna tatizo hamjasikia kelele yoyote Mji wa Serikali tutaendelea kufanya kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Sheria Ndogo imefanya kazi kubwa sana, ni mimi nimewahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati hii, naifahamu kazi hii, wameweza kuchambua sheria 685; siyo jambo dogo na wakabaini dosari 45. Wamefanya kazi kubwa na Kamati hii pamoja na mambo mengine pia imeweka azimio humu kwamba baadhi ya Wizara wakielekezwa wanakuwa hawatekelezi yale maazimio na maelekezo ya Kamati hasa kwenye sheria ndogo ambazo zina dosari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwaelewe Waheshimiwa Wabunge kwamba sheria hizi ndogo ndio zinazowagusa watu ambao tunawawakilisha humu ndani kwa hiyo ni lazima maelekezo yanapotoka basi sisi Serikali tunatakiwa tuwe active kuhakikisha kwamba tunafanya mabadiliko au tunajadiliana na Kamati na kueleza sababu kwa nini sheria ziko hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jukumu letu la uratibu kama Ofisi ya Waziri Mkuu litaendelea, tuliwakumbusha, nataka niwahakikishie Kamati kwamba tutaendelea kuwakumbusha tena ili maazimio haya yote toka tumeanza shughuli ya taarifa za Kamati yaweze kutekelezwa kwa kiwango kikubwa ili tukikutana mwakani kipindi kama hiki tuweze kuwa tunazungumza lugha ambayo hata kama hatukutekeleza yote lakini angalau tunasema kuna kazi fulani imefanyika kwa upande wa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na ninaunga mkono hoja. (Makofi)