Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia hotuba hii ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza ninukuu sehemu ya hotuba ya Waziri ukurasa wa tano kuhusiana na dira, vilevile iki-reflect Mpango wa Maendeleo ya Taifa Ibara ya 14 kwamba tunataka kujenga Taifa lenye umahiri mkubwa katika michezo ifikapo mwaka 2025, lakini ukiangalia bajeti hii huoni tafsiri ya dira hii na fedha. Huoni fedha zikienda kwenye hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano dhahiri sasa hivi na nimeshangaa sana kwa kweli Mheshimiwa Waziri Nape amezungumza hapa kuhusu watu kama akina Samatta walivyoiletea sifa nchi na siyo hivyo tu, michezo ni mingi na ni lazima tu-support michezo yote, lakini mchezo ambao Watanzania wanaupenda zaidi kuliko michezo yote ni soka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba hii kuanzia neno la kwanza mpaka neno la mwisho, halina neno Taifa Stars. Waziri ana picha kwenye kurasa nne za hotuba yake. Hakuna hata picha moja inayohusu soka. Mwezi ujao Taifa Stars inacheza na Egypt hapa Tanzania ambapo kwenye kundi letu ndiyo tumebakia na mechi mbili na zote ni timu hizo against sisi. Egypt against sisi, Nigeria against sisi. Tukishinda mechi ya nyumbani mwezi ujao, tarehe tano au tarehe sita, mechi ya ugenini ya Lagos ni mechi ya kumaliza ratiba. Hotuba hii ya Waziri haina hata kuwa-wish mafanikio Taifa Stars. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuwaje Taifa mahiri la michezo? Mheshimiwa Nape? Hata timu yako ya Yanga imeshinda juzi dhidi ya Angola umeshindwa kuwa-support humu, ambapo wakienda Angola kucheza wakifanikiwa wataingia round ya pili na Jerry Muro ameshaanza kututisha watapata hela, sijui na nini hata iwe nini, hata mshinde namna gani timu ya Kimataifa ni Simba tu!
MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupata maelezo ya Waziri kuhusu jambo hili la mchezo wa soka na namna gani ambavyo Serikali inajipanga kutengeneza Kina Samatta wengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tusisubiri watu wafanikiwe wao wenyewe tuje kuwapa sifa hapa lazima tuwatengeneze. Program ya kutengeneza sports academies nchi nzima iko wapi? Naiona kwenye Hotuba ya Kambi ya Upinzani. Viwanja vya michezo CCM imevikumbatia, viwanja vinaharibika, viwanja ambavyo vilijengwa na Watanzania wote kwa michango yao, Mheshimiwa Nape unashindwaje kuanzisha wakala wa viwanja vya michezo, viwanja vile viingie Serikalini, wala hayatakuwa maamuzi ya ajabu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mwenyekiti wenu wa CCM alitoa Chimwaga kuwa Chuo Kikuu cha Dodoma mnashindwaje kuvifanya viwanja tukaanzisha wakala wa viwanja vya michezo ili watu wacheze! tutengeneze tuweze kwenda na sisi tuingie World Cup. Kweli Mheshimiwa Nape huoni aibu hotuba nzima haina neno Taifa Stars?(Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya Waziri wa Fedha na Naibu wake hawapo hapa labda watapewa taarifa. Nchi zote duniani, fedha za bahati nasibu ndiyo huwa zinatumika kuendesha michezo. Leo hii Ujerumani waliweza kuwafunga Brazil bao saba, ile timu imetengenezwa kwa miaka 10 kwa fedha za bahati nasibu. Uingereza ni fedha za bahati nasibu, Australia ni fedha za bahati nasibu. Tunashindwa nini kuhakikisha kwamba Bahati Nasibu ya Taifa inasimamiwa chini ya Wizara hii ili Serikali isihangaike kutoa fedha za bajeti kupeleka kwenye michezo, fedha za bahati nasibu zitumike kuendesha michezo. Tunachoshindwa ni kipi?
Mheshimiwa Naibu Spika, jamani michezo ndiyo inayounganisha watu, tukienda pale Uwanja wa Taifa, Taifa Stars inapocheza, Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu wakifunga hamna CCM, hamna CHADEMA, hamna UKAWA, hamna ACT Wazalendo wote ni Tanzania, wote tuna bendera ya Tanzania. Kama unataka kuliunganisha Taifa ni michezo! Hebu tufanyeni maamuzi, tuhakikishe tunafanya maamuzi kuanzia Julai mwaka huu bahati nasibu itumike kuendesha michezo. Hatutahangaika hapa kumbana Mheshimiwa Nape na vibilioni mbili vyake anavyoviomba ambapo wala hatavipata! Tutapata fedha za kuendesha michezo. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu hapa wamezungumza suala la TBC. Mimi nashangaa sana, siku Waziri Nape ametoa kauli ya Serikali hapa kuhusu TBC tulibishana, Wabunge tukasimama, tukapinga, waliounga mkono wakasimama wakaunga mkono lakini Kiti chako kimetuita Wabunge wote tuliopinga kauli ya Nape kwenye Kamati ya Maadili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jana mimi nimepata barua kwamba mnatubana kusema, mnazuia Bunge lisionekane, hata kutoa maoni ndani ya Bunge tunaenda kuhojiwa? Mnaturudisha nyuma namna hii? TBC ni public broadcaster, TBC siyo government broadcaster ni public broadcaster.
Inaendeshwa kwa fedha za walipa kodi na kama tatizo ni bajeti Mheshimiwa Nape, TBC kwa nini hamjifunzi BBC? TBC inayo uwezo wa kuendeshwa kwa leseni maalum, kwa kodi maalum, kwa levy maalum, muhimu tu isishindane na vyombo binafsi kwenye biashara ndiyo BBC wanavyofanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuliwaambia wakati nilipokuwa Mwenyekiti wa PAC, tuli-commission report maalum ya financing public broadcaster na nilikwambia Mheshimiwa Nape kwamba TBC ni shareholder kwa Startimes. Nimeangalia report yako hapa kwenye randama ya Wizara yako hamna hata senti tano ambayo TBC inapata kutoka Startimes. Umefanya nini kuhusu mkataba kati ya TBC na Startimes? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vinga‟amuzi peke yake vikiwekewa fedha kidogo hata shilingi 500 tu vinaendesha TBC na tutakuwa na hata TBC Bunge tutaangalia bila shida yoyote. Kwa nini hamuwi-innovative Mheshimiwa Nape? Wewe ni kijana unatutia aibu vijana wenzako. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Nape wewe ukifanikiwa kwenye majukumu yako ndiyo na sisi wengine tutatembea kifua mbele tutataka majukumu zaidi kwa sababu tutaonyesha vijana wanafanya vizuri, brother be innovative! Tufanye kazi, tuifanye TBC iwe kama BBC iwe public broadcaster, wala hatutagombana tena, wala hatutakuwa na masuala ya bajeti hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii ukifungua redio zetu, ukifunga tv zetu zote binafsi na za public ni nyimbo za nje. Lakini ninyi mnasafiri, mkienda nchi za watu kuna limit. Leo ukienda Lagos husikii nyimbo za Diamond kama yuko Diamond peke yake. Lazima awe Diamond na Davido wamepiga pamoja ndiyo utazisikia, wana-promote wasanii wao. Sisi hapa sijui ni ulimbukeni wa ukoloni haujatutoka baada ya miaka 50!
Mheshimiwa Nape hili liko kwako, unataka kuwatetea wasanii, unataka kuwalinda wasanii hili wala huhitaji kubadilisha sheria. Content, kanuni za content ziko chini ya Waziri. Toa kanuni TCRA wazibariki asilimia 80 ya nyimbo zinazopigwa kwenye redio zetu na tv zetu ziwe za wasanii wetu. Anayetaka nyimbo za nje kutakuwa kuna channel za malipo aende kwenye channel za malipo alipie, apate hizo nyimbo za nje.