Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Nitachangia katika maeneo makubwa mawili; la kwanza Taarifa ya CAG imeongelea eneo la umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli findings za CAG kwenye Miradi ya ERPP na hata iliyokuwa miradi ya DADPUS ni sahihi na ripoti hii ya CAG ndio imekuwa msingi mkuu wa sisi kufanya mabadiliko katika Tume ya Umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Miradi ya ERPP ambayo Mheshimiwa Deus ameitaja ni miradi ambayo ilikuwa funded na World Bank na mfumo ule wa funding ulikuwa unaamua wenyewe namna ya kuwapata hadi Wakandarasi, hili ni jambo la kwanza. Wizara tumefanya mabadiliko sasa hivi ni sisi ndio tuna-design namna gani external funding ziende kwenye miradi ya umwagiliaji na hatutatekeleza mradi wowote wa umwagiliaji ambao hauna visibility study wala detail design. Hili ni jambo la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili miradi hii ya DADPs na ERPP kwa mfumo ulivyokuwa Tume ilikuwa makao makuu na sote tunafahamu katika Bunge hili. Nimekuwa Mbunge toka 2015, tumepitisha bajeti mbalimbali za Wizara ya Kilimo, tulikuwa hatutengi fedha za usimamizi wa umwagiliaji na sisi ndio tulikuwa tunapitisha fedha. Meneja wa Umwagiliaji wa Mkoa kwa mwaka anatengewa milioni mbili, tunatarajia muujiza. Sote tukiri hatukuweka concentration kwenye irrigation as a country for a very long time. Kwa hiyo tuchukue yale matokeo ya nyuma kama lesson wakati tunafanya reform. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Serikali inafanya nini? Sasa hivi tunaajiri Mainjinia 350, kila Wilaya tutapeleka Injinia wa umwagiliaji na Mheshimiwa Rais mwezi Machi atazindua magari ya Tume ya Umwagiliaji kwa ajili ya kupeleka katika kila wilaya ili tuweze kusimamia miradi ya umwagiliaji na fedha tunazopeleka katika eneo la umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili ambalo nataka niseme na Mheshimiwa Katani ametoka na hapa tumekuwa tunajadili. Je, bei inayoonekana sokoni anaipata mkulima ama haipati mkulima? Tumefanya survey kama Wizara na tuko tayari ku submit ripoti mbele ya Bunge hili. Mkulima wa mpunga msimu wa 2020/2021 na msimu wa 2021/2022 bei aliyoipata shambani ni mara mbili kuliko bei aliyoipata msimu wa 2020/2021. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili lazima watu tuelewe, msimu wa 2021/2022 sote sisi tunafahamu tumeishi na wakulima. Mkulima aliyeenda shambani kulima heka moja ya mahindi, alitumia shilingi 300,000 kwa ajili ya mbolea ya kupandia, alitumia shilingi 240,000 kwa ajili ya mbolea ya kukuzia, alitumia shilingi 60,000 kununua mbegu, alitumia shilingi 60,000 kulimia, alitumia wastani wa shilingi 40,000 kupandia na kupiga halo. Cost of production ilikuwa ni shilingi 720,000, tuna expect kitu gani kwamba auze, sisi Serikali NFRA tumenunua mahindi kwa wastani wa shilingi 700 na shilingi 800, haya tunayoyauza kwa shilingi 700 na shilingi 800 tuna- subsidize as a government.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli, wote tunafahamu kwenye commodity trading. Naomba hili nilisema kwa heshima kabisa, mkulima anayelima Nzega au anayelima Mbarali hutarajii ndio afikishe zao Soko la Dar es Salam lazima kuna intermediary. Ni jukumu letu kuviwezesha Vyama vya Ushirika viwe central aggregating na ndio hatua ambayo Serikali inachukua, ndicho tunachokifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwaambie ukweli, there is no way tutaondoa intermediaries. Tunachotakiwa kuangalia kama bei ya mlaji imeongezeka kwa asilimia mia kwa mkulima aliyeko shambani ka-benefit kwa asilimia ngapi kutoka kwenye ile asilimia mia, hili ndio la msingi. Sasa hivi Mheshimiwa Esther katolea mfano Tarime, Serikali imefanya nini? Tumevi-unlock Vyama vyote vya Kahawa, Pamba, Tumbaku vyote. Tumevipa mandate mbili ku aggregate cereals na ku-aggregate mazao yao ya biashara yanayoitwa, kwa sababu the biggest business itakuwa chakula. There is no way tutakimbia kwenye huu ukweli. Ni lazima sisi kama Serikali na sisi kama Wabunge, tum-protect mkulima, lakini hatuwezi kum-protect mkulima bila kufanya proper investment kwenye infrastructure. Serikali imetoa fedha mwaka huu, inajenga maghala 70, tuna-revive masoko ya Tarime, tuna-revive soko la Ngara, tuna-revive soko la…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Nimekuongezea sekunde 40 endelea Mheshimiwa Waziri wa Kilimo.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimalizie kwa kusema hivi, hakuna njia tutamwondoa mfanyabiashara kwa mazao, hakuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna njia tutamwondoa mfanyabiashara kwenye mazao. Vile vile hakuna njia tutakwepa forces za demand and supply kwenye soko. Bungeni hapa tuliilazimisha Serikali kwenye Korosho, tumeenda kuwatia hasara wakulima. Bungeni hapa tuliilazimisha Serikali ku-intervene kwenye pamba, tukatoa One thousand and two hundreds ambayo haiko sokoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tuna-struggle na matatizo ya pamba, it was this Parliament iliyoifikisha Serikali kununua pamba kwa shilingi 1,200 ambayo haiko sokoni. Aliyepata hasara ni mkulima. We will never allow this. Never government intervention ku-disturb soko. Tutapunguza gharama za ununuzi, tutapunguza gharama za uzalishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo ndiyo best practice, tutaongeza tija, tutaendelea kupunguza gharama za production ili mkulima azalishe kwa gharama ndogo, auze anakotaka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)