Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na mimi kunipa nafasi ya kuchangia machache kati ya yaliokuwa mengi yaliojiri kwenye Kamati yetu. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya PAC. Tumetoa taarifa yetu, hayo ni baadhi ya mengi tuliyoyaona.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza kuseme bado kuna changamoto kubwa ya value for money kwenye taasisi mbali mbali ambazo zinapewa fedha na Serikali. Taasisi nyingi au matumizi ya fedha yamekuwa si sahihi kwa sababu ya namna ambavyo haya mafungu, fedha zinavyotoka ina maana fedha kama haitoki kwa wakati, wakati mwingine inachelewesha kazi na hivyo Serikali kulipa riba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitachangia maeneo mawili, suala la kwanza ni mifuko ya uwekezaji ya wananchi kiuchumi lakini suala la pili, nitaongelea miradi ya maji, usanifu wa miradi ya maji; na hizi ni taarifa ambazo zipo kwenye Ripoti ya CAG.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza ni kuhusu mifuko ya uwekezaji wa wananchi kiuchumi. Katika taarifa ambayo ipo kwenye kishikwambi chetu, Mdhibiti ameonyesha ni kwa kiwango gani fedha zimetumika ndivyo sivyo; na kama hiyo haitoshi imetumika kwa watu wasiokuwa walengwa. Imesema out of 99 bilion ambazo zilitolewa ni zaidi ya bilioni 50.4 zilipigwa kwa maana ziliishia kwenye mikono ambayo haikuwa salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano kulikuwa na mifuko mitatu, mfano, mfuko wa pembejeo ambao ulitengewa bilioni 28, bilioni 20 zilipigwa ina maana kilichoweza kutumika ni bilioni nane tu ambapo ni sawa na zaidi ya asilimia 72 zilitumika ndivyo sivyo. Mfuko wa Kilimo Kwanza ambao ulitengewa bilioni 34, bilioni 28 zilipigwa au kutumika ndivyo sivyo, sawa na asilimia 80. Katika Mfuko wa Self-microfinance out of 34 ni bilioni 3.7 ambazo zilitumika ndivyo sivyo sawa na asilimia saba ya kile kiwango cha fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini ninasema haya, na kwa nini naongelea hizi fedha, ni kwa sababu hizi fedha zimetengwa kwa ajili ya kusaidia wale wafanyabiashara wadogo wadogo, wale watu ambao hawana access na maeneo ya benki.

Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zinaonyesha ni asilimia 28 ya Watanzania hawawezi ku-access fedha za benki, hawawezi ku - access mikopo. Kwa hiyo, hiyo mifuko ililenga asilimia 28 ya lile kundi la kundi la Watanzania ambalo haliwezi ku-access fund, kwa maana ya vikundi vidogo vidogo na watu ambao wana maisha ya chini. Kwa takwimu zetu leo ina maana ni zaidi ya watu milioni 17; na ukilinganisha na nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki, Kenya ni watu asilimia 18 ambao hawawezi ku– access fund, Uganda asilimia 14 na Rwanda asilimia 11. Kwahiyo, unaona kwamba Tanzania tuna asilimia kubwa ya wananchi hawawezi ku-access fund; na Serikali kwa maksudi ilianzisha mifuko na kuweka fedha ili ziweze kuwasaidia hawa watu kujikwamua.

Mhesimiwa Naibu Spika, nini kilichotokea? Kitu cha kwanza kilichotokea, wale ambao walipaswa kusimamia mifuko badala ya fedha hizo kupelekwa kwa wale wajasiriamali na watu wanaohitaji fedha; katika tathmini au katika study walioifanya mwaka 2016 na 2017 zaidi ya 80 percent ya zile fedha zilikuwa zimewekezwa benki au zimekopesha benki badala ya wajasiriamali wadogo wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini si hiyo tu wamesema kwa tathmini ya 2017 mpaka 2021 zaidi ya asilimia 72 fedha zilienda ambako hazikupaswa kwenda. Kwa maana ya wajasiriamali, wale watu wadogo wadogo wakulima akina mama hawakuweza ku-access fund. Kwa hiyo tunaweza kuwa humu ndani tunapiga kelele tunaangalia tutawakwamua vipi wananchi kumbe kuna watu wamepewa mamlaka, watu wanakusanya fedha au watu wamekuwa custodian wa hzio fedha lakini wanazipeleka maeneo yasiyofaa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mimi nakumbuka kipindi fulani nikiwa Halmashauri ya Ilala vilikuwa vinatengenezwa vikundi vya mfukoni watu wanaenda wanakusanya fedha wanapiga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na wameeleza na CAG ameeleza ni kwa nini hizo fedha zimepotea. Kwanza, watu walikuwa wanapewa fedha bila kufuata hata vigezo; pili, kulikuwepo na eneo la kuweka dhamana watu walikuwa wanapewa fedha bila hata ya kuweka dhamana, tatu; watu walikua wanakopa fedha bila hata kwenda kufanyia maksudi makubwa waliyoombewa fedha. Ambacho unaweza ukasema kwa kifupi ni kuona kwamba ni conspiracy. Watu waliopaswa kusimamia fedha walishirikiana na baadhi ya watu wakaweza kupoteza hizo hela. Inasikitisha sana, lakini si hiyo tu, walianzisha mifuko mingi; na Kamati yetu imekuja na pendekezo kwamba hiyo mifuko zaidi ya 52 waliyoanzisha kwa kazi ile ile; ningepata muda ningewasomea hii mifuko; mifuko hiyo inatoa mikopo kwa makundi yale yale na mwisho ya mwisho hizo fedha zikapotea. Ndiyo maana tumekuja na pendekezo kwamba mifuko iwe consolidated, iwe michache na iweze kuwa manage. Hayo ni machache (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika miradi ya maji, fedha nyingi zinapotea kwa sababu ya miradi ya maji ambayo Mdhibiti na Mkaguzi ameonesha katika ripoti yake ya ufanisi kwamba tatizo kubwa ni kutokuwa na masterplan. Ina maana usanifu wa kina haufanyiki licha ya kwamba sheria…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzumnguzaji)