Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Awali ya yote naunga mkono hoja ya Kamati zote tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia kwa kutafuta fedha na kupeleka fedha nyingi sana za maendeleo katika Halmashauri zetu. Kwa kweli hii ni kazi kubwa sana amefanya na kushirikiana na Serikali. Bado tunaona wako baadhi ya watumishi katika Halmashauri zetu ambao wanaturudisha nyuma kutokana na utendaji wao wenye madhaifu makubwa pamoja na vitendo vinavyotia shaka katika matumizi ya fedha hizi zinazoenda katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitolea mfano, pesa ambayo ilipelekwa katika ujenzi wa Vituo vya Afya karibu nchi nzima Shilingi Milioni 500, sasa hivi ukizunguka katika vituo vingi hivi havijakamilika. Vingi vimebaki tu majengo yako hapo, pia ukiangalia pembeni unakuta baadhi ya majengo utaona kuna vifaa vya ujenzi ambavyo vilikuwa vimenunuliwa vimebaki na hatua hiyo imeshapitwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hali hii sasa inaleta mashaka, wanachi wengi wanafika mahali wanaitilia mashaka Serikali yetu na wanafikia mahali ambapo hawaiamini Serikali yetu. Sasa baadhi madhaifu ambayo yanaonekana katika kazi hizi kwenye halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja; halmashauri nyingi zimeingia katika ujenzi wa majengo haya pasipokuwepo na quantity surveyors. Kwa hiyo, unaona BOQ nyingi ambazo zinaandaliwa, hazijaandaliwa na quantinty surveyors. Sasa mwisho wa siku jengo linafikia mahali halikamiliki ukiuliza wanasema hatukuwa na quantity surveyors. Sasa je, ni kwanini Serikali isitumie quantinty surveyors ili kuwa na uhakika wa gharama ya kujenga jengo hilo, badala yake tuanjenga na tunafikia mahali ambapo tunakwama na jengo halijakamilika, tunasema pesa hakuna?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini tunajenga tunafikia mahali vifaa vinabaki ambavyo havihitajiki tena na haviwezi vikatumika tena na ili hali tunasema kwamba hatukuwa na quantity surveyors? Inaigharimu shilingi ngapi hata kuweza ku–outsource quantinty surveyor ili tuweze kufanya kazi kwa uhakika?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia imeonekana kuwa watu wetu wengi wa manunuzi, kwa maana ya wale maafisa wa manunuzi, hawana knowledge ya kutosha katika supply chain management. Hivyo nitoe mapendekezo machache kwa ajili ya kuiomba Serikali iyafanyie kazi mapema ili tuondokane na changamoto hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja; tunaomba sasa majengo yote yanayojengwa katika halmashauri zetu tusiingie kujenga majengo haya pasipo kuwepo na BOQ ambayo imeandaliwa na quantinty surveyors.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili; hawa wataalam ambao wamesomea manunuzi, kila siku zinapoenda mtu anahitaji kuendelea ku-upgrade knowledge yake. Tunaomba hawa watumishi katika halmashauri ambao wanahusika na manunuzi wapatiwe knowledge ya supply chain management. Huwezi kukutana na habari ya material kubaki katika sites kama tutatumia watu wenye knowledge ambayo ni up to date.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini majengo yale ambayo yalijengwa katika halmashauri zetu na pesa zikaonekana hazitoshi yakiwemo majengo ya sekondari na majengo ya vituo vya afya, tunaiomba Serikali, kwa maana ya TAMISEMI, itenge pesa ili kukamilisha majengo yale kwa sababu sasa ni aibu kubwa sana katika maeneo yetu. Wananchi wanalaumu, wananchi wanalalamika na majengo yale yamekaa ilhali pesa nyingi ya Serikali imeenda pale na hakuna kinachoendelea. Naomba sana watu wa TAMISEMI watukumbuke pia katika kazi hii kule Serengeti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante. (Makofi)