Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa na naomba nichangie hoja iliyopo mbele yetu. Kwanza nataka nitumie nafasi hii kusema, tumesikia maoni ya Waheshimiwa Wabunge na ushauri waliotupa katika baadhi ya maeneo na sisi kama Wizara tunachukua na kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza mjadala umekuwa kwenye eneo la ushirikiano katika kutumia Taasisi za Majeshi na vilevile kutumia Vyombo vyetu vya Dola katika kushirikiana kwenye Sekta ya Kilimo. Nataka kuliambia Bunge lako Tukufu hivi karibuni nadhani siyo muda mrefu mtaona kwenye Vyombo vya Habari, Wizara ya Kilimo inasaini MoU na JKT kwa ajili ya maeneo yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, uzalishaji wa mbegu. Mbili, kwa ajili ya kutumia maeneo ambayo yanamilikiwa na Jeshi kwa ajili ya strategic crop mazao kama ya mafuta. Vilevile mbali na hapo jambo hili tulishalianza, namshukuru Waziri wa Ulinzi wa sasa na aliyemtangulia, mfano, mwaka huu wametuzalishia mbegu za alizeti tani 500, lakini vilevile mwaka huu tumesaini makubaliano na JKT Mgambo wanatuzalishia jumla ya eka 500 kwa ajili ya uzalishaji wa alizeti. Pia tunashirikiana na JKT Bulombora kwa ajili ya uzalishaji wa michikichi na sasa wameshaanza kusambaza miche ya michikichi itakayoweza kuzalisha jumla ya eneo la ekari 3,400. Kwa hiyo tumeshaanza mahusiano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nilitaarifu Bunge lako Tukufu na Kamati ya Mambo ya Nje, tumeanza ushirikiano mzuri sana na Wizara ya Mambo ya Nje na nimshukuru Waziri wa Mambo ya Nje, tumeshirikiana katika kufungua Soko la Parachichi China na sasa hivi tunashirikiana nao kwa ajili ya kuangalia namna gani tunaingia kwenye masoko ya COMESA hasa katika mazao ya tumbaku. Hivi karibuni pia tunashirikiana nao kwa ajili ya Mradi wa Maghala ambapo kuna wawekezaji wako tayari kuja kuweka. Tunafanya kazi kwa karibu na Balozi zetu zote, ingawa matokeo yanaweza yasionekane kwa haraka, lakini tumeanza ushirikiano mzuri sana na wenzetu wa Foreign.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niliongelee ni hili eneo la mfumuko wa bei kwa ufupi tu. Serikali inachukua hatua na mpaka sasa tumeshapeleka vyakula katika halmashauri 47 katika mikoa 15 katika nchi yetu na maeneo ambayo tayari yameishaanza uzalishaji tumefunga vituo. Mfano, katika Wilaya ya Sengerema, maeneo ya Buchosa ambayo Wakulima wameshaanza kuvuna tumefunga vituo vya kuuza mazao kwa bei ya nafuu na tunaendelea mpaka sasa tumeshagawa tani 23,000, lakini vilevile tumeweka allocations ya jumla ya tani 40,000 ya mahindi ambayo tutaendelea kuiingiza sokoni na kuiuza kwa bei ya kati ya Sh.700 mpaka Sh.800 ili ku-stabilize. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba na Bunge lako Tukufu lituelewe, hatuwezi kuondoa mfumuko wa bei kwa kuja na shortcut. Ni lazima tuongeze tija na ndiyo maana Serikali inawekeza kwenye maeneo ya umwagiliaji, inawekeza kwenye kutoa ruzuku za mbegu, tunatoa ruzuku ya mbolea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niseme tu Mradi wa Block Farm wa vijana; tunao vijana ambao wanatoka JKT aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ulinzi alisha-submit majina ya vijana ambao katika phase one tunaanza nayo, tutawachukua hao vijana kwenda nao kwenye hii project, hatuwaachi vijana waliyopo JKT, lakini lazima miradi hii iende parallel, maeneo ya JKT wataendelea kuwa-accommodate vijana na sisi tunaya-develop kupitia Wizara ya Kilimo tutawa-accommodate vijana wote. Ni Mpango ndiyo tumeanza, kunaweza kukatokea marekebisho, tutaendelea kurekebisha wakati tunakwenda mbele. Hata hivyo, la msingi lazima vijana wamiliki ardhi ili kuwafanya vijana wa nchi kuwaondoa kwenye kundi la watu wasio miliki ardhi na kuwaondoa kwenye hatari ya kuwa manamba katika nchi yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie eneo la ruzuku ya mbolea. Cha kwanza niwahakikishieni Waheshimiwa Wabunge mfumo wetu wa ruzuku wa mbolea ni mfumo bora kuliko mifumo ambayo tumewahi kuwa nayo huko nyuma. Mfumo wetu wa ruzuku unamtambua mkulima na niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, hofu ya kwamba tunaibiwa, kama tusingekuwa na Mfumo huu unaomtambua mletaji agrodealer, mkulima, hata mbolea ambazo zinatokea ubadhirifu tusingeweza kuzikamata. Niwahakikishie sitoingia kwenye record ya historia ya nchi kuwatia umaskini wakulima wa nchi hii kama baadhi ya watu walioingia kwenye record ya kuwatia umaskini wavuvi wa nchi hii. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. (Makofi)