Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nashukuru sana na nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais na Baraza lake la Mawaziri kwa namna ambavyo wameweza kutuletea mafanikio kwenye mazingira ambayo ni magumu sana, mazingira ambayo hata nchi zile ambazo zina chumi komavu hazijaweza kuyakabili inavyostahili na kwa hiyo mfumuko wa bei kwenye nchi hizo kubwa, nchi zilizoendelea, mfumuko wa bei uko juu ya tarakimu mbili na hapa kwetu unaona bado mfumuko wa bei ni takribani asilimia Tano au ni asilimia 4.8 na pia tunaendelea kukua kwa asilimia ambayo ni kubwa kuliko maeneo mengine na tumeweza kui-stabilize vizuri kwa namna moja au nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti kitu ambacho ni lazima tujivunie sana kwamba Serikali imefanya mambo ambayo lazima tufurahi kwamba inajizatiti na imeweka mifumo ambayo pengine kama itakuwa endelevu, kwa sababu tunaweza tukasema kwamba tumefanikisha lakini bado kuna viashiria kuna risk ambazo bado ziko kwenye uchumi ambavyo vinaweza vikapelekea hali ikabadilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inafurahisha pia kwamba malengo ya bajeti kwa mantiki ya matumizi na mapato yake yamefikia kwenye asilimia kwa wastani wa 95, ni nzuri yaani hatuja-miss sana malengo yetu. Kwa hiyo, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha na viongozi wengine wa Wizara niliseme hiyo ni jambo la kufurahisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema kweli suala la visababishi vya mtikisiko kwenye chumi nyingi siyo suala ambalo linakuwa ni la muda mfupi, siyo la mpito kwa sababu hivi vita vya Ukraine vinaonekana vinaendelea na vitaendelea, hatuoni upeo wake vitaisha lini. Kwa hiyo, siyo jambo tu la kusema kwamba tutapigana kwa mambo ya dharura kwa kufanya mambo ya dharura kwa kutoa ruzuku na kadhalika ni jambo ambalo lazima tuliangalie kwa mapana yake kwamba tuchukue hatua madhubuti ili kusema kweli tusipoteze muda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, turuhusu kwamba vitu vifanyike kwa namna ambayo inastahili na katika kufanya maamuzi yoyote ambayo tunajua kanuni moja ya kufanya maamuzi ni kutathmini kama lile jambo ni la mpito au kama litakaa, kama litakaa basi maamuzi unatakiwa kufanya ni maamuzi ya ku- accommodate ile na kuruhusu uchumi uanze kwenda kwa namna nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuje kwa mfano kwa upande wa suala zima la mfumuko wa bei. Mimi najiuliza tunatumia vigezo gani kulalamika sana? Kwa sababu asilimia Tano sisi tulioishi miaka ya kale hiyo, tulikuwa na mfumuko wa bei asilimia 30 tukaishi nao, yaani ukiwa na hela inaishia huko huko kabla hata hujaamka. Kwa hiyo, sasa kama kweli mfumuko wa bei tarakimu tunazopewa ni za uhalisia, mimi naamini kwamba pengine watu hawangelalamika kiasi hicho! Naamini kuna tatizo aidha katika hiyo takwimu tunayopewa, haijawa ya uhalisia kwa sababu kama mfumuko wa bei ya mahindi ingepanda zaidi mara mbili, asilimia Moja na Tano katika kipindi cha Septemba 2022, unachelea kusema pengine kuna kitu, mfumuko wa bei ungekuwa kidogo uko juu zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia niseme kuna jambo ambalo tulijue kwamba kuna ile base, ile index yenyewe ambayo inatakiwa iwe na episode za kupanda juu lakini baadae unaanza kui-stabilize kwenye level tofauti. Kiwango kile kinakuwa kimepanda halafu unai-stabilize kwenye level ile na inflation sasa inakuwa kwenye level nyingine kwa sababu ile index imepanda, lakini sisi hatuangalii hivyo vitu. Kuna two things, kuna kupanda ile index na yale mabadiliko ya ile index from time to time.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naamini kwamba hiyo ya kupanda, hiyo spike inatakiwa kwenye index ni nzuri mara nyingine. Kwa mfano, bei, nashukuru sana Mheshimiwa Mwigulu alisema siku moja, alisema mahali pengine sijui ni hapa, lakini ukweli ni kwamba bei za mazao ya wakulima zilikuwa chini sana kwa miaka mingi, miaka kama 10 hivi. Bei za mazao ya mahindi, mazao yote ambayo tunasema ni ya vyakula, zimekaa kama maji yaliyotulia. Sasa kwenye hali ya uchumi ya namna ile watu hawapati hamasa kuongeza uzalishaji, it doesn’t work.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka mwaka huu nikizalisha, nipate faida kubwa, inanirudisha kule kwenye shamba niongeze kilimo. Sasa unapoongeza kilimo, bei itashuka kidogo halafu bado ikishuka kidogo maana yake ni kwamba watu watasema sasa kuna glut, yaani mazao yamekuwa mengi kwa hiyo watu wanayapunguza kidogo kuzalisha, wanakimbizana na vitu vingine halafu kipindi cha mwaka unaokuja wanaona tena kwamba aah! mbona bei zimeanza kupanda kwa sababu mazao yameshuka? Kwa hiyo, inakwenda namna hiyo na that is the only how you can make agriculture pay. Kilimo hakitalipa!

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa mazao ya export, utaona kwamba pia exchange rate imekuwa stable sana. Tumesahau kwamba exchange rate pia ni instrument ya kutuwezesha kuendesha huu uchumi. Ili kuongeza faida ya exporters, watu wanaouza nje na hao wanaozalisha mazao ya kahawa, katani na kadhalika ni lazima exchange rate iwe ina-move ili akiuza akipata dola moja kule kwenye bei ya dunia haibadiliki sana. Utakuja kupata dola moja, inabakia Shilingi 2,300 kwa miaka mitano, utakuwa wewe gharama zinapanda lakini wewe hupati chochote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni lazima ifike mahali pia Serikali na Benki Kuu ione kwamba kuna umuhimu wa kuchochea exports kwa kuruhusu mabadiliko stahili kwenye exchange rate, siyo kuifanya tu ikae forever. Kwa sababu uzuri mmoja wa kufanya vile, ile haitakuathiri sana kwenye mambo ya ulipaji wa madeni kwa sababu export zipo kwenye dola ile ile na deni liko kwenye dola ile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme napongeza kukopa ndani zaidi kama tungekuwa kwa mfano, hiyo sekta binafsi haikopi, aidha sekta binafsi haikopi kwa zile riba ziko juu. Kwa sababu Serikali ikikopa actually deni linakuwa na uhimilivu zaidi kwa sababu deni la ndani halina tatizo la uhimilivu, lina tatizo la kukusanya tu mapato kwa sababu ni domestic revenue, lakini lile la nje lina tatizo kwa sababu lazima u- generate dollars, kama haujauza exports hutapata dola za kulipa zile dola na utapata matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo issue ni kwamba lazima tukubali kwamba exports lazima ziongezeke kwa sababu lile deni tunalo na lazima tutalilipa na tutalilipa kwa madafu. Madafu ukiwa nayo lazima uyabadilishe yawe dola. Kwa hiyo, ni lazima tukazane na hiyo na ninaamini mfumo mzima wa kusema tukimbizane na kilimo ni sawa, lakini pia tukimbizane mimi nafikiri katika vipaumbele tunavyo vingi, vipaumbele ambavyo lazima tuvikazanie sana ni utalii ambao unaleta haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo kina risk nyingi bado, hata ukijenga mabwawa, itajengwa kwa miaka mingapi uweze kuhamisha? Itachukua muda. Nadhani utalii, madini, mifugo utaona sasa hivi tuna-export nyama kwa wingi, mifugo na uvuvi pamoja pengine na madini, madini nimeshataja lakini naamini kwamba kuna ambavyo vipo najua kwamba ukifanya vitapiga. Ukisema utafanya hata ukiongeza itachukua muda na ile chances za ku-realize the potential ambayo wewe unalenga ni may be is fifty fifty. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme jambo la mwisho ukiniruhusu ni kwamba kuna hii mikopo ambayo imetengwa kwenye dirisha lile la Shilingi Trilioni Moja ambayo imetolewa wanasema Benki Kuu iko tayari kutoa, kusema kweli hiyo siyo realistic. Ukweli ni kwamba Benki Kuu Kifungu cha 40 cha Sheria ya Benki Kuu hakiruhusu Benki Kuu ikopeshe mabenki zaidi kwa kipindi zaidi ya miezi mitatu, sasa kilimo gani kinalimwa kwa miezi mitatu, hakuna! Mkimkopesha mtu utaenda kuvuna mazao yale ili akulipe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kuna tatizo hapo ni kwamba ni dirisha ambalo ni zuri lakini mimi naamini kwamba, hata hivyo wamewekea masharti kwamba lazima Benki ipeleke dhamana za Serikali, lakini ambacho wangefanya ni kwamba wangesema benki ilete mikopo ambayo imetoa kwa sekta binafsi kwa riba chini ya asilimia 10, walete hiyo portfolio halafu wa i–refinance wakifanya hivyo, benki ambazo hazina hata hii dhamana zitakopesha zitapeleka ile mikopo ita-refinance watapewa fedha wataendelea kukopesha sehemu nyingine watapewa kwa hiyo asilimia Tatu. Kwa hiyo, that is the only realistic way, otherwise mimi nafikiri kwamba ni ngumu sana kupata mabenki ambayo yatakopa na kukopesha kama inavyohitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kwamba muda umekwisha, naunga mkono hoja, mimi pia ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti, ahsante sana. (Makofi)