Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa nafasi ya kuchangia katika Hotuba ya Kamati hizi mbili, lakini kwa sababu ya ufinyu wa muda, nitachangia kwenye Kamati ya Bajeti peke yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna suala geni ninaliongea, ni masuala ambayo tumeshayaongea hapa kuanzia wakati mpango wa Serikali unaletwa, wakati wa bajeti tunayaongea na bado hayajapata majibu ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaenda kwenye kipengele 2:1:4 cha Taarifa ya Bajeti ambacho kinapatikana ukurasa wa 10 ambacho msemaji aliyetoka kuongea amekigusia au ndio amemalizia kinachohusiana na akiba ya fedha za kigeni, lakini nitaongelea pia au nitafungamanisha na kipengele 2:4:1 kilichopo ukurasa wa 25 kinachosema kutotabirika kwa Sera za Kodi na namna mambo haya yanavyoweza kusababisha biashara kudorora nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku mbili, tatu zilizopita kuna mchangiaji alisema humu kwamba kuna uhaba mkubwa wa fedha za kigeni hasa dola kwenye mabenki yetu. Wako wafanyabiashara na kuna Wabunge wafanyabiashara wamekwenda benki inachukulia hata wiki mbili kwa Dola laki moja na hili limeendelea na maeneo mengine unashawishiwa angalau mteja wako unayetaka kufanya naye biashara kwa Dola umshawishi aweze kuchukua fedha nyingine kama Euro na kadhalika. Sasa hatujapata majibu ya kutosha kwamba huu upungufu wa fedha za kigeni huku kwa wafanyabiashara unatokana na nini? Kwenye taarifa hapa inaonekana tuna fedha za kigeni za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini naifunganisha na kipengele 2:4:1, kutokutabilika kwa Sera za Kodi. Nataka kusema kwamba siyo Sera za Kodi tu lakini ni sera za uendeshaji katika nchi hii. Tulifanya operation ya kuondoa Bureau De Change, tukafunga Bureau De Change na kunyang’anya watu hela na nyaraka nyingine zilichukuliwa na tukasema kwamba sasa benki ndio zitafanya hiyo biashara na watu wakakubali, lakini kumekuwepo na utaratibu wa watu wachache kupewa leseni za bureau de change. Wako watu wengi wamekidhi vigezo vipya lakini hawapewi leseni za bureau de change.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siko tena kule kwenye kuuliza warudishiwe leseni, kule nimeshaona kwamba haiwezekani kwamba warudishiwe fedha zao, lakini wako ambao aidha walikuwa katika lile kundi la mwanzo au wengine wapya wamekidhi vigezo vyote vilivyowekwa kwenye maandishi lakini hawajapata. Nina uhakika na ushahidi wa watu saba, wanapojibiwa kwamba do not meet seat and proper test, yaani unajibiwa hivyo tu, mtu ana hela, mtu anafanya biashara nyingine, mtu analipa kodi, mtu amewekeza kwenye maeneo kedekede, lakini kwenye Bureau De Change anajibiwa hivyo tu au wengine wanaambiwa wana integrity issues, haielezwi. Sasa sijaelewa ipo kwenye kanuni, ni utashi wa Wizara au ni utashi gani, lakini tunaleta usumbufu mkubwa, watu wanahangaika na hatujui twende kwa nani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapoongelea suala la Bureau De Change nikiongelea Moshi Mjini na Arusha hatuongelei tu hawa wafanyabiashara wakubwa, tunaongalea Porter and Tour Guider aliyetoka porini au mlimani ameingia pale mjini saa kumi amelipwa tip yake kwa Dola anataka kubadilisha anunue nyama aende nyumbani hana mahali pa kubadilisha hiyo hela na ni kwa nini? Kwa sababu Bureau De Change zimezuiwa na benki hazifungui baada ya ule muda wa kawaida wa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tungependa Waziri atuambie, Serikali ituambie, kuna siri gani kwenye issue ya Bureau De Change? Kwa nini leseni wamepewa watu wachache? Watu wengine wanakwenda wanajibiwa kirahisi na hakuna majibu na watu wanateseka na dola hakuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kubwa zaidi, Bureau De Change walikuwa wana-change currency mpaka 20, lakini kwenye mabenki wana-change currency chache sana, Kenyan money ni baadhi ya benki kama KCB, Euro, dola, paund currency nyingine hawabadilishi, lakini tunajua kwamba kuna watu wetu wanakwenda hija wanahitaji hela, kuna watu wetu wanakwenda Dubai, wanahitaji hela ya Dubai, kuna watu wetu wanakwenda South africa wanahitaji hela ya South Africa, lakini mabenki yamejikita kwenye currency chache. Kwa hiyo ningependa sana Serikali itoe wingu kwenye suala la Bureau De Change kwa sababu linasababisha hasara kubwa, linasababisha usumbufu kwa wananchi na linawasababisha wafanyabiashara kushindwa kufanya biashara zao kwa uhuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu nyingine ambayo ningependa kuiongelea ni kipengele 2:1:2 ambacho kiko ukurasa wa saba, linalohusiana na mfumko wa bei. Nataka nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hela anayotoa kwa ajili ya ku-subsidize mafuta. Nimeona taarifa juzi Wizara ya Kilimo nayo imesema italeta mahindi mtaani kwa Sh.700 kwa kilo. Kwa kweli hizo ni juhudi kubwa sana za Serikali, lakini ukiangalia kwenye jedwali lililoko hapa katika mfumko wa bei, jedwali namba moja kwenye Taarifa ya Bajeti, inaonyesha chakula ndio kimekwenda asilimia 9.7 kwenye mfumko na chakula siyo mahindi peke yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunathamini sana mchango wa Serikali kupunguza hayo makali, lakini jicho zaidi litupiwe kwenye chakula, ni dhahiri kabisa purchasing power ya chakula Tanzania na Kenya zinatofautiana kwa sababu uchumi wake ni mkubwa. Kenya wana demand kubwa kwa sababu chakula chao hakiendi kwenda kuliwa, kinaenda kulisha viwanda na wana-export. Kwa hiyo wanaweza kununua kwa bei kubwa, tukiachia uhuru asilimia mia moja watu wetu watakufa njaa, lazima kuwe na control mechanism ya kuhakikisha chakula kinapata bei nzuri kwa namna ambavyo Serikali itaona inafaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishie hapa. Ahsante sana na naunga mkono hoja. (Makofi)