Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. YAHAYA O. MASSARE K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UKIMWI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa nafasi ya kuja kuhitimisha hoja yetu ya Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumepata wachangiaji wawili katika wengi lakini Mheshimiwa Waziri Simbachawene pia amesaidia kutoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo. Mheshimiwa Mwandamila alikuwa na hoja ambayo amezungumzia sana namna ya udhibiti wa madawa ya kulevya, waraibu wanavyoathirika na ukosefu wa waratibu kule kwenye Halmashauri zetu. Hili jambo ambalo tunaliomba, Kamati italisimamia na kuishauri Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna jambo ambalo kama Kamati imeliona ililete katika Bunge lako pamoja na mapendekezo ya Kamati kwamba zile Kamati za UKIMWI kule vijijini kwenye Halmashauri zetu zina Serikali kupitia TAMISEMI waone ni namna gani zitaweza kuhusishwa pia na dawa za kulevya. Maana yake zinajulikana tu kama Kamati za UKIMWI.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kulikuwa na mchangiaji mwingine ambaye ni Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, alizungumzia jambo ambalo Mheshimiwa Simbachawene pia amelitolea ufafanuzi. Nami pia niongezee kidogo. Hizi tafiti zinapofanyika zinalenga sana wale ambao wameathirika kwa kiwango kikubwa. Hii DHIS imechukua watu above 18 kwa sababu waliozidi miaka 18 mpaka 24 ndio wenye maambukizi makubwa. Wale ndio waathirika wakubwa. Kwa hiyo, Unapochukua sampling za kupata result ya research yoyote; ili sampling ziwe na matokeo mazuri, NI lazima uchukue kundi ambalo linaathirika sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa sababu mradi huu unaenda kwisha na Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba mradi huu unaisha, lakini sababu ilikuwa ni hiyo, kwamba watu waliokuwa wameathirika sana ni zaidi ya miaka18. Kwa hiyo huku mbele tunakoenda nadhani Serikali itaona na italifanyia kazi. Nasi kama Kamati tutaendelea kuishauri Serikali kwamba ione hilo pia, lakini kupunguza gharama za sampling. Unapofanya utafiti wowote, ili mchukue sampuli za watu wachache upate uhalisia, watu wa chini ya miaka 18 utahitaji kundi kubwa sana na gharama zitakuwa ni kubwa sana. Kwa hiyo, nashukuru sana kwa hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kama mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati hii, naliomba Bunge lako Tukufu lichukue mapendekezo ya Kamati na kuyafanya kama mapendekezo ya Bunge pamoja na nyongeza hii ambayo nimeiwasilisha hapo kwako. Naliomba Bunge lako Tukufu lipitishe mapendekezo ya Kamati kuwa mapendekezo ya Bunge ambapo Serikali itayatekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja.

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.