Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi, nashukuru pia kwa kuwa mchangiaji wa mwanzo jioni hii.

Mheshimiwa Spika, mimi ni mjumbe kutoka Kamati ya USEMI, sehemu kubwa ya taarifa uliyoiona maana yake hata mimi mawazo yangu yako hapo. Nitakwenda kwenye maeneo machache kwa msisitizo.

Mheshimiwa Spika, eneo la TARURA kama tulivyoongea kwenye Kamati. Wenzetu wa TARURA kwa kweli wanafanya kazi kubwa na niseme kipindi hiki ambapo tuko kwenye majira ya mvua ukienda katika maeneo mbalimbali nchini barabara zimekatika. Kwa hiyo suala zima la Mfuko wa TARURA katika eneo la dharura, tukizungumzia kuongeza fedha ni kwa maana hiyo. Eneo la TARURA upande wa dharura.

Mheshimiwa Spika, kila sehemu, ukienda Katavi, huko kote mvua zinakonyesha hata maeneo mengine ambapo hakuna mvua. Kwa hiyo eneo la kuongeza fedha nilikuwa naomba sana.

Mheshimiwa Spika, eneo la TARURA pia nilikuwa naomba kuna baadhi ya maeneo kuna miradi mingine kwa kupitia TASAF unaweza ukakuta wananchi kwa maana ya kujipatia kipato wameelekezwa kwenye utengenezaji wa barabara. Wengine wamefikia hatua ya kuchimba mitaro. Point yangu ni nini? Ikiwa kazi nzuri imefanywa na wananchi kwa kupitia vyanzo vingine kama TASAF, au Mfuko wa Jimbo, kazi hii nzuri isipounganishwa na kazi za TARURA hautoiona thamani yake. Fedha nyingi inaweza ikapotea katika eneo hilo, lakini inapendeza barabara nzuri ikifunguliwa, mitaro ikichimbwa, basi na wenzetu wa TARURA wazipokee kazi hizo ili kuwe na uendelevu wa shughuli.

Mheshimiwa Spika, naomba nitoke hapo. Eneo la pili ni kuhusu TAKUKURU rafiki. Nishukuru tumepitia kwa kupitia Kamati na tukaona mpango huu ni mwema, ni mpango mzuri, suala zima la TAKUKURU rafiki. Kwa maana siku zote tunaambiwa kama hujafanya utafiti hauna vielelezo usiongee. Wenzetu wa TAKUKURU rafiki wanatuambia 81.5% inazungumza kwamba rushwa ni tatizo nchini, lakini 92% wako tayari kwa mapambano dhidi ya rushwa na kuwapa ushirikiano Maafisa wa TAKUKURU. Point yangu ni nini? Mwelekeo wa dunia kwa sasa hivi au ulimwengu ni kuzuia rushwa kabla haijatokea na kwa kupitia TAKUKURU rafiki pia nao wamejikita huko kwa maana ya kuzuia zaidi.

Mheshimiwa Spika, wenzetu hawa kwa kupitia TAKUKURU rafiki na nimeeleza hivyo kwamba 92% wako tayari kutoa ushirikiano, lakini wenzetu wa TAKUKURU peke yao hawawezi, ni wachache, peke yao hawawezi, lazima wapewe ushirikiano. Niseme hivi, tutaishia kuwalaumu watu hawa, yaani mtu kama ni katika halmashauri, jiji au manispaa, usitimize wajibu wako, umemsainisha mtu ameingia kwenye kazi, mkataba haueleweki, baada ya hapo mtu huyo kapotea, amepotea kwa uzembe wa wewe kutomshirikisha kwenye mikataba, ikifika hapo unasema TAKUKURU njooni wakati wajibu wa kwanza ulikuwa ni wa kwako. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ninachotaka kusema nje ya hapo tutabebesha watu lawama, lakini naomba turudi, ndiyo maana suala zima la TAKUKURU Rafiki inatuelekeza kwenye uwajibikaji wa pamoja. Mbali na uwajibikaji wa pamoja, juzi nilikutana na familia moja nikaambiwa na mzazi wake, ananiambia mwanangu hata ukimpa fedha kiasi gani, ni mtoto mdogo, ukimpa fedha sana sana ataileta kwa mama yake. Hakuna mahali atatumia atafanyaje. Nataka kujifunza nini? Yaani mtoto mdogo akiwa na umri mdogo anaanza kujengewa maadili, hili ndilo, hili hapana, hili ndilo, hili hapana. Kwa hiyo kwake yaani fedha, yule mtoto mdogo amefika mahali ambapo hata kama atakwenda kwa makuzi hayo, anajua hiki kinanihusu, hiki hakinihusu. Nikisema hivyo nataka kumaanisha nini pia?

Mheshimiwa Spika, bado ukiacha uwepo wa vyombo hivi, na vyombo hivi kwa utamaduni vina asili ya mabavu kidogo, lakini tutoke nje ya mabavu. Kila mmoja hapa ana dini yake, wapo Wakatoliki, wapo Waislam na wengine hawana dini, lakini bado siku zote, kwa mfano mimi ni Mkatoliki, ukienda kwenye amri pale kuna sehemu unaambiwa usiibe, usiseme uongo na vitu vingine vya namna hiyo. Kwa hiyo kwenye maadili yetu ya dini yatuelekeze kwenye kusema hili hapana.

Mheshimiwa Spika, nimesikia kengele ya kwanza hiyo. Kwa hiyo ninachotaka kusema, ushirikishwaji wa pamoja wenzetu peke yao pamoja na nia yao njema bila watu kuwasaidia, hawatoweza.

Mheshimiwa Spika, Sekretarieti ya ajira. Niwashukuru sana watu wa sekretarieti ya ajira na hasa kwa sababu kulikuwa na maombi, vijana wanasafiri umbali mrefu kwenda kufanya usaili, leo sekretarieti ya ajira kwa kupitia Mheshimiwa Jenista pale wamesikiliza kilio cha Wabunge. Sasa hivi usaili umepelekwa kwenye kanda na mimi niseme hili ni jambo jema. Wakati ule ilikuwa watu wanasafiri, atoke Katavi, atoke Mwanza, atoke wapi labda kuja Dodoma au Dar es Salaam. Wazazi vipato vidogo, lakini nitoke hapo.

Mheshimiwa Spika, tumekwenda kwenye kitu kingine ambacho nacho naomba kiendelee kufanyiwa kazi. Habari ya kupata ajira kwa kigezo cha kwamba umepitia JKT niombe, Kamati imeelekeza kwa sababu nafasi za JKT hazitoki kwa kila huyo. Ukituacha sisi, mimi ni namba Z2639 OP Kambarage ya kutoka tarehe 15 Juni, 1990 mpaka 14 Juni, 1991. Sasa sisi wa miaka hiyo ilikuwa ukisema mtu awe na sifa ya kupita JKT ni kwa sababu ilikuwa tunapita kwa mujibu wa sheria. Sasa hivi nafasi ni chache, ukija na kigezo kwamba mtoto lazima apite JKT wakati hakupewa nafasi ya kwenda JKT, tunawanyima nafasi. Kwa hiyo naomba kigezo cha kwamba lazima mtu apite JKT vinginevyo tutimize wajibu wetu kwa kuhakikisha wote tunawapeleka JKT halafu tuwahukumu baadaye. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuheshimu muda, naomba kuishia hapo. (Makofi)