Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, mimi ni mwalimu na nimefundisha darasani kwa muda wa miaka isiyopungua tisa, kwa hiyo haya ninayotaka kuyaongea leo kwa uchache nayaongea kwa uzoefu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namba moja, hakuna mtoto ambaye hafundishiki akifundishwa. Kinachotokea kwa hawa watoto wetu hawa tunaona wanafeli masomo, wanafeli kwa sababu hawafundishwi. Kwa nini hawafundishwi? Kwa sababu hakuna waalimu wa kuwafundisha. Nina maana ipi, ametoa data nzuri sana Mheshimiwa Husna mimi siwezi kuzirudia kwa sababu ya muda. Mtoto anaanza form one, mwalimu wa hesabu hayupo, mwalimu wa physics hayupo, mwalimu wa chemistry hayupo, mwalimu wa biology hayupo. Akifika form two tunamtaka mtoto huyo afanye, mtihani wa form two ambao unahusisha hayo masomo yote unajumlisha hayo masomo yote ambayo hajafundishwa tunamtaka afanye mtihani na afaulu. Hakuna kitu kama hicho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hawa watoto tunaowaona wa shule zingine wanafaulu vizuri hakuna muujiza wowote, ni kwa sababu wanafundishwa. Hiyo ndiyo hoja yangu ya msingi leo. Sasa sisi kama Taifa tujiulize, kwamba kipaumbele chetu ni nini? Kama elimu hatuitilii mkazo kwa namna hiyo, kila siku matamko mbalimbali ambayo hayatekelezeki tunafikiri yatatufikisha mahali? Kwangu mimi kama mwalimu nasema hayo matamko yanayotolewa na viongozi wa kisiasa kila siku bila utekelezaji hayatufikishi mahali kokote. Kwa taarifa, naongea kwa uzoefu, issue ya kufundisha haianzii darasani pale pale kwenda kusimama kushika chaki kufundisha. Issue ya kufundisha inaanzia mbali.

Mheshimiwa Spika, kuna kitu kinaitwa scheme of work, kuna lesson plan. Mimi natakiwa nisome ile content, nisome ile mada ninayokwenda kufundisha nielewe, niingie darasani ndipo nifundishe. Sasa unapewa darasa ukafundishe lina wanafunzi 1,000. Hivi ninyi mnawajua watu 1,000? Wakikaa hapa yaani ukaambiwa watu 1,000 sisi humu ndani tuko 400 kasoro humu watu wote sisi. Sasa ndiyo umepewa darasa la watu 1,000 ukafundishe wewe mmoja na nimewaambia kufundisha hakuishii pale darasani kusimama kama kweli unataka wanafunzi wafaulu. Una watu hawa 1,000 ufundishe, ukimaliza kufundisha haki bin haki inapaswa uwasimamie je, wameelewa? Wameelewa, umewapa zoezi wamefanya. Ili ujue wameelewa ni lazima nisahihishe. Lazima nisahihishe na hakuna somo linalotaka kusahihisha kama somo la hesabu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kama hausahihishi unajuaje kama watoto wako wameelewa? Nitasahihishajke mimi wanafunzi 1,000 mimi siwezi wala wewe Mheshimiwa Spika huwezi wala mwingine hawezi? Huo ndiyo uhalisia. Watoto 1,000 leo niingie nisahihishe madaftari 1,000 kesho niingie nisahihishe madaftari 1,000. Mimi Tunza Issa Malapo siwezi wala mtu mwingine hawezi. Kwa hiyo tusikae tukatafuta mchawi, kaangalieni matokeo ya form four, kuna shule ipo inaitwa Taifa, wanafunzi 1,032. Form four, yaani darasa moja, management inakuwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mimi nachotaka kushauri, tunakaa hapa tunasema madarasa mengi yamejengwa, ndiyo yamejengwa lakini hayatoshi kwa sababu kila siku population inaongezeka. Population ya mwaka jana si ya mwaka huu. Kwa hiyo jitihada za makusudi bado zinahitajika kuwekeza katika elimu kuanzia kwenye miundombinu, waalimu na hawa waalimu hawa; unajua katika maisha hamna kitu kibaya kama kufanya kazi wakati una stress, asikudanganye mtu. Yaani wewe unatamani wanafunzi wako waelewe, ukiingia darasani unakutana na wanafunzi 1,000 unafundisha unajiona kabisa mimi hapa sijaeleweka, inaumiza sana kama mwalimu mwenye wito kama nilivyo mimi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, suala lingine nalotaka kusema kuhusu mgogoro wa ardhi wa hapa Dodoma. Mgogoro huu ni mkubwa sana, wananchi wanalalamika, wamedhulumiwa. Sisi kama Bunge, kama Kamati tumetoa ushauri. Ukisoma kwenye maoni yetu tumeeleza. Tunaomba Serikali ifanyie kazi kwa usimamizi wetu sisi Bunge kwa sababu Bunge kazi yetu ni kuisimamia na kuishauri Serikali.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.