Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa nafasi uliyonipa ili nami niweze kuchangia katika hizi kamati mbili. Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kukabiliana na wanyama wakali tembo. Suala hili ni suala kubwa, katika Wilaya yangu ya Meatu, wananchi waliouwawa na tembo kwenye Jimbo la Kisesa na Jimbo la Meatu kwa maana ya Wilaya ya Meatu. Wananchi waliouwawa na tembo ni 18, wananchi waliojeruhiwa ni tisa, mashamba yaliyoharibiwa ni 2,086 na nyumba zilizobomolewa ni 480. Mazao yaliyoliwa nyumbani ndani ya majumba ya wananchi ni tani 150.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili tunapolizungumza ni suala nyeti, suala ambalo lina tatizo kubwa la wananchi wetu na tunataka kwa kweli majibu sahihi ya Serikali namna ya kupambana na hawa wanyama wakali. Taarifa hapa imeandikwa, Serikali inapambana na wanyama, inafanya doria kupambana na hawa wanyama lakini inajenga vituo. Suala la kujenga vituo nilipongeze kwa sababu katika Jimbo langu la Kisesa, vituo viwili vimejengwa, Kituo cha Ng’anga pamoja na Kituo cha Marwiro. Vinajengwa na viko hatua ya kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu kubwa ni kwamba hizi doria zinazozungumzwa na Serikali zinaendeshwa wapi? Mbona mashambulizi ya wanyama hawa hasa tembo ni makubwa kiasi hicho? Je huyu TAWA ambaye kazi yake ni kupambana na hawa wanyama kuwadhibiti wasiingie kwa wananchi ametengewa bajeti kiasi gani? Fedha zilizotengwa katika hiyo doria kwa sababu doria lazima uwe na fedha, magari, mafuta na vifaa. Sasa hawa tembo tunakwenda kupambana nao kwa namna gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaitaka Wizara ituambie leo, lini itakomesha tatizo la tembo kwa wananchi ambao wanahangaika nalo kila siku? Watu wanauwawa kila leo, kipaumbele chetu ni nini? Lazima Wizara leo ituambie namna inavyoenda kushughulikia jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo la migogoro ya ardhi. Migogoro ya ardhi hii kila mahali, wahifadhi, wakulima, wafugaji wanapigana kila leo. Kila leo wanapigana na baadhi ya watendaji wa Serikali wamegeuza mtaji wa haya mapigano na hawako tayari kuona haya mapigano yamekwisha kwa sababu wamegeuza kuwa mtaji unaowapatia fedha. Wamegeuza kuwa ATM. Kwa hiyo, migogoro hii hawako tayari migogoro iishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano mmoja, suala la mipaka na alama zinazoonekana kwenye hifadhi zetu umekuwa ni wimbo wa miaka nenda rudi. Maeneo mengi hayajapimwa, alama hazijawekwa, mipaka inayotenganisha shughuli ya wananchi na shughuli za wakulima na wafugaji wataachaje kugombana na kupigana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni utanuzi holela wa hifadhi. Kumekuwa na utaratibu tu watu wanaweza kutanua tu unashtukia GN imetangazwa ambayo siyo shirikishi, maeneo yanatanuliwa, maeneo ya wafugaji yanachukuliwa, maeneo ya wakulima yanachukuliwa, migogoro itaisha lini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni maeneo mengi ya wafugaji yanageuzwa kuwa hifadhi, yanageuzwa kuwa WMA, wafugaji kila leo maeneo yao yametaifishwa, migogoro itakwisha lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukamataji holela wa mifugo, mtu anakamata tu mifugo inakamatwa kiholela, inauzwa kiholela na wananchi wamelalamika muda wote mifugo mingine inafungiwa bila maji, bila malisho mpaka inakufa. Sheria za Mifugo zipo zinazozuia hayo lakini watu wanavunja sheria makusudi kwa kisingizio cha uhifadhi. Haya mambo yatamalizika lini na wananchi wakawa kwenye hali nzuri? Mahusiano yatapatikana lini kama wengine wanashinda kesi mahakamani kama wafugaji, zaidi ya ng’ombe 6,000 wameshinda kesi mahakamani lakini hazijarejeshwa mpaka leo. Mahusiano utayapata wapi ya wakulima na wafugaji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, faini kubwa zinazotozwa hasa kwa wafugaji, ng’ombe mmoja kutozwa faini ya shilingi 100,000 ambayo hata kwenye sheria haipo. Leo Mwenyekiti wa Kamati atuambie hizi faini Wizara ya Maliasili wanaitoa wapi ya kutoza shilingi 100,000 kwa ng’ombe mmoja ambayo ni karibia 30% ya thamani ya ng’ombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, gari likipata shida, basi la Milioni 300 likipata matatizo litatozwa faini ya Shilingi 30, ngo’mbe wa shilingi laki tano anatozwa faini ya shilingi laki tatu…

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hatutaki mifugo nchi hii si tuseme kuliko kuwanyanyasa wafugaji kiasi hicho, kuliko kuwaonea Wafugaji kiasi hicho? Sheria za mifugo ziko vizuri…

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Mpina.

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, The Animal Welfare iko vizuri, Kanuni zinazozuia manyanyaso haya ya mifugo ziko vizuri, kwa nini sheria zinazoangaliwa ni Sheria za Uhifadhi tu na Sheria za Mifugo zikitelekezwa? Leo Mwenyekiti wa Kamati atuambie manyanyaso hayo yanafanywa chini ya misingi gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafugaji wetu wamekuwa wakipata shida kubwa maeneo mbalimbali, nenda huko Ilunde kule Kigoma, Mwandubanu, Kisesa Jimboni kwangu kule mpakani mwa hifadhi, manyanyaso ni makubwa! Nenda huko Serengeti, nenda Tarime, nenda hata huko Mbarali majuzi hapa wakulima unafika msimu wa kilimo wanaambiwa ondokeni hapa, mambo haya hayakubaliki! Mwenyekiti atupe maelezo ya kina juu ya masuala haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mfumuko wa bei. Suala la mfumko wa bei tukiendelea kupokea taarifa za kwamba eti! mfumuko wa bei umesababishwa na COVID-19, eti! mfumuko wa bei umesababishwa na vita ya Ukraine na Russia tukakubaliana na hayo, mfumuko wa bei unaowatesa wananchi wetu hatuwezi kuutatua. Mfumuko wa bei kwa sehemu kubwa mimi nakubaliana na hizo sababu lakini sababu kubwa za mfumuko wa bei kama nilivyosema tumezitengeneza wenyewe. Kama tumezitengeneza sisi wenyewe tuondoe mfumuko wa bei sisi leo katika Bunge hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumuko wa bei wa nchi hii umesababishwa na mambo makubwa mawili; Moja, usimamizi dhaifu wa sheria; Pili, usimamizi hafifu wa sera za fedha mambo mawili tu. Nasema hayo kwa sababu gani? Huwezi uka-control mfumuko wa bei kama unaweza kufanya malipo, kama usimamizi wako wa bejeti hauko sawasawa. Unaweza kufanya malipo ambayo ni nje ya bajeti, Bilioni 350!

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bilioni 350 tumemlipa Symbion fedha ambazo hazimo kwenye bajeti, huwezi kupata utulivu wa inflation katika mazingira ya namna hiyo. Pia kama huwezi kupeleka fedha zilizopangwa kwenye maeneo husika hasa kwenye sekta muhimu kama ya kilimo, jana tumeambiwa mpaka Februari hii ni asilimia 17 tu ya fedha zilizopelekwa uta-control vipi mfumuko wa bei?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuingia mikataba mibovu. Unaingia mkataba mbovu kama mkataba ulioingiwa wa TRC pamoja na CCECC wa Trilioni 6.34 mkataba ambao una mashaka, una malipo yenye mashaka ya zaidi ya Trilioni 1.7 halafu ukategemea kwamba utapata utulivu wa fedha nchini, halafu ukategemea kwamba uta-control inflation haiwezekani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sera za kodi, ukawa na sera za kodi hapa. Tumekuwa na sera za kodi za mpaka unaenda unawasamehe wawekezaji mahiri, unasema hawa ni wawekezaji mahiri ukawasamehe kodi zote, kodi ya VAT, corporate tax zote umewasamehe halafu maskini akaendelea kutozwa kodi zote zinazotakiwa kutozwa mpaka tozo, lakini Tajiri huyu ameambiwa kwamba amesamehewa kodi halafu ukafanikiwa kwa nchi yenye …

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi uka-control inflation katika mazingira hayo.