Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA URATIBU): Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na nianze kwa kuzipongeza Kamati zote mbili; Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji pamoja na Kamati ya Miundombinu kwa kuwasilisha hoja zao leo asubuhi na kwamba tumepata michango ya kutosha. Kusema kweli Kamati hizi zinafanya kazi nzuri sana. Nianze kwa kuunga mkono hoja za Kamati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo, nina maoni katika maeneo mawili. Kwenye mapendekezo ya Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kwenye aya ya 3.3, ukurasa wa 60, limetolewa pendekezo linalohusiana na kuimarisha dhana ya ushirika nchini. Katika pendekezo hilo, Kamati imesema Serikali ilete Bungeni marekebisho ya sera na sheria za ushirika; wamezitaja na zile sheria.

Mheshimiwa Spika, nataka kushauri azimio hili lirekebishwe kidogo ili kusiwe kuna ulazima wa Serikali kuleta sera humu Bungeni kwa sababu siyo utaratibu. Kwa hiyo, isomeke, “Serikali iangalie upya au ipitie upya Sera ya Ushirika nchini ya mwaka 2002 na kuleta marekebisho ya sheria.” Isomeke hivyo, litakuwa azimio linaloweza kutekelezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo la pili linahusiana na pendekezo la aya ya 3.6 ambayo imeelezea umuhimu wa kuwa na chombo cha Kitaifa cha Kudhibiti, Kuratibu na Kusimamia Kipango ya Kaendeleo ya nchi yetu. Ilikuwa ni concern kubwa ya Bunge hili hata wakati wa Bunge letu la Bajeti, walieleza haja ya kuwa na Planning Commission (Tume ya Mipango) ambayo kama kumbukumbu tunazo, basi tunakumbuka tuliivunja na kufuta ile sheria mwaka 2018.

Mheshimiwa Spika, maoni haya kwa sababu yametolewa na safari hii yamekuja kwa mapendekezo ya Azimio la Kamati, nataka tu niwape taarifa Waheshimiwa Wabunge na Kamati inayohusika kwamba Serikali ililichukua jambo hili kwa uzito mkubwa toka wakati ule na kwamba Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wiki hii kama siyo wiki iliyopita, aliagiza tuanze mchakato wa kuunda Tume ya Mipango. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama ingekuwa siyo kuvunjwa kwa sheria ile kwa uzima wake, tulitaka tutafute namna ya urahisi wa kwenda kwenye hiyo, lakini kwa kuwa mchakato wake ni lazima uanze kutoka mwanzo, ianze sheria, tupitie stages zote, tunatarajia mpaka kwenye Bunge la mwezi wa Nne angalau tufanye first reading. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pengine ikilipendeza Bunge lako na kwa mamlaka uliyonayo, tunaweza tukaenda kwa speed utakayoona inafaa ili tuweze kuwa na Planning Commission katika nchi, itusaidie kupanga mipango yetu hii mikubwa ambayo kwa kweli tunaitekeleza, lakini unaiangalia uratibu wake hauna chombo kikubwa chenye uzito wa Kitaifa wa kuweza kuratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilitamani nichangie maeneo haya mawili, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wa Kamati husika kwa michango mizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)