Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili nami niweze kuchangia hoja ya Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Bunge, hasa ya Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, nawashukuru sana Kamati ya Miundombinu wakiongozwa na Mheshimiwa Selemani Kakoso na Makamu wake Mheshimiwa Anne Kilango na Wajumbe wote kwa jinsi ambavyo wanatushauri sisi kama Wizara na kutoa maelekezo.

Mheshimiwa Spika, bila kupoteza muda, naomba sasa nijielekeze kwenye mchango wangu hasa kutokana na maoni ya Kamati. Nilisikia Kamati kwamba karibu mambo yote ambayo walikuwa wametuelekeza tunaendelea kuyatekeleza, nami nataka nitoe mchango kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu muundo wa TBA ili iweze kufanya na sekta binasfi; Machi, 2022 wakati Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anazindua Mogomeni Quarter, moja ya jambo ambalo analieleza, ni kueleza Wizara na TBA kwamba waangalie uwezekano wa TBA kufanya kazi na sekta binafsi. Hivi ninavyoongea, tayari muundo wa TBA umeshakuwa reviewed kwa maana ya establishment order, pamoja na majukumu yake yote ambayo ilikuwa inayafanya, lakini pia sasa itaanza kufanya na sekta binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, sasa hivi kwa maana ya taratibu zote tunasubiri tu baraka za mamlaka ambayo ndiyo ilitoa hayo maelekezo pamoja na Kamati ya Miundombinu. Hivyo, tuna uhakika suala hili liko mwishoni na itakuwa hivyo, kufanya kazi na sekta binafsi ikiwa ni pamoja na majukumu yake yote iliyokuwa inayatekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, limejitokeza pia suala la TANROADS kuachia kazi kwenda TAA. Nataka kulijulisha Bunge hili kwamba hilo suala pia wataalam wameshashauri. Ni kweli kwamba TANROADS itaachia shughuli zote kwenda TAA lakini kwa hatua. Kwa sababu gani? Kwa sababu shughuli zote ambazo zilikuwa zimeingiwa mikataba na TANROADS, zitaendelea kufanyika kwa sababu ya mikataba yake, huku kama walivyoshauri wataalam, TAA ikianza kuchukua kazi.

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara, kwa sababu taasisi zote ziko chini ya Wizara, hilo tumeshalikubali na litakwenda kutekelezwa hivyo, lakini kwa muda ili tusije tukaathiri miradi ambayo inaendelea ambapo tayari TANROADS walishaingia mikataba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu TEMESA, tayari Kamati ilishashauri kwamba Serikali iangalie muundo na utendaji kazi wa TEMESA na Serikali inaendelea kulifanyia kazi hilo. Kwa hiyo, nataka nilihakikishie Bunge hili kwamba tunaendelea kulifanyia kazi kama alivyoshauri Mheshimiwa Dkt. Ndugulile. Tayari Serikali ilishaliona na Kamati ilishashauri na tayari kazi inaendelea kuunda upya majukumu yake na muundo wake ili kuleta tija.

Mheshimiwa Spika, suala la fidia ya Itoni – Lusitu – Mawenge – Ludewa hadi Manda; ninapoongea sasa hivi, ni mama mmoja ambaye hajapata ambaye hakuwepo, na mtu mmoja, nyumba Na. 45 Kijiji cha Mlangali ambaye baada ya realignment alisahaulika, lakini fedha yake ipo na atalipwa wakati wa kulipa watu wa kati ya Mradi wa Itoni kwenda Lusitu ambapo jedwali liko tayari. Kwa hiyo, tumetekeleza yale maagizo ya Kamati.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Hazina kuipatia fedha TBA; kwa kweli kwa sasa Hazina imeendelea kutoa fedha nyingi na ndiyo maana tunaona sasa hivi majengo mengi TBA yanajengwa, pamoja na ruzuku ambayo TBA wanaitoa ya kujenga majengo kwa ajili ya wafanyakazi na nyumba za Serikali.

Mheshimiwa Spika, mwisho, kuhusu bajeti…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Sekunde 30.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, utakubaliana nami kwamba katika kipindi ambacho Serikali inalipa wakandarasi, ni kipindi hiki. Ndiyo maana miradi mingi inakwenda. Hata ukiwauliza wakandarasi, kwa kweli ni tofauti na ilivyokuwa na ndiyo maana miradi mingi inalipwa. Kadri tunavyotengeneza certificate kwa kweli Wizara ya Fedha inalipa na ndiyo maana tumekuwa kati ya Taifa ambalo yanafanya vizuri sana katika miundombinu kwa Afrika Mashariki na hasa miundombinu ya barabara.

Mheshimiwa Spika, mwisho, kuhusu madeni ya TBA, tayari pia lipo kwenye ngazi za juu kwa maana ya kwamba wale wadaiwa sugu na hata taasisi ndani ya Serikali, mpango umeandaliwa kati ya Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Fedha na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kuona namna bora ya madeni yote yaweze kulipwa. Kwa hiyo, nina hakika hili nalo litafanyika ili kuipa uwezo TBA kupata madeni yake kwa ajili ya kuiimarisha kuweza kutimiza majukumu yake.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. Ahsante. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana. Hebu tusaidie kufafanua moja lile la uwezo wa kampuni za hapa nchini kuweza kutengeneza meli na kutengeneza vivuko halafu zisiweze kukarabati. Au ni ule utaratibu wa sheria yetu kwamba mlifanya hiyo International Competitive Tendering, kwa hiyo, akashinda yule? Hebu tueleweshe vizuri hapo.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Moja ulilolisema ndiyo hilo kwamba mikataba mingi huwa inatangazwa kwa maana ya kwamba iko wazi Kimataifa na mtu yeyote anaweza aka-tender. Pia tuna kampuni za Tanzania ambazo kwa kweli siyo nyingi.

Mheshimiwa Spika, moja ya kampuni ambayo inafanya vizuri sana ni Songoro Marine, Iakini tunaona kazi nyingi ambazo anazifanya kwa sasa hivi ni nyingi sana.

Nasi ni kati ya watu ambao tunam-promote sana. Kwa hiyo, kutokana na hilo tukaona pengine atachelewa zaidi kwa sababu ya taasisi yake na watu alionao. Kwa hiyo, naamini kwamba kama tungempa hiyo kazi pengine angeweza kuchukua muda mrefu kuifanya. Ila ni tenda iliyotangazwa kwa maana ya kwamba iko wazi kwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)