Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kidogo taarifa zilizowekwa mbele ya Bunge lako leo. Nichukue nafasi hii kulipongeza Bunge kwa kazi nzuri ya kuisimamia Serikali kupitia Kamati hizi mbili; Kamati ya miundombinu na Kamati ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, specific kwa Kamati ya Miundombinu, kwa Taarifa yake, nichukue nafasi hii kuwapongeza sana Kamati hii kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wanaifanya katika kipindi cha Taarifa hii chini ya Mwenyekiti Ndugu Kakoso ,Makamu Mwenyekiti Mama Anna Kilango na Wajumbe wake, wanafanya kazi nzuri sana ya kuisimamia Serikali na kushauri. Mafanikio tunayoyaona ni matokeo ya ushauri mzuri na kazi nzuri inayofanywa na Kamati hii kwa niaba ya Bunge. Kwahiyo tunawashukuru sana Kamati kwa kazi nzuri waliyofanya.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza na kumshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwanza kwa msukumo wa kipekee aliyouweka kuhakikisha Sheria ya Taarifa Binafsi inatungwa na kuletwa Bungeni; na nalishukuru Bunge lako kwa kuipitisha Sheria ile. Pia namshukuru kipekee Rais kwa kuisaini kwa wakati na sasa iko tayari kuanza kufanya kazi. Wizara tunakamilisha Kanuni zitakazoiwezesha Sheria hii kufanya kazi. Sheria hii imetupa heshima duniani, imetuingiza katika nchi salama mtandaoni kwenda kuwekeza na kufanya shughuli. Kwakweli Mheshimiwa Rais ametutendea haki katika jambo hili na tuna sababu za kumpongeza na kulipongeza Bunge lako kwa kutunga Sheria hii. Sheria hii itakapoanza kufanya kazi tunahakika usalama mtandaoni utakuwa mzuri. Wakati tunakwenda kutunga kanuni tutawashirikisha wadau ili washiriki kuhakikisha kanuni hizi zinatungwa vizuri, zinaendana kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na kuhakikisha mtandao wetu unakuwa unakuwa salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili niishukuru Kamati na nilishukuru Bunge lako. Inavyoonekana kwa kauli moja wameunga mkono uwamuzi wa kufungia simu ambazo haziko halali katika mtandao wa nchi yetu. Kwa mahesabu ambayo tumeendelea kuyatoa mpaka jana tulikuwa na simu takriban million mbili na kitu ambazo hazijahakikiwa. Tunaendelea kutoa hizi siku mpaka tarehe 13. Tunaamini kwa kauli moja, kwakuwa tumekubaliana kudhibiti uhalifu kwenye mtandao basi tunashukuru kwa endorsement iliyopatikana; na tarehe 13 Mwezi 2 saa kumi jioni kama kuna simu itakuwa haijahakikiwa hatutasogeza muda tutaifunga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa usalama wa mtandaoni unategemea Sheria, unategemea mifumo lakini unategemea pia usimamizi. Tumeongeza usimamizi kwenye baadhi ya maeneo, Sheria zimetungwa na tunaendelea kuzitunga na mifumo inaendelea kuwekwa. Hapa pametokea malalamiko na yamekuwa yakizungumzwa na Kamati imegusia. Bado kuna message nyingi ambazo watumia huduma za mawasiliano wanazilalamikia, kwamba zinatumwa kwao bila wao kutaka wala kuziomba; na message nyingi zinahusiana na biashara na biashara zenyewe za hovyo, biashara za waganga wa kienyeji mambo ya betting sijui mambo ya kuhamasisha biashara zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Sheria iko wazi, na kwenye hili nataka kuchukua nafasi hii kuwataka TCRA, nadhani tumevumiliana vya kutosha, sasa tuchukue hatua tukomeshe jambo hili. Watu wamelalamika sana inatosha, tunaharibu jamii yetu. Watu wanatumia taarifa za watu, wanawatumia message ambazo kwa kweli zimegeuka kuwa usumbufu. Hili jambo limezungumzwa kwa kina hapa na sisi kama Serikali tunalipokea, na kupitia TCRA hii ndiyo kauli ya mwisho, tunataka hili jambo likome. Tumezungumza, tumevumiliana, imefika wakati sasa inatosha. Watoa huduma za mawasiliano, kwasababu message, zinapitia kwao. Mtoa huduma ambaye ataruhusu jambo hili sasa tutachukua hatua na bila shaka ndiyo itakuwa suluhisho la jambo hili. Inatosha, message zimekuwa nyingi. Kwa hali ilivyo tukiendelea kuruhusu jambo hili nadhani tutakuwa hatuwatendei haki watumia huduma za mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, baada ya kupitisha Mfumo wa Anuani za Makazi, na bahati nzuri kamati imezungumza vizuri, kwamba mfumo huu utaendelea kujengwa, utaendelea kuhimarishwa na kuboreshwa. Tuko hatua za mwisho za mchakato wa kutunga kanuni, na pengine sheria za kuufanya sasa mfumo huu uwe katika matumizi ya kawaida. Sasa hivi unaweza usione effect yake kwa sababu bado hakuna kanuni za kuufanya utumike. Tunakoelekea huduma nyingi zitatolewa kwa kuzingatia pia Mfumo wa Anuani za Makazi; na hii itarahisisha sana utoaji wa huduma.

Mheshimiwa Spika, suala la mwisho kwenye ripoti imezungumzwa changamoto tuliyonayo hasa kwenye mipaka ya nchi yetu, suala la huduma za mawasiliano lakini pia suala la usikivu wa shirika letu la utangazaji.

Mheshimiwa Spika, pamoja na bajeti yake kuwa ndogo lakini hivi tunavyoongea tuko kwenye hatua za mwisho za kukamilisha makubaliano kati ya TTCL na TBC ili kuwawezesha TBC watumie minara ya TTCL kupeleka huduma ili tukabiliane na changamoto ya uwekezaji wa minara kwa shirika letu la utangazaji. Tunaamini jambo hili likitekelezwa litaongeza usikivu wa shirika letu. Hivi leo tunavyoongea, tarehe 31/01/2023, ile minara 763 tenda yake imefunguliwa leo. Tunaamini baada ya hapa tutatengeneza mchakato mzuri. Niahidi mbele ya Bunge lako, siku tutakapowakabidhi wajenzi tutaomba kibali tukutane Wabunge wote tukiwa hapa ili tushuhudie kukabidhiwa hawa wanaokwenda kujenga, na kila mmoja amuone nani anakwenda kujenga kwenye eneo lake ili isaidie ufuatiliaji, na bila shaka itapunguza tatizo tulilonalo la Mawasiliano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono Hoja za Kamati. Nakushukuru sana. (Makofi)