Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi nichangie katika hoja hizi mbili, kwa maana ya hoja ya Kamati ya Kilimo, Uvuvi na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Mimi kwa sababu ya muda nitaongelea hoja mojawapo tu hii hoja ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, Kamati hii imefanya kazi nzuri sana kwa sababu Kamati hii inaishauri Serikali kwa niaba ya Wabunge wote. Katika ushauri wake kwenye maoni na mapendekezo ya Kamati, kuna mahala Kamati hii imesema categorically kwamba, sababu mojawapo ya kwa nini miradi mingine ya Serikali inashindwa kutimia ni sababu ya ufinyu wa bajeti ya baadhi ya taasisi. Imetoa mfano mojawapo kama TANROADS.

Mheshimiwa Spika, napenda kuongezea kwenye ushauri ambao Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeshauri. Kwa mfano, tunafahamu vizuri kabisa duniani kwamba resources are limited but needs are unlimited. Kwamba vyanzo vina ukomo lakini mahitaji hayana ukomo. Kwa hiyo ni ushauri wangu kwamba, Wizara hii inapokuwa inapanga taratibu zake za ujenzi wa barabara iwe inatumia Kanuni ambayo tunaita Kanuni ya kipaumbele au the principle of priority.

Mheshimiwa Spika, nitoe mfano kwenye Kanuni ya kipaumbele, kwamba resources are very limited but needs are unlimited. Kwamba tunakuwa na vyanzo vilevile lakini mahitaji ni mengi kuliko vyanzo, kwa hiyo lazima uwe na sheria ya kutoa kipaumbele uanze na nini, umalizie na nini kutegemea na umuhimu wake kwa wakati wake. Kwa mfano, kuna barabara inayotoka Tegeta inapanda mpaka Kiwanda cha Wazo Hill - Kiwanda cha Cement mahala ambapo, ni barabara ina urefu kama wa kilomita Tatu au Nne hivi. Kama unavyojua kiwanda hiki cha Wazo Hill kilijengwa tangu 1966. Wakati kiwanda hiki kinajengwa wananchi walikuwa hawakai hayo maeneo ya Tegeta, maeneo ya Madale lakini sasa kiwanda kimejengwa na wananchi wanakaa, barabara hii ni nyembamba kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unapojaribu kujiuliza ni kwa nini hii barabara haijajengwa? Nikupe takwimu za kweli kutoka kiwandani. Kiwanda hiki kinatoa corporate tax kwa mwaka zaidi ya Bilioni 100, narudia tena Bilioni 100 corporate tax kwa mwaka, lakini barabara yake ni nyembamba kiasi kwamba mwaka huu tu tulioumaliza 2022 zaidi ya watu 10 wameuawa pale kwa ajali kwa sababu barabara ni nyembamba malori yanapangana kutoka kiwandani kuja pale Tegeta na yanasababisha ajali si za kawaida.

Mheshimiwa Spika, sasa unaweza kujiuliza, kama kiwanda hiki kinaipa Serikali ushuru Bilioni 100 corporate tax kwa mwaka, kuna tatizo gani kwa Serikali kupanua barabara hii ili malori yatembee na ipate ushuru zaidi. It’s very simple principle kwamba huyu ng’ombe ambaye anakupa maziwa, unampa majani ya kutosha ili upate maziwa zaidi ununue ng’ombe wengine. Lakini kwa kutokujua kanuni ya priority ni kwamba barabara hiyo haijajengwa, matokeo yake malori yanapangana kutoka Tegeta kiwandani yanafika pale mpaka Tegeta barabarani hayawezi kwenda. Kumbe kama tungeweza kupanua barabara hii kwa kuangalia priority hawa watu wanaotulipa Bilioni 100 kwa mwaka wangekuwa wana uwezo wa kulipa zaidi ya pale na tungejenga barabara nyingine zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mimi naishauri Serikali kwamba, it is very important and crucial kuwa tunaangalia priority tuanze na nini ili kitupe nini kwa ajili ya kujenga mahali pengine, hili ni jambo la muhimu sana. Inashangaza kwamba imekuwa kero kubwa sana kwa watu wa pale kwa sababu watu wanauwawa kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo jingine la kuangalia ni muhimu sana TANROADS au na Wizara hii wakati wanapanga bajeti zao waangalie priority. Kwa mfano, kuna bandari moja pale Mbweni barabara ya kwenda kwenye Bandari ya Mbweni, bandari ndogo mahali ambapo watu wanafanya biashara kati ya Zanzibar na Mbweni. Bandari ile ni ndogo tu lakini kwa mwezi inakusanya mapato Milioni 400, lakini ile barabara tu ya kwenda bandarini haipo kiasi kwamba watu wanatumiwa ng’ombe. Yaani Mashekhe wangu pale lazima watumie ng’ombe kubeba mizigo yao. Can you imagine Dar es Salaam - Mbweni mahali ambapo Milioni 400 zinakusanywa kila mwezi, hakuna barabara ya kufika kwenye bandari hiyo lazima watu wabebe na ng’ombe, hizi milioni 400 zinaenda wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilikuwa nafikiri it is very crucial kutumia kanuni ya kipaumbele (the principle of priority) kwamba mahali panapozalisha tupatengenezee barabara ili pazalishe zaidi kwa ajili ya fedha za kuisaidia nchi yetu, hii it is a simple mathematics it doesn’t cost matrix, haihitaji matrix wala integration. Kwamba hapa wanalipa milioni 400 kwa mwezi lakini hawana barabara, gari haiwezi kufika bandarini, wanatumia ng’ombe ukifika pale ni Dar es Salaam lakini kwenda pale bandarini lazima utumie ng’ombe. Sasa kama wangekuwa wametumia magari tungezalisha zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo naomba sana kujaribu kuunga huu ushauri na Kamati ya Miundombinu kwamba ni muhimu sana kuangalia priority waanzie wapi ili tupate nini kwa ajili ya kupata nini pale baadae. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niendelee na palepale kuionesha Wizara hii kwamba wakitumia the principle of priority itawasaidia sana. Kwa mfano, pale Basihaya kuna mtaro wa maji, huu mtaro wa maji, maji huwa yanajaa yanaporomoka kutoka juu yanaua watu kila mwaka. Kila mwaka watu wanauawa kwa sababu ya mtaro wa Basihaya mpaka Nyamachabes. Serikali ilishafanya tayari study pale kuonesha kwamba TANROADS wanatakiwa kujenga mtaro wa ku-deliver maji kwenda baharini.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais alipopita pale aliahidi akasema mtaro huu utajengwa. Haya sasa siyo maendeleo, haya ni kuokoa maisha ya watu wanaoangamia kwa ajili ya mafuriko wakati wa mvua. Inashangaza sana, unakuta eneo lile lilikuwa na tatizo la maji kwa maana kwamba watu hawana maji, wakati huo huo lina tatizo la mafuriko ukimwelezea mtu hawezi kukuelewa. Una tatizo la upungufu wa maji, wakati huo huo una tatizo la mafuriko anakwambia akili yako ina matatizo. Hii ni kwa sababu ya kutokujua priorities, tuanze na nini, tufuate na nini ili tupate nini hapo baadae. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie tu bila kuchukua muda wako mwingi kwamba ni muhimu sana hii Kamati ya Miundombinu imeshauri jambo zuri kwamba Serikali ni vizuri sana iweke priorities mahali ambapo panatupa return kubwa tuwekeze zaidi ili tupate return ya kutosha kwa ajili ya kuijenga nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho kwenye hilo hilo. Kuna barabara inayotoka Bunju ‘B’ kwenda Mabwepande inaenda mpaka Kihonzile, inakwenda kuunga mpaka ile barabara ya stendi ya Mbezi mwisho. Ukiangalia kwenye priorities hizo hizo kwamba Wizara hiyo inafanya priority barabara hiyo inatokea Mbezi Luis inakuja kwenye Jimbo la Kawe kupita Mabwepande mpaka Bunju B. Ingejengwa ungeona badala ya mabasi kutoka Morogoro yakaingia Ubungo Mjini yangekuwa yanapita moja kwa moja yanatokea Mabwepande na hata ile maana ya kujenga Bandari ya Bagamoyo mtu angetoka kule aka-connect moja kwa moja kwenda Morogoro. Kwa hiyo ni muhimu sana Wizara ichukue ushauri wa Bunge kwamba tuangalie priority tunapofanya mambo yetu kwa sababu resources are limited but needs are unlimited.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)