Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. George Mcheche Masaju

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kupata fursa ya kuchangia kwenye hoja hii muhimu na nakushukuru wewe kwa kunipa fursa hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa hotuba yake nzuri na mipango mizuri kwa ajili ya Jeshi hili la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania. Pia niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa michango yao ya kuboresha hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kutoa ufafanuzi wa masuala mawili, matatu hivi ya kikatiba na kisheria ambayo yamejitokeza hapa. Moja, linahusu utumishi wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetajwa na Ibara ya 1 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kwamba ni nchi moja nayo ni Jamhuri ya Muungano. Ibara ya 2 ya Katiba inasema:-
“Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo”.
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kupata fursa ya kuchangia kwenye hoja hii muhimu na nakushukuru wewe kwa kunipa fursa hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa hotuba yake nzuri na mipango mizuri kwa ajili ya Jeshi hili la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania. Pia niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa michango yao ya kuboresha hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kutoa ufafanuzi wa masuala mawili, matatu hivi ya kikatiba na kisheria ambayo yamejitokeza hapa. Moja, linahusu utumishi wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetajwa na Ibara ya 1 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kwamba ni nchi moja nayo ni Jamhuri ya Muungano. Ibara ya 2 ya Katiba inasema:-
“Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo”.
Mikoa, kifungu cha tano (5) kinataja majukumu ya Wakuu wa Mikoa, naomba kunukuu:-
“(1) Mkuu wa Mkoa atakuwa mwakilishi mkuu wa Serikali katika eneo la mkoa ambalo ameteuliwa na kwa madhumuni hayo majukumu yote ya kiserikali yanayohusu mkoa huo yatatekelezwa na/au kupitia Mkuu wa Mkoa.
(2) Katika kuendeleza madhumuni na masharti ya kifungu kidogo cha (1) Mkuu wa Mkoa atakuwa na wajibu wa kusimamia utekelezaji wa sheria na uwepo wa amani katika mkoa huo, kutoa mwelekeo mahsusi wa sera za jumla za Serikali katika mkoa na kutekeleza kazi na majukumu mengine kama yanavyotekelezwa au kutolewa kwake na/au chini ya sheria hii au sheria nyingine yoyote”.
Mheshimiwa Naibu Spika, utaona kwamba hawa hawahusiki kabisa na shughuli za vyama vya siasa. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge waamini kama Serikali ilivyokwisha kufafanua hapa kwamba, hawa ambao Katiba imewapiga marufuku kuwa wanachama wa vyama vya siasa kama Wanajeshi, hata wanapoteuliwa kuwa Wakuu wa Wilaya au Mikoa, hawawezi kuwa Wajumbe wa Kamati za Siasa za Kamati za Halmashauri Kuu za CCM.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa hivi hakuna sheria yoyote katika hizi ambazo zimeshatungwa zinazotoa majukumu kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya kujihusisha na vyama vya siasa. Kimsingi wanapoteuliwa, mara ya mwisho nilishuhudia pale Ikulu Mheshimiwa Rais alipowateua hawa Wakuu wa Mikoa wa mwisho wakiwemo na Wanajeshi, aliwakabidhi katiba na sheria. Hata Wakuu wa Wilaya wanapoapishwa kule na Wakuu wa Mikoa wanakabidhiwa katiba ya nchi na sheria, hawakabidhiwi hizi katiba za vyama vya siasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kushauri tu kwamba, hili ambalo linaleta wasiwasi humu ndani Waheshimiwa Wabunge hawana sababu ya kuwanalo. Jeshi letu lina watu wanaheshimika sana, wana nidhamu kubwa sana, wana utii mkubwa sana, hawawezi wakakiuka masharti ya Amiri Jeshi Mkuu. Mkiangalia sehemu yao kubwa wanapelekwa katika maeneo ambayo yana matatizo ya ulinzi na usalama. Hawa Maafisa wa Jeshi walioteuliwa wamekwenda kwenye maeneo yale ambayo yana matatizo makubwa ya usalama. Ukiisoma ile Sheria ya Tawala za Mikoa unaona kabisa mojawapo ya majukumu yao ni kusimamia ulinzi na usalama katika maeneo yao ya utawala.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja.