Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. TOUFIQ SALIM TURKY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza naomba nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu Sub-hanau Wataallah kutujaalia mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani uwe salama na baraka kwa Taifa zima, pia nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lililopita tulikuwa tunahojiana sana katika suala la tozo, kila mmoja anapiga kelele tozo lakini sasa hivi toka tumekuja wote wamekaa kimya kwa sababu zile neema za tozo kila kona ya Tanzania zimefika. Hivi tunavyoongelea mpaka mimi kupitia Jimboni kwangu nina Skuli ya Sekondari sasa hivi hapa nina meremera na speed yake kali, kwa hivyo ninaipongeza sana kwa ubunifu na nakiri kuzitumia hizi pesa ipasavyo kwa kila Mtanzania kupata zahanati na skuli kila kona. Kwa hiyo, tunampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa maamuzi hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nataka niipongeze Serikali kwa kuja na suala la postcode na suala la sensa, mataifa yaliyoendelea haya masuala mengi pengine watu hawaelewi kwa nini hizi postcode na sensa ina umuhimu wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, postcode tunapata kujua kama kuna kifaa mtu yeyote unataka kumpelekea unajua njia gani, mtaa gani, nyumba gani, unampelekea unapata ile postcode na kwa kupitia sensa unajua ndani ya nyumba ile kuna watu wangapi, wana mahitaji ya aina gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kupitia hizi mbili ndiyo mataifa mengi yameweza kuendelea. Sasa hoja yangu au mchango wangu uko sehemu moja kwamba tunaweza tukawa na sensa tunaweza tukawa na postcode lakini kama hatuna mfumo wa kuwezesha watu kuitumia hizi postcode tutapata athari kubwa sana. Wenzetu sasa hivi wana database kupitia hii database ndiyo service industries wanapata kodi, leo kila siku tunatafuta tunabuni kodi kwa ajili ya mradi ndiyo maana vifaa bidhaa zinapanda bei, lazima sasa hivi tuondokane kwa mlaji tu tuende katika services.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ukitizama kuna mitandao ya booking.com kuna Airbnb, hatuna mfumo wa kuweza direct kupata hizi kodi. Watu wanalipa wanapata pesa zao Serikali inakosa kodi zile kwa kupitia watu kukodishwa.

Hali kadhalika kuna mataifa makubwa ya Google, Facebook wanafanyabiashara na watu wengi sana, sasa hivi tunafanya online purchase lakini kinachofanyika Serikali inakosa kodi zao. Ninachoomba sana tutafute mfumo wa kuhakikisha tunadhibiti kodi zetu kuweza kuzipata na hayo yote haitowezekana kama hatujawekeza katika elimu ya artificially intelligence.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliongelea Bunge lililopita na safari hii naongea tena, jamani dunia inapoelekea inaenda katika digital hakuna jambo hata moja linalotumika bila artificial intelligence, bado elimu yetu hatujawekeza katika artificial intelligence.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Rwanda wameanza kwa kuwa wanataka kuwa ni sehemu ya market ya AI sisi tuko wapi? Leo mpaka unamaliza University somo la coding hatujalianzisha wenzetu kuanzia Darasa la Sita coding inakuwa ni compulsory, lazima watu wafundishwe coding wanajua dunia ijayo haitakuwa na mikono tena itakuwa dunia ya akili lazima tuwekeze elimu yetu katika digitalization ni ombi langu mahsusi hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia tuna wenzetu walemavu wa kuweza kuzungumza na kusikia, tunafurahi sana kuwa sasa hivi television zote wanakuwa wanaweka sehemu kwa ajili ya watu kufahamu. Lakini ni lazima pia tuanzishe katika madarasa japo zile sign ndogo ndogo za kuweza kuongea nao mtu ana mahitaji yake haiwezekani mtu ana mahitaji leo, mahitaji yake mpaka akufanyishe kwa mkono hivi haipendezi tunawanyanyapaa! Kwa hivyo ninaomba sana kupitia sekta ya elimu tuanzishe at least kuwe na curriculum ya kuwa na masuala ya sign language lakini suala la artificial intelligence siyo tena suala la kulipuuza ni lazima lipewe kipaumbele chake, dunia ndipo inapoelekea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana naunga hoja. Ahsante sana. (Makofi)