Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na nichangie kwa kifupi sana. Nianze kwa kumpongeza sana Waziri wa Ulinzi, Mheshimiwa Dkt. Mwinyi kwa kazi nzuri anayofanya. Kazi hii anaifanya kwa unyenyekevu na uadilifu mkubwa tunakupongeza sana Dokta. Pia nilipongeze jeshi letu kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya. Nchi yetu inaendelea kusifiwa kuwa na amani na utulivu kwa sababu ya kazi yao nzuri wanayoifanya, ahsanteni sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama kuweka rekodi sawa, kwenye hotuba ya Kambi ya Upinzani, ukurasa wa 11, wamenukuu Katiba ya CCM, Ibara ya 80(1)(c) na 94(1)(c). Bahati mbaya sana na nadhani ni kwa makusudi, wamenukuu nusu ya Ibara hizo na wakaamua kwa makusudi kupotosha ukweli. Sasa nimesimama kuuweka ukweli sawa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wao wamenukuu Ibara ya 80(1)(c) lakini (d) inasema hivi, Mkuu wa Wilaya ambaye anatokana na CCM. Ukienda Ibara ya 94(1)(c) inasema, Mkuu wa Mkoa ambaye anatokana na CCM. Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya nafasi hizi zinateuliwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika Katiba na sheria zote zinazosimamia uteuzi huu sifa ya kuwa mwanachama wa chama cha siasa haipo. Kwa hiyo, mtu yeyote anaweza kuteuliwa kwenye nafasi hizi bila kujali chama chake cha siasa
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Sikilizeni, kwa utaratibu huo ndiyo maana katiba ya CCM imeeleza Wajumbe wa Kamati za Siasa ambao wao wanalalamikia kwamba hawa ni wajumbe imeeleza wajumbe hao ambao ni Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ambao wanatokana na CCM, siyo kila Mkuu wa Wilaya ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya CCM na siyo kila Mkuu wa Mkoa ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa na ushahidi upo. Tunao Wanajeshi ambao wameteuliwa kuwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya na kadri tunavyoongea sasa hakuna hata mmoja ambaye amehudhuria kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya wala ya Mkoa na ushahidi upo. (Makofi)
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishauri ni vizuri tusitumie Bunge hili kujaribu kupotosha ukweli na kujaribu kulipaka matope jeshi letu…
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Jeshi letu linafanya kazi nzuri, tuache unafiki, tunasimama tunawapongeza tunasema wanafanya kazi nzuri wakati huo huo tunatumia mlango wa nyuma …
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe mfano wa wazi kabisa kwa sababu bahati mbaya sana Bunge hili linataka kutumika kucheza siasa za hovyo. Alikuwepo Brigedia Jenerali Balele, aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga akiwa amestaafu. Alipofika Shinyanga akaenda Ofisi ya CCM, alipofika Katibu wa Mkoa alikuwa anaitwa Agusta Muba akamuuliza Jenerali wewe una kadi ya CCM? Huwezi kuingia kwenye vikao vya CCM kama wewe siyo mwanachama wa CCM. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya sana, mimi hapa sizungumzi kama Katibu Mwenezi, uenezi nilishaacha huko, wenzetu wamekuwa na utamaduni wa kutoheshimu Katiba za vyama vyao. Katiba ya CCM inasema Ukuu wako wa Wilaya, Ukuu wako wa Mkoa haukuingizi kwenye vikao hivi. Katiba ndivyo inavyosema na tunaisimamia. Isipokuwa uanachama wako plus Ukuu wa Wilaya na Ukuu wa Mkoa wako, kama siyo mwanachama huingii na hapa ninapozungumza tunao Wakuu wa Mikoa ambao ni Wanajeshi hawajastaafu na hawaingii kwenye vikao vya CCM. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni vizuri tukaweka rekodi sawa; ukizoea vya kunyonga vya kuchinja vinakua tabu. Acheni uwongo na kutaka kuwadanganya Watanzania kwa mlango wa nyuma. Liheshimuni jeshi kwa maneno na matendo yenu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.