Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALOSS NYIMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii ya kuchangia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kuchangia toka Bunge hili lianze, nimpongeze Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuchaguliwa na wananchi kwa kura nyingi. Pia nimpongeze Makamu wa Rais, Mheshimiwa Mama Samia kwa kuteuliwa, imani yetu wanawake hatatuangusha maana tuna uhakika na kazi anazozifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa wakati huu nimpongeze Mheshimiwa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Dkt. Mohamed Ali Shein kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi na kwa imani yake na Wazanzibari. Nasema nampongeza Mheshimiwa Rais wa Zanzibar kwa sababu ameonesha hakika yeye ni kiongozi na kiongozi wa kupigiwa mfano. Uvumilivu wake, utu wake, ubinadamu wake umefanya leo Zanzibar iwe ni nchi ya amani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Rais huyu hakuwa kiongozi ambaye ni mchu wa madaraka, hakuwa kiongozi ambaye anashibisha tumbo lake, amekuwa kiongozi mwenye kuitakia wema Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Ukimya wake kwa muda wote na maneno yote kwa muda wote aliokaa kimya lengo lake lilikuwa ni moja kuhakikisha Zanzibar iko salama, kuhakikisha Tanzania iko salama. Kama Rais alikuwa na mamlaka tosha na alikuwa na kila cha kufanya na alikuwa na aina ya sababu ya yeye pia kujitangaza lakini hakufanya hivyo, alitaka kwenda kwa utaratibu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii pia kumpongeza Waziri Mkuu kwa kuteuliwa kwake na kuthibitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Niwashukuru Mawaziri wote, imani yangu kwenu ni kwamba tutapiga hatua, hapa tulipo tutaendelea kusonga mbele. Tunaitegemea Tanzania mpya katika miaka mitano hii ijayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, shukrani zangu pia ziende kwa wapiga kura wangu ambao ni Wanawake wa UWT, Mkoa wa Magharibi. Nawashukuru kwa kunirudisha Bungeni na kuniamini kama mtoto wao naweza nikafanya kazi, nawaahidi sitowaangusha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Spika, nikupongeze wewe kama mwanamke, ujasiri wako tumeuona na tumeona ukifanya kazi kama mwanamke ambaye hutuangushi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nijielekeze moja kwa moja kwenye kuchangia. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri, kwa bajeti yake nzuri aliyoileta na nipongeze kikosi kizima cha Jeshi la Wananchi wa Watanzania. Kazi zenu ni nzuri zinaonekana ndiyo maana ukaona watu wanapiga kelele, mngekuwa hamfanyi kazi watu wangenyamaza kimya lakini kwa kuwa mnafanya kazi ndiyo maana watu wakapata fursa ya kunyanyua midomo yao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Waziri na wananchi wake kwa ujumla, niwapongeze kwa kumrudisha kila siku Bungeni kwa mbwembwe. Hii yote inaonesha ujasiri wake na uwezo wake wa kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sura ya tisa katika kitabu cha Mheshimiwa Waziri imezungumzia suala zima la maendeleo ya viwanda, kilimo na ajira kwa ujumla. Vijana tumaini kubwa liko kwake. Akitaka kujua kama Tanzania vijana matumaini yako kwake aone wakati unapofika wa kuchukua watakaojiunga na JKT au jeshi kwa ujumla. Vijana wengi huhangaika na nafasi hizi kwa sababu matumaini yao kama vijana wa Tanzania yako kwake. Nadhani ni vema wakashirikiana na Wizara ya Viwanda na Kilimo wakaona ni jinsi gani wanaweza kuwasaidia vijana wa Tanzania. Naamini kwa kufanya hivyo tutaendelea zaidi kama vijana wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nijielekeze kwenye suala zima la uchaguzi. Toka tulipoanza Bunge hili hoja kubwa na michango ya Wizara zote zilizochangiwa ni hoja ya uchaguzi wa Zanzibar. Uchaguzi wa Zanzibar umekwisha, Rais yupo, anatawala, tunaendelea kama kawaida. Sasa hizi kelele unaenda kumpigia Jeshi la Wananchi wa Tanzania amekufanya nini? Kwa sababu wanaposema wanadhani hawana uwezo wa kuingia humu ndani ili kujibu. Jeshi la Wananchi wa Tanzania limeitendea haki Zanzibar. Kati ya vyombo ambavyo tunastahili kuvipongeza Tanzania ni pamoja na Jeshi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sikuwa na shida ya kuzungumza hapa, nazungumza kwa sababu jeshi hili halikumpiga mtu, halikumchapa mtu, halikumtukana mtu, halikufanya kitendo chochote cha kuweza kuzungumzwa kwenye Bunge hili. Jeshi lile limekaa Zanzibar kwa amani, limepita kwa mbwembwe, hivi jeshi linapita wewe unaogopa nini? Una masuala gani ya kukufanya uliogope Jeshi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Hebu tuambie hoja yako ya msingi juu ya Jeshi hili ni nini ili tuwapeni majibu ya uhakika. Toka Bunge lianze tumekosa jibu la kuwapa kwa sababu hatukuona suala la msingi juu ya masuala yenu mnayozungumza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jeshi limekaa Zanzibar…
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ukurasa wa nane wa kitabu cha hotuba ya Waziri wa Jeshi la Ulinzi kimezungumzia suala zima la kuimarisha muungano, mlidhani muungano unaimarishwaje? Mlidhani ile kuoa na kuoana tu kunatosha kuimarisha muungano? Muungano utaimarishwa na Jeshi la Ulinzi. Mimi niwapongeze, kati ya mtu ambaye anajisikia ufahari mkubwa leo kusimama hapa kuziona zile kofia zipo pale mmoja wao ni mimi. Tunawapenda, fanyeni kazi na kila uchaguzi ukifika msimsubiri Waziri awapeni amri. Jenerali upo, viongozi wote wapo tunataka mshuke iwe kwa boti, iwe kwa ndege na kadhalika lakini muingie Zanzibar kufanya kazi. Hata uchaguzi ukirudiwa warudi, wakitaka kuja kesho waje, kitakachotokea tunakuombeni mje msisubiri amri, fanyeni kama wajibu wenu, fanyeni kama kazi zenu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wamezungumzia mambo mengi kuhusu uchaguzi lakini tu tungependa kuwaambia kwamba uchaguzi pamoja na kwisha, kulikuwa na hoja zinazongumzwa na Tume, Mwenyekiti wa Tume alikaa kwenye TV zikachambuliwa kasoro, kila kitu kilichoonyeshwa kule, hamkuwa na hoja na ninyi kutafuta Kipindi mkajibu, mbona mlinyamaza kimya? Kama masuala mnayozungumzia kwamba document mnazo, mna ushahidi hata sisi document tunazo mpaka leo, kura mbili mbili zipo, saini wanaweka watu wawili wawili zipo, hakuna kilichokuwa hakipo! Mmebaki mnawinda lakini hayo mawindo yenyewe mnayowinda hakikisheni kwamba hayapo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa siku ya leo yangu yalikuwa hayo machache, nakushukuru kwa kunipa fursa hii.