Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, naungana na Watanzania wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa jinsi alivyoijalia nchi yetu baraka zake katika ustawi wa jamii, amani, demokrasia, uchumi, diplomasia ya mashirikiano na mataifa mengine.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuipongeza Serikali yetu ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ilivyotatua changamoto zinazowakabili wananchi katika sekta za elimu, afya, maji, barabara na vitendea mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, aidha binafsi ninakupongeza sana kwa kuchaguliwa kwako kuwa Spika wa Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwenyezi Mungu akujalie mafanikio mema.

Sasa naomba nitoe mchango wangu katika hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu; kwanza Serikali itazame kwa upana suala la kukabiliana na majanga kutokana na matukio mbalimbali kwa kuja na mkakati wa kukabiliana na matukio yanayojitokeza kama vile corona, moto, ukame, mafuriko, viwavi jeshi na milipuko ya magonjwa, kwa kuandaa rasilimali wataalam fedha na vitendea kazi.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali ifanye tathimini ya kina kuhusu mafanikio ya viwanda 100 kwa kila Halmashauri ili kuleta tija zaidi kwenye ajira kama ilivyo kusudia awali; tatu, Serikali ifanye mapitio ya kina ahadi za viongozi wakuu wa Serikali walizotoa wakati wa uchaguzi na ziara wanazofanya mfano ni miaka saba sasa ahadi ya Mheshimiwa Hayati Dkt. John P. Magufuli ya lami kilometa tano, Mbulu Mji ni kilometa 2.5 mpaka sasa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.