Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa nafasi hii ya kuchangia hoja hii ya Mpango. Niwaambie Waheshimiwa Wabunge kwamba Wizara ya Nishati maoni yao na mapendekezo tumeyachukua na tutayafanyia kazi kwa upana wake. Niongelee tu kwenye maeneo machache mengine ni ya kuweka taarifa sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza kwenye gesi asilia. Kama tulivyosema juzi Serikali imeipa mtaji TPDC wa dola bilioni 1.193. Kwa kubadilisha deni la bomba la gesi kuwa sasa pesa ambayo TPDC inaweza ikaitumia. Kwa hiyo hatuna wasiwasi na tunakoelekea kwamba TPDC itaweza kukopesheka na kufanya biashara katika mazingira ambayo itakuwa na bargaining power za kuweza kupata mikopo yenye riba nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili tayari mikataba ya interest MOU zimesainiwa kati ya Tanzania na Uganda, Tanzania na Kenya, wenzetu wa Malawi na Rwanda wameonesha interest, kwa hiyo tukitoa gesi hii Dar es Salaam na Mtwara kupeleka Uganda hii Mikoa yote ya katikati itapata tukipeleka Kenya Mikoa ya katikati itapata kwa hiyo humu ndani tutaisambaza vya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo jingine ambalo nimeona nilisemee kidogo ni eneo la idadi ya vijiji vyenye umeme na visivyokuwa na umeme. Ukurasa wa 32 wa Mpango umeeleza taarifa na ni taarifa sahihi na naomba niseme kwa sasa. Vijiji tulivyonavyo kwa mujibu wa takwimu za TAMISEMI ni 12,345, kwa mujibu wa taarifa za TAMISEMI na kwenye mpango imeandikwa hivyo. Vijiji vyenye umeme mpaka kufikia Tarehe 31/10/2022 ni 9,163, Vijiji ambavyo bado ambavyo vyote viko kwenye REA III round II ni Vijiji 3,182 ambavyo mikataba yake inaendelea kwenye maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya takwimu ilitokea kwenye mazingira tuliyokuwa tunafanyia kazi. Huko nyuma kuna vitongoji vikubwa ambavyo vilipewa umeme na wenzetu wakavihesabu kama vijiji. Sasa vimeondolewa kwenye idadi ili tubakie na vijiji halisia na Waheshimiwa Wabunge tunafahamu kwenye maeneo yetu, maeneo ambayo tumeweka umeme kwenye vitongoji lakini vilihesabiwa kama vijiji. Sasa taarifa sahihi ni hii Vijiji 12,345, Vijiji 9163 tayari umeme na Vijiji 3182 umeme bado lakini vina mikataba vyote na vinafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Tatu ni kwenye uhakika wa umeme na wenye gharama nafuu. Mpango wetu umeelaza vizuri kabisa kwenye ukurasa wa 18, ukurasa 32 na kiambatisho C ukurasa wa 1- 3, umeeleza miradi mingi sana ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mchangiaji alisema hata mpango wa kutoa umeme Mwalimu Nyerere kuuleta Chalinze haupo. Ukurasa wa 33 umeeleza vizuri kabisa kwamba tunatoa umeme Mwalimu Nyerere na tutauleta Chalinze na kazi inaendelea tunatarajia ikamilike mwaka unaokuja na miradi ya kutoka Chalinze kuja Dodoma, kutoka Chalinze kwenda Mwalimu Nyerere yote imeelezwa kwenye mpango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye miradi ya uzalishaji kuna mwenzetu mmoja alichangia kwamba…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri hapo ndiyo ambapo kidogo huwa tunachanganyikiwa, mwaka ujao kwa maana ya 2023 au mwaka 2024 maana unasema mnatarajia ikamilike mwaka ujao, wakati taarifa tulizonazo ni 2024.

NAIBU WAZIRI WA NSHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa kutoa umeme Mwalimu Nyerere kuuleta Chalinze unakamilika mwaka wa fedha huu. Nina maana ya Januari kuelekea Juni, mwaka wa fedha huu. Kwa hiyo, kwa program tuliyokuwa nayo itakamilika kabla ya Bwawa la Mwalimu Nyerere kukamlika ambalo kwa mujibu wa mkataba wa extension nitakaousema baadae inatakuwa kuwa Oktoba mwakani. Kwa hiyo, ni mwaka wa fedha huu tuliopo sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi ambayo mpango umeitaja kwa ajili ya uzalishaji. Tunao Mwalimu Nyerere, megawatt 2115, tunayo Rusumo unakamilika muda siyo mrefu megawatt 80, tunayo Ruhuji inakuja megawatt 358, tunayo Rumakali megawatt 222, tunayo Kikonge megawatt 300 tuna miradi ya upepo na jua megawatt 300, tunayo Kinyerezi One Extension megawatt 185, zote hizo tunatarajia kwamba zitatupatia umeme kwa mujibu inavyotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba unipe nafasi kidogo ya kueleza mambo mawili kwenye mradi wa Mwalimu Nyerere.

MWENYEKITI: Sasa kila Waziri anaomba apewe nafasi kidogo tu sijui nimkate mmoja ili ndiyo niwe nimezigawanya hizo? Haya dakika moja malizia.

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa sababu ya muda nizungumzie vitu viwili tu. Kimoja muda tuliouongeza kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere ni mwaka kwa mujibu wa mkataba, tumeongeza mwaka mmoja na muda huo utakapoisha ndiyo tutaanza kugombana kuhusu nani kachelewesha mradi.

MWENYEKITI: Mwaka mmoja ndiyo mpaka lini?

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Oktoba mwakani kwa mujibu wa mkataba tuliosaini. Iko taarifa na mpango kazi wake aliouleta anapoomba miaka miwili sisi tulimwambia tunampa mwaka mmoja na wenzetu wataalam wanaendelea kuchanganua ule mpangokazi wa utekelezaji ili u-fit mwaka mmoja lakini mkataba wa nyongeza extension of time ni mwaka mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kidogo kuhusu hii habari inayosemwa ya liquidated damages, taarifa sahihi ni kwamba liquidated damage kwenye mkataba wa Mwalimu Nyerere ni 0.1% kwa kila siku kwa maximum ya asilimia Tano siyo asilimia Kumi siyo zaidi ya hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni kwenye CSR tunaambiwa tunatoa taarifa kwamba tungezikata hizi pesa. Mkataba unatueleza kwamba tumpe Mkandarasi atekeleze CSR, tulikuwa hatujakubaliana miradi ya kutekeleza sasa tumekubaliana Mkandarasi ataanza kutekeleza CSR za bilioni 263 na tuko ndani ya muda na tutakamilisha kazi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. (Makofi)