Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na mimi kwa kunipatia nafasi niweze kutoa maoni yangu katika mapendekezo ya mpango wetu wa mwaka mmoja. Moja kwa moja naunga mkono mapendekezo ya mpango pia naunga mkono maoni ya Kamati yangu ya Bajeti ambayo na mimi ni mmoja wa wanakamati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimshukuru Mheshimiwa Rais, niishukuru Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kutupatia tani 30 za mahindi Wilaya ya Meatu kwa ajili ya kukabiliana na uhaba wa chakula. Wilaya ya Meatu tuna upungufu wa tani 19,000 hii imesababishwa na ukame uliokuwepo wananchi hawakuweza kulima kwa kiasi kikubwa na waliolima mazao hayakuweza kuota na yaliyoota wengine hawakuweza hata kupalilia. Hivyo tuna upungufu mkubwa wa chakula na tunaomba Serikali iendelee kusaidia Wilaya ya Meatu pamoja na jirani zetu Mkoa wa Singida ambao wanatusaidia mahindi kwa kuleta mahindi yale yamekwisha katika Mkoa wao, Serikali iongeze speed ya kusaidia Wilaya ya Meatu. (Makofi)

Mhshimiwa Mwenyekiti, niendelee kumshukuru Mheshimiwa Rais wetu kwa mipango yake mizuri na kwa kazi yake nzuri hasa katika matumizi ya zile Trilioni 1.3. kazi kubwa imefanyika. Pamoja na kazi kubwa iliyofanywa ya ujenzi wa miundombinu ya madarasa pia kazi kubwa imefanywa katika Wizara ya Maliasili na Utalii. Miundombinu ya barabara imetengenezwa vizuri kwa ajili ya kuwawezesha watalii wetu ili ku-facilitate kazi za utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa, uwekezaji mkubwa umefanywa katika ununuzi wa mitambo ya kutengenezea barabara pamoja na ununuzi wa magari makubwa katika Wizara ya Maliasili Idara ya TANAPA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu na ushauri wangu, Wizara hii sitegemei uendeshaji wa mitambo hii utegemee asilimia 100 kutoka ruzuku ya Serikali. Mitambo hii iliyopelekwa ni mipya kwa sasa ina sifuri katika suala zima la uchakavu, niliomba mitambo hii ijiendeshe yenyewe kwa kufanya miradi mbalimbali si ya TANAPA peke yake lakini hata taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili ikiwemo TAWA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu niltaka sasa kuwena mpango Pamoja na mpiango mingine ya TANAPA na Maliasili kuwe na mitambo ya kuchimba malambo katika hifadhi zetu katika mapori ya akiba ili kuodoa suala la binadamu na wanyamapori kuchangia miundombinu iliyotengenezwa ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mathalani katika Wilaya ya Meatu bwawa letu la Meatu tembo wapatao 15 zaidi ya mwezi mmoja waliweka kambi katika bwawa letu ambalo ni kilomita tatu kuja Mjini Mwanuhuzi. Kwa hiyo, kuwapunguzia wananchi huduma kulikuwa kuna uhaba mkubwa wa maji katika Mji wa Mwanuhuzi kutokana na tembo hao ambao 15 waliweka kambi lakini zaidi ya 15 walikuwa wanakuja na kuondoka. Kwa hiyo Serikali ijikite kuchimba malambo katika hifadhi ili wale Wanyama waendelee kubakia kule kule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Wizara hiyo kupewa fedha ya uwekezaji huo nilitaka sasa fedha zile zitakazopangwa ziwekwe katika kuwekeza miradi mingine, katika Maliasili na Utalii kufikiria kuanzisha miradi itakayo ingiza mapato ujenzi wa mahoteli, tuna upungufu wa hoteli katika Mbuga zetu kutokana na uwingi wa watalii wanaokuja kutokana na Mama yetu kuutangaza utalii wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Halamga ya kufungua malango. Tuombe katika Wilaya ya Meatu tufunguliwe lango la kuingia katika Hifadhi ya Serengeti kwa sababu Wilaya ya Meatu Serengeti imo kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niunge mkono maoni ya Kamati katika kipengele cha kilimo cha umwagiliaji na ujenzi wa mabwawa. Wizara ya Kilimo ina hekta Milioni 29 ambayo inaweza ikafanywa umwagiliaji lakini ni asilimia Mbili tu ambayo iko chini ya umwagiliaji ambayo ni hekta Laki Nane. Tukiangalia katika hekta Laki Nane hizo naamini kabisa kuna miundombinu ambayo ilishakufa kuna miradi ambayo ilitekelezwa lakini haijakamilika. Kwa Mfano miradi iliyotekelezwa na DASP katika miaka ya 2014 miradi ile haikukamilika lakini ilitumia Mabilioni ya Shilingi kwa mfano kutokana na fedha za Benki ya Afrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe miradi hiyo ya DASP iliyoanzishwa ya umwagiliaji ili iweze kukamilishwa iingizwe katika ile idadi kukabiliana na uhaba wa maji katika nchi yetu. Mfano Wilaya ya Meatu mradi ulitekelezwa kiasi kwa Bilioni 1.2 ambo ungeweza kuhudumia hekta 150 sawa na kaya 129 ambapo tungepunguza kabisa uhaba wa chakula, kwa sababu tulitegemea kulimwa mazao ya bustani, mahindi, mpunga na mambo mengine lakini pia wananchi wangeweza kujipatia kipato kwa kuuza ziada. Kwa hiyo, niombe miradi ya DASP ikamilishwe ambayo haijakamilishwa. (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, pamoja na hayo nilitaka kuomba Wizara ya Maji na Wizara ya Kilimo ziweze kushirikiana kwa sababu kitengo cha umwagiliaji kiko katika Wizara ya Kilimo. Wizara ya kilimo haiwezi kufanya peke yake ikaweza kutekeleza miradi ya umwagiliaji. Kwa mfano, Wizara ya Kilimo inaweza ikachangia fedha zake katika miradi ya kutoa maji katika maziwa makuu kwa mfano ule mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya athari ya Tabianchi unaotekelezwa katika Mkoa wa Simiyu kuna component ya umwagiliaji, katika fedha za ufadhili zinahitaji pia nchi yetu ichangie, basi zile fedha ambazo ziko katika Wizara ya Kilimo ziletwe katika mradi huo ili tuweze kutekeleza ule mradi mkubwa wa kukabiliana na athari ya mabadiliko ya Tabianchi hii katika Mkoa wa Simiyu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuisaidie Meatu, Meatu ina uhaba mkubwa sana wa mvua kwa ajili ya binadamu na hata kilimo. Mimi ninashukuru na ninaunga mkono hoja. (Makofi)