Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Leo ningependa kutoa mapendekezo yangu katika mpango huu wa Mwaka Mmoja wa 2023/2024 kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunafahamu kwamba Wizara na Serikali imetueleza hapa, kwamba imejipanga kuhakikisha kwamba inaboresha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara hata hivyo pia mazingira mazuri katika ufanyaji biashara na uwekezaji katika nchi yetu hii ya Tanzania.

Leo mchango wangu na ushauri wangu utajielekeza kuielekeza Serikali kuongeza bajeti na kutenga bajeti na fedha katika kuhakikisha kwamba ina invest kwenye Jeshi letu la Polisi hasa katika kuwekekeza zana za kisasa katika kuweza kupunguza matumizi ya Askari Polisi barabarani. Ni ukweli usiopingika kwamba tunapozungumzia ukuaji wa uchumi na tunapozungumzia mazingira mazuri ya uwekezaji inaonesha ya kwamba ni lazima tutengeneze mazingira yanayoenda na uhalisia wa kumwezesha mfanyabiashara kutekeleza majumu yake kwa wakati au biashara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii utaona Jeshi letu la Polisi katika nchi yetu hii ya Tanzania imekuwa ni obstacle, imekuwa ni kikwazo kikubwa katika kuhakikisha ya kwamba inamwezesha mfanyabiashara kutimiza majukumu yake na kumwezesha kutimiza majukumu yake kwa wakati. Leo hii utaona unapozungumzia habari nzima ya uwekezaji ni lazima uzungumzie habari ya miundoimbinu. Serikali yetu nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kuweka fedha kuimarisha miundombinu ya barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii utaona barabara ambayo Serikali ime- invest fedha nyingi ili kumwezesha mfanyabiashara huyu aweze kutimiza majukumu yake ya kwa wakati, Jeshi la Polisi na hususan Usalama wa Barabarani wanasimama barabarani kuhakikisha ya kwamba ukaguzi wa magari yale, pia mara zote kuhakikisha ya kwamba huyu mfanyabiashara anaweza kutoka hapa kwa namna moja ama nyingine wanaweza kumzuia mfanyabiashara huyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejenga barabara ya njia Nane kutoka Dar-es-Salaam kuja mpaka Chalinze lakini utaona kila baada ya mita tano Askari Polisi hasa traffic hawa wamejaa barabarani, lengo ni ukaguzi ambao ukaguzi huu unamchelewesha mfanyabiashara kwenda kutimiza majukumu yake kwa wakati. Sasa niiombe Serikali iweze kuona namna gani inaweza ku- invest fedha ili iweze ku-invest kwenye Jeshi la Polisi kuwa na mitambo ya kisasa kuhakikisha kwamba inafanya kaguzi mbalimbali kwenye maeneo ya barabarani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala zima la Madini. Niipongeze sana Wizara, mimpongeze Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba anaweka jicho lake kumsaidia mchimbaji mdogo mdogo katika maeneo yale. Pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya katika sekta ya madini. Ninaomba na ninashauri Mheshimiwa Waziri wa Fedha upo hapa, leo hii mchimbaji mdogomdogo hasa sekta ya madini na Mheshimiwa Rais alitoa maealekezo kwamba anahitaji Wizara ya Madini, iweze kuchangia Pato la Taifa sasa ili Wizara ya Madini, iweze kuchangia Pato la Taifa lazima Serikali iweke mkakati na bajeti kubwa kuhakikisha ya kwamba inamwezesha huyu mchimbaji mdogomdogo. Kwa hiyo, naomba nishauri Wizara na Serikali iweze kutenga fedha ili iweze kuwakopesha hawa wachimbaji wadogowadogo katika kwenda kufanya uwekezaji kwenye maeneo yao ili waweze kuzalisha kwa wingi na kuweza kuchangia Pato hili la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nizungumzie suala zima la barabara. Leo miundombinu ya barabara yetu katika maeneo yetu haya niipongeze Serikali na nimpongeze Mheshimiwa Rais kwenye Jimbo langu la Msalala, ametoa maelekezo kwa ajili ya ujenzi wa barabara yenye kiwango cha lami kutoka Bulyanhulu kwenda mpaka Kahama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na urasimu katika utekelezaji wa miundombinu hii kwa wakati. Sasa niiombe Wizara kwamba ihakikishe pale ambapo tunatenga fedha na bajeti kwenda kujenga barabara wapitie upya mambo ambayo yanakwamisha utekelezaji wa miundombinu hii ya barabara ili kuwezesha barabara hizi ziweze kutekeleza kwa wakati na kumwezesha mfanyabiashara kutumia barabara hizi katika kutekeleza majukumu yake kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara yangu ambayo tayari Mgodi wa Bulyanhulu umetenga fedha kiasi cha Dola Million 40 kwa ajili ya utekelezaji wa barabara. Barabara hii kwa muda mrefu sana tumeweza kuipambania Mheshimiwa Waziri wa Fedha ni shahidi, mpaka dakika ya mwisho Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan, ametoa tamko kwamba barabara ile sasa fedha ipo tayari na barabara ile ianze kujengwa maana ya kutoka Bulyanhulu mpaka Kahama, lakini leo hii utaona Wizara ya Miundombinu na Ujenzi kutoa tu kibali cha kuweza kuitangaza barabara hii ianze kujengwa mpaka leo bado hakijatoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niombe ili mpango huu ambao tunaujadili hapa uweze kutekelezeka kwa wakati ni lazima tupunguze urasimu ndani ya Serikali. Tunapanga mpango huu sisi wenyewe lakini sisi wenyewe hawa hawa tunaukwamisha huu mpango. Kwa hiyo, niombe sana Mheshimiwa Katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi, aweze kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais ya kuanza kutangaza barabara hii na ianze kujengwa kwa wakati, barabara yenye kilometa 77 ambapo fedha zake anayelipa ni mgodi na mgodi upo tayari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha sana leo hii tunaona fedha zile tumepewa na Mhisani hivi ikitokea leo madini yamepotea fedha zile tutazitoa wapi? Mlipaji yupo tayari na anataka kujenga barabara ile kwa wakati lakini Katibu Mkuu kutoa tu kibali barabara ile ianze kujengwa hajatoa mpaka leo ilkitokea leo madini yale yamepotea tunafanya nini? Ahsante sana. (Makofi)