Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuweka mchango wangu kwenye Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2023/2024.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajadili Mpango wa Mwaka Mmoja katika Mpango wa Miaka Mitano wa 2021/2022 hadi 2025/2026 ambao vipaumbele vyake ni pamoja na kuchochea uchumi shirikishi na shindani, vilevile kuimarisha uwezo wa uzalishaji. Ili mpango huu uweze kutekelezeka ni lazima Serikali iwekeze kwenye sekta ambazo kwanza zitaongeza uzalishaji na kwa maana hiyo katika kuongeza uzalishaji tutaongeza mauzo yetu nje jambo ambalo litasaidia kuongeza Pato la Taifa. Vilevile Serikali iwekeze kwenye sekta ambazo zitatengeneza ajira kwa wingi, jambo ambalo litasaidia kutengeneza nguvu ya manunuzi kwa mtu mmoja mmoja na kwa maana hiyo kuongeza mzunguko wa kifedha na kwa level ya chini kuongeza hali ya kipato kwa Halmashauri zetu na kuimarisha mfumo wa utendaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze kuhimarisha sekta hizi nilitaka nichangie kwenye maeneo kama matatu hivi: Kwanza ni eneo la uvuvi. Ninatambua mpaka mwaka jana sekta ya uvuvi imekua kwa karibu asilimia Sita na kuchangia kwenye Pato la Taifa kwa asilimia kama 1.71. Tunaweza kuzalisha zaidi kama tutawekeza kwenye sekta hii ya uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana kwa mfano mavuno ya samaki, tumevuna tani karibu laki nne na elfu kumi na tano. Niipongeze Wizara, pamoja na kuwekeza karibu Bilioni 20 kwenye mfumo wa ufugaji wa samaki kupitia njia ya vizimba, jambo ambalo litasaidia angalau vizimba 800 kuanzishwa lakini tunaweza tukazalisha zaidi kama tutawekeza zaidi kwenye ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo yangu pamoja na Serikali kupitia Wizara ya Uvuvi, kuwekeza Billion 20 kwenye ufugaji wa vizimba. Ninashauri kuwe na mnyororo wa ufuatiliaji kutoka Wizara na wale watakao pewa mikopo ili kuweza kuwasaidia kutoa ushauri wa kitaalam, vilevile kusaidia kutafuta masoko ya bidhaa ambazo watu hawa watakuwa wanazalisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ni la utalii. Pamoja na kwamba kwenye mwaka uliyopita sekta hii ya utalii imechangia karibu asilimia 17 ya Pato la Taifa na zaidi ya asilimia 25 ya fedha za kigeni lakini tunaweza tukafanya vizuri zaidi. Nimpongeze Mheshimiwa Rais, kupitia Royal Tour sekta ya utalii imefanya vizuri sana baada ya uzinduzi wa Royar Tour, lakini nishauri maeneo kama mawili:

Kwanza, bado tuna vivutio vingi sana vya utalii atujaweza kuvitambua na kuvitangaza. Eneo kama Ukerewe tunavyo vivutio vingi, tumekuwa tunasema hapa tuna jiwe linalocheza, tunazo fukwe nzuri sana lakini bado azijaweza kutambuliwa na kuweza kutangazwa pamoja na maeneo mengine, nishauri Wizara ya Utalii, iweze kutafuta bado, kubaini vivutio vingine vingi vya utalii vilivyopo iweze kuvitangaza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Pili, lingine ni eneo la kilimo. Ni muhumu sana, wachangiaji wengi wamesema juu ya sekta ya kilimo, nami bado nashauri tunahitaji kuwekeza nguvu kubwa kwenye sekta ya kilimo. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri, anafanya kazi kubwa sana kwenye sekta hii ya kilimo lakini bado tunahitaji tuwekeze kwa kiasi kikubwa sana, tuweze ku-utilize rasilimali tulizonazo ili ziweze kuwa na tija na kuongeza Pato la Taifa kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo kama Ukerewe wiki iliyopita tumeomba chakula Wizara ya Kilimo lakini kwetu Ukerewe tumezungukwa na maji, tunaweza tukafanya kilimo cha umwagiliaji tuna hekta zaidi ya elfu mbili ambazo ziko tayari kwa kilimo cha umwagiliaji. Tunachohitaji ni msaada tu wa Serikali kuwekeza ili tuweze kutumia maeneo yale kwa tija. Jambo hili pamoja na Ukerewe lakini hata maeneo mengine. Kwa hiyo, nishauri bado tunahitaji kuwekeza kwa kiasi kikubwa sana kwenye kilimo cha umwagiliaji kwenye Taifa hili kwasababu tunayo ardhi ya kutosha tunazo rasilimali maji za kutosha jambo ambalo linaweza likatufanya tukafanya kilimo cha umwagiliaji na kikawa ni kilimo cha tija. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na uwekezaji huu kwenye sekta za uzalishaji. Kwenye sekta zinazotengeneza ajira bado haitokuwa na tija sana kama wananchi wetu hawawezi ku-move kutoka upande mmoja kwenda eneo lingine kufanya shughuli zao za kiuchumi. Nimeona kwenye mpango juu ya uimarishaji wa barabara zetu mbalimbali. Niombe kwa utulivu kabisa Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, wanisikilize kwa makini kwenye ukurasa wa 24 wa mpango imetajwa barabara Na. 4141 imetajwa kwa jina la Nyamswa, Bunda, Kisolya ningeomba barabara hii ifanyiwe marekebisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii kwa asili tokea upembuzi, usanifu wa kina imetajwa kwa barabara kwa jina la Nansio, Kisolya, Bunda, Nyamswa. Kwa hiyo, ifanyiwe marekebisho na kwenye hoja yangu kwenye eneo hili, ili kuimarisha mawasiliano kwa sababu barabara hii ilitengenezwa kwa Lots tatu, lot ya kwanza na lot ya pili tayari inaendelea basi ikamilishwe lot ya tatu ya kutoka Kisolya kwenda Nansio ili kurahisisha mawasiliano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.