Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii na mimi kuweka baraka yangu katika mpango huu wa Mheshimiwa Waziri wa Fedha.

Kwanza kabisa na mimi kwa niaba ya wananchi wa Gando natoa zangu pole kwa wote wahanga waliofikwa na issue hii ya Precision Air, lakini kwa wale waliotangulia mbele ya haki tunasema Allahumma ghufilahum warhamni maskanahum fil Jannah (Mwenyezi Mungu aende awape pepo na mapumziko mema na sisi atujalie hatima njema).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi leo nitachangia mambo matatu katika mpango huu ambayo naona kidogo hayakuzunguziwa sana kwa mujibu wa nilivyosoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukuza uchumi wa nchi ni lazima tuweze kukuza teknolojia ndani ya nchi yetu. Nimeangalia miongoni mwa means ya kukusanya kodi ni pamoja na kuliongezea Jeshi la Polisi uwezo wa kiteknolojia. Leo Mheshimiwa Bonnah alisimama hapa kazungumzia suala la kamera za barabarani, jambo hili ni la msingi sana. Wengi ambao hawana taaluma na masuala ya kamera wanaona kwamba labda ni kumulika tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kamera hizi zitakapowekwa barabarani zinauwezo wa kuwa integrated na system za kileo ambazo zina uwezo wa kuweza ku-capture plate numbers na kuweza kupiga automatic fine na mwisho wa siku Taifa hili likakusanya fedha nyingi kuliko traffic kutembea na gadgets ambazo traffic unaweza uka- bargain naye barabarani, bwana nipige faini ama la na akakuacha, lakini teknolojia haina bargaining.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ningeshauri katika Mpango huu Mheshimiwa Waziri wa Fedha uchukue suala hili la CCTV camera tuweze kuweka walau kwa kuanzia first phase tuweke katika junctions za barabara zetu. Wapo wanaopita taa nyekundu, wanao overtake hovyo, wako wanaofanya mambo ya hovyo kabisa barabarani ili wakumbane na system hii mwisho wa siku tuweze kuweka nidhamu bora barabarani na kukusanya mapato kwa kutumia digitali hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda mbali zaidi teknolojia hii hii iende i-apply katika kulinda heshima, mali na utu wa Mtanzania na kwa wale wenzetu wanaotoka nje ya Tanzania wanaokuja hapa Tanzania. Nasema hivi kwa sababu lipo janga kubwa ndani ya Taifa letu sasa hivi na mimi naliona na tiba yake inaendeshwa lakini kidogo kidogo sana likisimamiwa na Jeshi la Polisi, suala la kuchafuliwa majina ya watu kupitia mtandao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwapatia uwezo askari polisi na tukawajengea unit maalum ya cybercrime iliyo ya kweli kabisa kwa kila kituo cha mkoa, tukawapa na equipment na skills ili waweze kuwakamata hawa watu ambao wanachafua watu ambao wamejenga heshima zao kwa miaka mingi, basi Taifa hili tutaweza kwenda mbali zaidi. Lakini sio tu kuchafuliwa majina, lakini pia mtandao unatumika kwa ajili ya kufanya fraud ya kuwaibia watu fedha. Wapo watu wanatapeliwa wengi, kuna zile namba utasikia tuma kwa namba hii. Kuna watu wanasikiliza information za watu halafu mara tu wana-dump in na wanakuja kuchukua fedha pasipo na kuzifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba Wizara ya Fedha walichukue hili tuliwezeshe Jeshi letu la Polisi kwa skills pamoja na equipments, kwa kila mkoa iwepo kweli cybercrime na sio tu maneno. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi katika kituo cha mkoa wetu Wete pale simuoni askari hata mmoja ambaye ana iPad ya inayoshughulika na masuala ya kwenda ku-extract information kwa ajili ya kuweza kutupa majibu haya. Jambo hili linapelekea polisi kuweza kupewa lawama kubwa. Kesi ni nyingi lakini watuhumiwa hawakamatwi mpaka polisi waende wakaangukie taasisi nyingine, wakapigie watu magoti sjui TCRA, mobile providers hao. Polisi wenyewe waweze kutengenezewa unit na waweze ku-extract information kiukweli hasa ili tuweze kuendelea zaidi ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho kabisa ningependa pia Mheshimiwa Waziri wa Fedha aliangalie suala la kuongezea nguvu Jeshi letu la Uokozi (Fire). Kwa mfano wa Jiji la Dar es salaam, juzi hata mimi nilipata kadhia ya kuunguliwa gari langu moto, lakini gari la zimamoto mpaka lisukumwe au liwe boosted. Sasa hadi liwe boosted tayari watu watakuwa wamefariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliunguliwa na soko letu la Kariakoo, hivi ukiangalia distance ya kutoka kwenye Ofisi ya Fire pale hadi Kariakoo, soko lile ni la kufikia mpaka likaangamia namna ile? Ipo haja ya Serikali kuongeza magari ya kisasa, yaliyopo ni chakavu, yana umri sawa na Salim miaka 34 na kwenda mbele. Ukiangalia matukio yanatokea frequently, lakini kubadilisha equipment hizi imekuwa ngumu ndani ya Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba na mimi nitoe mchango wangu huo In Sha Allah uende ukatekelezeke. Ahsante sana. (Makofi)