Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipatia nafasi hii. Vilevile namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii ya kuchangia katika Mapendekezo ya Mpango wa Taifa wa Mwaka 2023/2024. Nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha, kutuletea Mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekit, kwa kuanza kabisa, kwa sababu Dira ya Taifa ya 2025 inaenda kwisha nilitegemea nione kuna mahali panaonesha kwamba sasa tunaanza Dira ya Taifa nyingine mpya ambayo wengine wanaiita ya muda mrefu, wengine sijui wanaita nini; kama ni ya miaka 50 ndiyo tutafanya break down ya namna gani tutafanya kazi. Hii ishirikishe wananchi na wadau mbalimbali ili kusudi tuwe na dira ambayo itakuwa ni shirikishi. Kwa hiyo, naomba sana kwenye Mpango huu nione mahali ambapo kwenye bajeti zetu tunaingiza hiki kitu kwasababu tumebakiza nafikiri mipango miwili na hii itakuwa inakwisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda ukurasa wa nne wa Mpango wa Mapendekezo tuliyoletewa hapa, utagundua kuna takwimu za ukuaji wa uchumi katika Mataifa yetu haya kwa maana ya East Africa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ukienda ukurasa wa nne wa Mpango wa Mapendekezo tuliyoletewa hapa utagundua kuna Takwimu za Ukuaji wa Uchumi katika mataifa yetu haya kwa maana ya East Africa. Kumbukumbu zangu ambazo nimezitoa hapo zinanionesha Kenya mwaka 2019 uchumi wao ulikuwa unakua mpaka 4.9, mwaka 2020 ikaenda negative 0.3, mwaka 2021 wameenda 7.2, maana yake waemsukuma kwa nguvu 7.2 unaongeza na 0.3 wameenda 7.5. Nchi ya Rwanda walikuwa 9.5 ilivyofika 2020 wakaenda negative 3.4, lakini 2021 wakaenda 10.2. Ukienda Sudani walikuwa 0.9 wakaenda mpaka negative 6.6 kwa sababu ya corona, lakini wamekwishajivuta wamekwenda mpaka 5.3.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tulikuwa 7.0 hatukwenda kwenye negative tulikwenda mpaka 4.8 na tumejivuta tuko 4.9 maana yake tumeongeza 0.1. Uganda walikuwa na 7.2 wakaenda mpaka negative 1.4, sasa wamefikia 5.1 maana yake wamekwishakwenda kama 6.5. Burundi walikuwa 0.8 wakashuka mpaka 0.3 sasa hivi wemekwenda 2.4 maana yake wameenda 2.7. Sisi tunakua kwa 0.1 mpaka 0.4 maana yake kuna tatizo hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuunge mkono ndugu yangu jirani yangu hapa Mheshimiwa Mwijage anaposema tuwe na Tume ya Mipango. Jana Mheshimiwa Ndugulile alisema Tume ya Mipango, maana yake hatujagusa mahali ambapo uchumi wetu unaweza kuchangamka, tunagusa, lakini tunagusa kwa kukua kwa 0.1, maana yake data haziwezi kudanganya ukuaji wetu ni mdogo kulinganisha nan chi zote za East Africa. Maana yake tunachokifanya sisi hatujagusa mahali pake. Ni wapi hatujagusa, ni kwa sababu hatujaingiza pesa ya kutosha kwenye productive sectors. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuwa na majibu rahisi kwenye maswali magumu. Tunatakiwa kwenda na wenzetu kwa sababu tunaenda kwenye mikutano, tunazungumza nini wakati wao wamekuza kwa 7.5 sisi tumekua kwa 0.5 au 0.4? Maana yake sisi tunavutwa badala ya kuendelea kutembea na wenzetu, sisi tunavutwa nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika robo ya kwanza ukuaji wetu wa pato la Taifa unaonekana umekwenda kwenye 5.2, maana yake tuna-predict kwenda kwenye 5.3 ndio maoteo yanavyoonesha. Kwa hiyo, hata malengo yetu ya ukuaji ni madogo, yaani ukijiwekea malengo madogo unategemea process yako nayo itakwenda kwenye malengo madogo. Kwa mfano, tunategemea kuona Ziwa Viktoria linashughulikiwa kufanya umwagiliaji wa kilimo chetu. Sijaona mahali popote tumeanza kumwagilia kwa Ziwa Viktoria. Tunasema tu mvua hainyeshi, kule maji yapo, kwa nini tusianzishe skimu ambazo zinatoa maji Ziwa Viktoria, zinatoa Nyasa, zinatoa Lake Tanganyika badala ya kuanza kushughulika na maji ambayo ni non predictable? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu wazi Mpango huu naomba uangaliwe vizuri tunapoenda kwenye utekelezaji wake, lakini Mpango huu umekuwa mara nyingi Mipango yetu ya Miaka Mitano, hoja yetu kubwa ilikuwa ni kuchochea uchumi shirikishi na shindani. Tuna miradi mingi sana tumeisema, iko mingi sana ambayo imefanyika ya barabara na niseme tu wazi kama kuna mahali ambapo pamoja na mambo tuliyoyafanya mwaka jana na bajeti yetu bado ile ahadi ya kuongeza mtandao wa umeme kwenye vijiji vyetu ya kilometa mbili haijafanyika. Kwa hiyo, uwezo wa wananchi wetu ku- access umeme bado ni kilometa moja ile ya kwanza, tuwaongezee hizo kilometa mbili ili uchumi huu uweze kuchangamka, bila hivyo hauwezi kuchangamka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile vijiji ambavyo tuliona bado havina umeme vipate umeme. Yako mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye ripoti yako kwenye page number 21 na TEHAMA. Watu wamekuwa wanazungumza hapa, inaonekana kilimo wanasema neno lao, tunataka Wizara hizi zisomane, zi-communicate. Kwa mfano, unachimba bwawa la maji, bwawa la maji tunategemea mtu wa kilimo atafanyia irrigation, wananchi watakunywa maji, lakini mifugo watawekewa sehemu zao za kunywea maji. Utakuta Wizara ya Mifugo inashughulikia bwawa lake, Wizara ya Kilimo bwawa lake, there is no communication, hawa watu wa-communicate ili matumizi ya Serikali yaende chini. Nategemea haya mambo niyaone kwenye hiyo nani hii iliyoletwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na moja, kuimarisha uwezo wa uzalishaji viwandani na utoaji wa huduma, hapa ndio kuna changamoto. Natoka kanda ya ziwa, naomba niseme ukweli, tulikuwa na ginnery 11 kule NCU, hakuna hata moja inayofanya kazi. Unategemea tunaposema tunataka tuuze processed goods kutoka kwa hawa watu ambao viwanda vyote 11viko chini watafanya nini? Kwa hiyo, kuna kitu cha kufanya hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri niseme tu kama story, nilipita juzi mahali fulani kwenye ginnery nikakuta usiku saa 4.00 wanafanya harusi, yaani sehemu ambayo walikuwa wanazalishia pamba, kuna harusi na watu wanastarehe, yaani inaonekana kabisa tumekwishatoka kwenye reli tuko mahali pengine. Turudi kwenye reli sasa kwamba, at least huko tunakotoka kwenye ginnery 11 angalau ginnery tatu zifanye kazi, tuwe na mambo ambayo sasa yanaonekana tunaweza kujenga uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kengele ya kwanza nimeisikia imelia, niseme wazi kwenye production sector. Wenzetu Waganda, nilikuwa namsikia ndugu yangu hapa, hata uki- surf kwenye internet utagundua kwamba, wao kwenye diary export yao wana dola kama milioni 220 ambayo ni milioni 500 wana-export kwa mwaka mmoja, sisi tuna-export zero na tunataka tuchangamshe uchumi. Wale ambao wanajua nilikuwa natembea juzi nafanya mazoezi, ofisi ya watu wa maziwa Tanzania iko pale kama unaenda stendi ya hapa Dodoma hapa, ukifika tu unajua hapa hamna kitu hapa, ukiiona tu ofisi unajua hamna kitu hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme wazi kuna kitu cha kufanya. Lazima tukubali tunakwenda ku-invest ili tupate kitu fulani kwa sababu, wenzetu kama wanauza bilioni 500, sisi tunauza sifuri halafu tunategemea huu uchumi wetu utakua haraka, haitawezekana. Kwa hiyo, niwaombe sana kwenye mipango hii sasa tujue kabisa tunekwenda kufanya nini kwenye productive sector na ionekane na haya tukayatekeleze, tutaona uchumi huu ukiwa umechangamka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema kuna kuimarisha mifumo ya upatikanaji kwenye kilimo na sasa wanasema kule kwamba, kuna guarantee scheme ya wakulima wadogo, mimi sina uhakika, labda ninakotoka Wabunge wenzangu wanaweza kusema; wanasema wameandaa guarantee scheme, yaani skimu inayoshughulika na wakopaji wadogo kwa ajili ya kilimo, sijaiona hii, lakini kwenye mpango huu naiona imeandikwa kwamba, inaonekana kuna mpango huo. Kwa hiyo, haya mambo mengi mazuri yaliyoandikwa yawe implemented…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)