Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi. Naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, pia na mapendekezo kwamba ataendelea kumalizia miradi ile ya kimkakati kama SGR, Bwawa la Mwalimu Nyerere na maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mipango ya maendeleo ya nchi yetu, ni vizuri tukatumia fursa pia ya kuwa na watu wengi. Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 inaonesha kwamba tuna Watanzania milioni 61.34 ambao wanawake ni milioni 31.24 sawa na asilimia 50.9 na wanaume tupo milioni 30.1 sawa na asilimia 49. 1; na nguvu kazi ya Taifa ni asilimia 55.9; na ndiyo maana tunazungumza hapa, kuna njaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kwamba ukifuatilia hata katika familia zetu, jamii zetu za kawaida, ni watu wachache sana wanafanya kazi. Kama kuna mtu ni mtumishi au mfanyabiashara, unakuta watu wengi wanamtegemea. Sasa hao watu ambao wameongeza ni vizuri ukawatumia kama fursa pia. Maana yake tuwekeze kwao kwa kuwawezesha kufanya kazi ambazo angalau hata pato la mtu mmoja mmoja ataweza kujitegemea na kuchangia kidogo katika pato la Taifa ili kupunguza mzigo kwa watu. Hatuwezi kuona watu wameongezeka, watu milioni 61 halafu tunapata njaa na watu wapo mtaani wanazurura tu. Watu wanakaa vijiweni tu, wanataka tu kupiga mzinga, nipe mia tano, nipe buku, na maisha yanaenda. Sasa nadhani ni muhimu tuangalie jambo hili na kujua kwa nini watu hawafanyi kazi? Nini kifanyike ili watu waweze kufanya kazi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna watu wa kutosha, wana nguvu, wala hata siyo wagonjwa; wagonjwa ni wachache, lakini kwanini kuna njaa? Nadhani jambo hili lichukuliwe hata nje ya mpango huu lijadiliwe. Ukitembea mtaani watu wapo saa mbili asubuhi wanazurura, hawafanya kazi, tunagombana bure tu. Hata ukienda ukaombwa hela usipotoa maana yake ni adui yako. Sasa hili siyo jambo ambalo kwa kweli tunaweza tukalifanya liendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata watu wa kutosha, wafanye kazi, wajilishe wenyewe, wachangie, na walipe kodi. Ndiyo maana watu hawalipi kodi, kwa sababu kama mtu hafanyi kazi, ukimdai kodi atalipa nini? Wanakamatwa vijana wenye nguvu, wenye utashi, eti ni wazururaji; kwanini? Hana kazi ya kufanya? Nadhani hili jambo lifanyiwe kazi vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, kuna Watu wa TASAF. Mpango wa Serikali ulikuwa ni kuwawezesha watu ambao ni kaya masikini, wanawezeshwa fedha kidogo kila mwezi, lakini wa-graduate kutoka hatua ya kuwa masikini zaidi. Kulikuwa na miradi midogo midogo; miradi ya kilimo cha umwagiliaji, ili mwisho wa siku hii tabia iishe. Siyo sawa, ukienda kwenye kata zetu, kwenye vijiji siku ambazo zimepangwa akina mama, vijana, wazee vikongwe wanakaa wanasubiri fedha, shilingi 30,000 mpaka shilingi 35,000 kwa mwezi mzima. Ukikaa pale ukaangalia, yaani Tanzania hili jambo lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wale watu ambao wana uwezo wawezeshwe watoke kwenye hiyo hali, tusaidie watu ambao kweli wana uwezo mdogo na tuweze kuwa- monitor. Kuna mchezo ambao wale ambao hawana uwezo hawapewi fedha, wale wenye uwezo wanapewa pesa. Majina yamegeuzwa chini juu. Hili nalo lifanyiwe kazi vizuri sana. Huwezi kuwa na Taifa ambalo watu wao wanasubiri mwezi mzima waende kupiga foleni eti wapewe shilingi 30,000, inatosha kitu gani? Hivi kwa mfano kiroba shilingi ngapi unanunua? Zaidi ya shilingi 50,000! Haisadii! Ni hela kidogo sana, lakini udhalilishaji ule; kwa sababu mtu anakaa pale; kwa kweli hili tuliangalie, lifanyiwe kazi. Taifa ili liweze kuendelea ni lazima watu wafanye kazi na mtu wa kusaidiwa kweli atambulike na anayepaswa kupewa msaada, apewe msaada. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa.

T A A R I F A

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Mbunge mchangiaji. Nadhani jambo analolisema Serikali imekusudia kufanya hivyo hivyo. Naomba tu nimpe taarifa kwamba Mpango huu wa Kaya Masikini lengo lake ni hilo hilo, kwamba ni kuziwezesha zile kaya masikini, lakini baada ya muda zina- graduate; na zikisha-graduate zinatoa fursa kwa wengine ili waingie na mwisho wa siku wengi watakuwa wameboresha hali zao za maisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Ushahidi, nataka tu nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kufanya utafiti na kufanya tathmini ya Mpango wa TASAF mpaka sasa tayari tunazo kaya zaidi ya 1,000 zinazoanza kuandaliwa ku-graduate kutoka katika Mpango wa TASAF kwenda kujitegemea hili kaya nyingine zisizokuwa na uwezo ziingie na mwisho wa siku ziweze kujitegemea. Hizi kaya zinazopewa hizo shilingi 30,000, shilingi 12,000, shilingi 22,000, upo uthibitisho wa wanakaya wameweza kuanzisha miradi ya kimaendeleo na ya kiuchumi ambayo imeweza pia kusaidia kwenye jamii.

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Waitara, muda wako umelindwa.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mheshimiwa Waziri nimekusikia, naomba uchukue mawazo yangu yafanyiwe kazi. Bado kazi iliyofanyika ni ndogo sana sehemu kubwa watu wetu kuna hiyo hali ambayo nimeizungumza. Sitaki kubishana na Serikali, nakubaliana kwamba tuendelee kufanya kazi na ni- recognize kwamba kuna maeneo wame-graduate na kuna watoto wamesaidiwa na wamesoma. Nikasema ukienda kuangalia namna ambavyo wamekaa pale, wanasubiri hicho kiasi kwa kweli, bado inabidi tufanye kazi zaidi na Serikali itoe ushirikiano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kwenye mpango zimetajwa baraba za vijijini na mijini kwa maana ya TANROADS na TARURA. Nilikuwa nataka nishauri kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha, ukienda kwenye Majimbo yetu Vijijini, Barabara za Vijijini nyingi hazihitaji hata kuwekwa lami. Unakuta Mbunge anakosa hata grader aweke mafuta hata Mfuko wa Jimbo au dau aweze kulima barabara, lakini barabara moja kila mwaka inatengewa fedha nyingi sana shilingi milioni 500, shilingi milioni 300 au shilingi milioni 700 wanalima, kila mwaka au kila baada ya miezi sita, na malalamiko ni mengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini msitenge fedha hiyo mnunue magreda na ma-compacter mgawe kwa kila Jimbo ili wale ma-engineer wa TARURA walime barabara kwa bei nafuu, unaweza ukapata mdau ukajaza mafuta kwenye grader badala ya kukodi. Hapa tunapiga mark time, nunua magreda mpe kila Mbunge kwenye Jimbo aajiri ma-engineer walime barabara kwa gharama ndogo. Halafu kama ni mpango mkubwa wa kuweka lami au changalawe, tangaza mkandarasi afanye kazi hiyo. Utaokoa fedha nyingi sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na pia huduma itapatikana katika Majimbo yetu na malalamiko mengi ya Wabunge yatapungua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, katika hotuba ya Mheshimiwa ya Mheshimiwa Waziri, ukurasa wa 27 amezungumzia uchumi shindani na shirikishi. Mheshimiwa Waziri, kwa mfano ukienda kule Sirari, tuna eneo tumetenga muda mrefu kwa ajili ya Soko la Kimataifa la Mabwe. Huduma zote kutoka Kanda wa Ziwa zinatoka katika mpaka wa Sirari. Ukijenga pale soko, bidhaa zote kutoka Kenya utapata mapato na fedha hiyo itaraudi haraka sana na uchumi utapanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nilikuomba ukienda kule Nyamuhonda, mpaka Sirari, na Itiru kumtoa mwananchi wa kawaida ambaye anataka mifuko miwili ya cement au mabati aende kulipa ushuru Sirari ni mbali sana. Tuwee fedha ndogo ili watu waweze kulipa kodi, tuweze kupata fedha katika maeneo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka nizungumze katika huu uchumi shirikishi, nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, Watanzania na Serikali, ni kwamba Wizara ya Maliasili ina lugha yake, Wizara ya Maji ina lugha yake, Wizara ya Kilimo wana lugha yao, Wizara ya Ardhi wana lugha yao. Tunazungumza uchumi shirikishi; mimi nina mfano, halafu tunajadili hapa mambo ya Watanzania watu wanaongea Kichina, Kihindi, kama Wamarekani au Wacanada, kama wamezuka leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie, mfugaji ukienda ukachukue ng’ombe zake 30 ambapo ng’ombe mmoja ni Shilingi milioni tatu, unazungumza karibu Shilingi milioni 90 umemnyang’anya, halafu umeenda umetaifisha, na eneo hilo huyu mtu hana sehemu ya kunywesha maji ng’ombe zake, hana sehemu ya malisho, hana sehemu ya soko, mifugo hiyo ndiyo benki yake. Huu uchumi unaozungumzwa shirikishi siyo sawa. Hapa kila Mbunge ana malalamiko. Nimefuatilia sana ziara za Waheshimiwa Viongozi wetu, wanatoa maamuzi kana kwamba wao sio Watanzania. Hivi unafuta Kijiji, halafu wale wananchi wanaenda wapi? Huyu Mbunge aliyempigiwa kura wanakwambia tulikuchagua wewe halafu tumefutwa, turudishie kura zetu; unafanyaje? Hili jambo naomba Serikali ilichukue very serious.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapozungumza mwezi wa Tisa uliopita, kule katika Jimbo langu wamekusanya ng’ombe kutoka Nyanungu, Nyarokoba, Kuyancha wameenda wametaifisha ng’ombe, wanasema hazina mwenyewe, watu wangu wanalia; halafu tena tarehe 15 mwezi wa Kumi wamekusanya nyingine, na ninapozungumza ziko hifadhini. Jua limekausha maji, only source ya maji ni Mto Mara, hakuna sehemu ya kunywesha wale ng’ombe, wamewekwa pale ndani; kuna maji ya chumvi, hawasikilizwi, hawaendi. Sasa huyu mwananchi wa kawaida ambaye mtoto wake yupo sekondari, yupo chuo, angeuza mfugo amsaidie, sasa hawezi; chakula hana, angeuza ng’ombe apate chakula; anaishije ndugu zangu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Viongozi na Mawaziri mtusikilize. Mnaenda kwenye Majimbo, sikilizeni watu. Hawa sio Wanyama, tuzungumze na Watanzania wenzetu, haitafurahisha; kuna watu hapa wanaitwa chawa, ukichangia jambo hapa badala yakujadili hoja, wanakujadili wewe. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Waitara.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaombe, mlinde uchumi wa Watanzania, halafu…