Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi ya kuchangia katika hotuba hii ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru sana Mwenyezi Mungu kunipa kibali pia cha kusimama, nampongeza sana Mama Samia Suluhu Hassan na Serikali yake yote kwa jinsi ambavyo wanaendelea kufanya kazi kwa umakini mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, magonjwa yasiyoambukiza ni magonjwa mengi na mengi yao yanazuilika, machache ni ya kurithi lakini ndiyo maana tumeendelea kuishauri Serikali katika Sheria zisizopungua 62 ambazo zimepitishwa na Bunge hili, nyingi sana kwa njia moja au nyingine zinahusika katika masuala mazima ya kuzuia magonjwa haya yasiyoambukiza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivyo, tunaomba Serikali izipitie na kuziboresha sheria hizi ili ziendane na mapambano dhidi ya kuzuia magonjwa ya kuambukiza ambayo hakika mengi yanazuilika. Sheria hizi ni kama moja apo Sheria ya Tumbaku, Sheria ya Bima ya Vyombo vya Moto vya Barabarani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ajali za barabarani zinatokana na vyombo vya moto ni mojawapo ya magonjwa yasiyoambukiza, tatizo hili limekuwa tatizo kubwa sana. Nimeona nizungumzie hili kwa sababu lina kuja kwa kasi kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashauri kwamba Serikali ije na mpango wa uhakika sana wa kuhakikisha inapunguza madhara inayotokana na vyombo vya ajali barabarani. Kama inawezekana Serikali iunde Mfuko wa Ajali za Barabarani tunaita (Road Accident Fund) huu mfuko utasaidia kwanza kupunguza gharama kuwagharamia wale watu wanaopata madhara ya hizi ajali za barabarani ambao ni mojawapo wa ugonjwa usioambukiza, lakini pia mfuko huu utasaidia vituo vyetu vya afya viwahudumie hawa waathirika au waliopata madhara ya ajali kwa haraka kwa upesi bila kujali kabisa rasilimali fedha, yaani huu mfuko utasaida akipata ajali tu paa! akienda kituo cha afya atahudumiwa bila kungoja kwanza malipo ya rasilimali fedha. Kwa hiyo, mfuko huu utasaidia sana kuokoa maisha ya ndugu zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ninashauri uboreshwe kwamba wahanga wanaotokana na ajali hizi wawe wanalipwa kutokana na bima ya chombo kile kilichosababisha ajali. Kwa sababu sasa hivi ni mpaka dereva ashitakiwe ahukumiwe aonekane anahatia ndiyo yule muhanga wa ajali alipwe fidia au wale wafiwa walipwe fidia.

Mimi nashauri iboreshwe hii bima kuna Sheria ya Bima ya Vyombo vya Moto iboreshwe kwamba, wahanga walipwe siyo kwa kuzingatia mashtaka au ya dereva kuhukumiwa hapana! As long as chombo kimethibitika ndiyo kilisababisha ile ajali au kile kifo basi sheria iboreshwe kwamba wawe wanalipwa kutokana na ile bima ya kile chombo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hii sheria iboreshwe kwa sababu ni sheria mojawapo ambayo inahusika na magonjwa yasiyoambukiza ambayo ni ajali imezidi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni masuala ya magonjwa yanayohusika na masuala ya UKIMWI. Ni suala lisilopingika kwamba asilimia 90 ya mapambano au madawa Afua zote za kupambana na UKIMWI tunategemea wafadhili, ni suala lisilopingika kwamba viwanda katika nchi au maboresho ya viwanda katika nchi ni mojawapo ya mustakabali wa kuboresha maisha ya Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nasema hivyo? Kulikuwa na kiwanda Arusha cha kutengeneza dawa za kuzuia makali ya virus vya UKIMWI mwilini, kiwanda hicho kilikuwa kimepewa ufadhili mkubwa wa European Union wakatengeneza mitambo ya kisasa kweli kweli, lakini kiwanda hiki kimekufa. Ninaishauri Serikali kupitia MSD wakifufue kile kiwanda, Msajili wa Hazina na asilimia 40 wale Wawekezaji walikuwa na asilimia 60 sasa MSD kwa maana ya Serikali ilinunua asilimia 60 ya kiwanda kile. Kwa nini nasema hivyo? Dawa, matibabu kwa mwananchi ni suala la usalama. Hatuwezi kutegemea kila siku matibabu ya mwananchi wako yatoke nje ya nchi. Huwezi kujua mtu anawaza nini, kuna vita kuna kila kitu!

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi leo kuna vita mtu atakazana kutengeneza dawa akuletee wewe, aache kupambana na vita yake? Kwa nini tusiwekeze kwenye viwanda vyetu hapa nchini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini tusiwekeze kwenye viwanda vyetu hapa nchini? MSD kwa miaka miwili sasa hivi kwenye ile Keko Pharmaceutical Industries walianza kutengeneza dawa moja tu ya paracetamol, na sasa hivi wana products kumi, vilevile wale wale wametengeneza barakoa. Mwananchi wa kawaida alikuwa hawezi kununua barakoa, lakini sasa hivi tumetengeneza barakoa pale Dar es Salaam, tuna kiwanda. MSD pia imetengeneza kiwanda cha gloves kule Mufindi kwenye baridi, maana ndiyo mazingira yanayotakiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo bado tuna uwezo wa kufanya vitu vyetu. Suala la dawa ni usalama, usalama kabisa kwa wananchi ambao unawaongoza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la dawa za kulevya. Haya ni mapambano ambayo ni nyeti sana. Wenzetu wanatumia vyombo vya kisasa ambavyo ni sophisticated kama vile boti na mitambo mbalimblai. Sasa nishauri tena kwa mara ya tatu, hii mamlaka itengewe fungu la maendeleo ili waweze kununua vifaa vya kisasa, pamoja na kujenga vituo ambavyo waraibu wakishahitimu wanaenda kufundishwa stadi kazi ili wasirudi tena kwenye dawa za kulevya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii mamlaka sitoiongelea sana; kila siku naongea, kwamba waongezewe fungu la maendeleo, waongezewe fungu la pesa kwa kuwa kazi yao ni ngumu na ni ya kishawishi sana. Sijasema waongezewe mafao binafsi, waongezewe mazingira ya kufanya kazi, waongezewe wafanyakazi, kwa sababu wana upungufu wa wafanyakazi zaidi ya 189. Kazi yao ni ngumu. MACH clinic zao ziko chake. Kwa mfano Kanda ya Ziwa yote ina MACH clinic moja tu ambayo iko Mwanza. Ile dawa wanakunywa kila siku, hivyo haiwezekani utoke Ukerewe uje Mwanza leo asubuhi halafu kesho urudi tena. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo nashauri tena kwa mara ya tatu katika michango yangu. Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya itengewe fungu, iongezewe fedha kwa kuwa kazi yake ni nyeti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni kuhusu Workers Compensation Fund. Nimeiona imeelezwa vizuri; lakini nilikuwa nashauri, lengo lisiwe tu kutoa fidia au ufanisi uwe tu kwa sababu umetoa fidia, hapana. Lengo liwe ni kuwekeza maeneo ambayo yatasaidia kupunguza ajali maeneo ya kazi; siyo mafanikio ni kufidia, hapana. Lakini pia nilikuwa nashauri, ikiwezekana mitaala ya medical schools zote iwe inajumuisha masuala ya ulemavu utokanao na ajali na magonjwa mahala pa kazi. Mitaala ya medical schools ihusishe masuala yote ya tathmini ya ulemavu unaotokana na ajala na magonjwa mahala pa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mwisho kabisa ni suala la wenzetu OSHA. Nipongeze kwa kazi nzuri wanayoendelea kufanya ya kuhakikisha usalama wa nguvukazi mahala pa kazi. Hata hivyo, nilikuwa naishauri Serikali, kwamba, ije na sheria, kama ikiwezekana, ambayo itawezesha kuajiri either part-time or fulltime watu wote wanaohusika na masuala ya OSHA mahala pa kazi ili kuhakikisha usalama wa nguvukaziwatu mahala pa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo machache naunga mkono hoja, ahsante.(Makofi)