Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa hii. Ninayo mengi kidogo, lakini nitajaribu kuzungumza machache. Niseme na najiunga na wenzangu kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wetu kwa mafanikio mengi tunayoyaona na ambayo yameorodheshwa vizuri kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Pia nimpongeze Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi na Makamu wa Rais wetu Philip Mpango na wewe pia Mheshimiwa Spika nikupongeze jinsi unavyofanya kazi yako.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hivyo, naomba niseme, tumesikia mengi yametekelezwa kwenye uchumi wetu, miradi mikubwa sana, lakini naomba Serikali ielewe kwamba, wakati unapofanya makubwa usahau kwamba kuna vikero vidogo vidogo ambavyo ukiviondoa vitakupa amani na kutekeleza yale makubwa.

Mheshimiwa Spika, ukiingia kwenye mtihani usianze na maswali magumu, anza na yale madogo na yale rahisi ambayo utayamaliza mara moja, halafu uende kwenye makubwa. Hasa ukienda kwenye halmashauri zetu kwa mfano, kuna vijikero kama kwa mfano kule Vunjo, barabara ya kilometa saba toka Mji Mdogo wa Himo kwenda Lotima, kitu ambacho unaweza ukakimaliza kwa fedha utakayoita ni chenji tu.

Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye barabara tunayoita ni ya Mandaka - Mkirema kilometa saba ni pesa kidogo, ukienda Uchila – Kisomanji - Kikolarii ni kilometa saba au nane, kwa hiyo unaweza ukaviondoa na mimi nisije tena hapa nikiwa naomba kuuliza maswali hapa na pale, nitawaachia na wengine wakiuliza maswali kwa sababu vile vidogo vimetoka, mimi nina amani na Serikali ina-implement vitu vizito itaweza kui-implement bila kusema kule Vunjo kuna matatizo gani mbona huyu jamaa anasimama kila siku. Naomba Serikali ichukulie hilo na iweze kuvikamilisha vile vidogo.

Mheshimiwa Spika, tunaipongeza sana Serikali kwa miradi mikubwa iliyotekelezwa na tunasema kwamba hii miradi ina maana kubwa sana hasa hii tunayoizungumza ya huduma za jamii, mashule na hospitali na kadhalika. Nafikiri tuangalie vizuri kwamba je, the current costs implications zake zikoje. Unapojenga shule ufikirie OC na mishahara itakayotosheleza ile shule, iende ifanye kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, nafikiri kwamba hilo jambo ambalo kila saa nikiangalia najisikia na-shrink sana. Hivi itakuja kufika mahali kwa mfano leo naamini kama tungesema mahitaji yote ya Walimu, watoa huduma za afya na wafanyakazi wengine wa Serikali ambao wanatakiwa kwenye Wizara ambao hawapo kama wote wangepewa, tungepewa ile ikama kama inavyoombwa, naamini kwamba bajeti nzima isingetosheleza kukidhi mahitaji yale.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo naamini kwamba ni lazima tuangalie vizuri na tufanye uchambuzi vizuri, tusije tukaishia kukopa ili tule. Nakubaliana na mambo haya mnayosema inflation, kwani hii inflation niseme na ni lazima tujue, leo hii mfumuko wa bei Marekani na nchi za kanda za ulaya imefikia asilimia 7.5 kwa wastani.

Mheshimiwa Spika, ni mfumuko mkubwa kuliko wakati wote kuanzia mwaka 1982. Kwa hiyo hili ni suala la kidunia ni structural na kitu ambacho hatuwezi kuki-address kusema kwamba tunaenda kuomba pesa, ni kufanya nini, ni kukaza mikanda, this is the time to belt tighten, ni wakati kusema kwamba there is no way tutaepuka makali haya, kama ulikuwa unaenda jimboni kila siku nenda mara mbili, mara tatu kwa sababu hela utakayokuwa nayo haitatosheleza.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka kusema kwamba hilo ni jambo ambalo tuliangalie, sio kwamba ni letu na sio jambo la kufanya haraka haraka na sio kitu ambacho Benki Kuu inaweza ikashughulikia mara moja, haiwezi it is not monetary policy ya hapa ndani itafanya hicho kitu kwa sababu kinakuwa given na imported inflation.

Mheshimiwa Spika, sasa turudi hapa, ambacho nimepongeza kwenye hii miradi mikubwa, kuna kwa mfano hili suala la Vyuo vya VETE, naishukuru sana Serikali imeanza kutoa vipaumbele stahiki kwa VETA, vyuo hivi ambavyo vinatupa study na ufundi. Hata hivyo, naambiwa kwa takwimu ambazo sio rasmi, VETA ina upungufu wa Walimu 1400 na ni kabla havijaongezwa hivi vyuo vingine ambavyo vinakamilika kwenye mwezi huu wa Juni na mwaka unaokuja wanaweka vyuo vingine thelathini.

Mheshimiwa Spika, ukiweka pengine upungufu utakuja kuwa ni mkubwa sana wa watu, lakini sio tu upungufu wa Walimu, lakini ni upungufu pia wa vitendea kazi, vifaa vile vya kufundishia. Watu wanataka kujifunza cherehani, wanahitaji kushona kwa sababu sasa hivi tunavaa nguo zimeshonwa hapa, kwa hiyo lazima wawe na basic equipments kwenye hivi vyuo. Kwa hiyo, ni lazima tufikirie tunafanyaje pesa inatoka wapi ili tuweze kuhakikisha kwamba wanajenga ndiyo tusije tukajenga magofu, yaani kuwa na majengo tu it doesn’t help, haitasaidia.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu mkubwa nilitaka kuingiza kwenye uwekezaji ambao Mheshimiwa Rais wetu ameufanyia kazi sana na naamini utaanza kuona miradi mingi inasajiliwa. Wamesajili miradi 294 kutokana na hotuba tuliyopewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu na kweli kama miradi hii yenye kubeba thamani ya Dola Bilioni Nane itatekelezwa ajira zitaongezeka, kipato cha Taifa kitaongezeka, tutabakia kwenye kundi lile la watu walioendelea vizuri kipato cha kati na pengine tutaenda juu, lakini miradi hiyo inatakiwa kutekelezwa, tutafanyaje mimi nataka nishauri mambo matatu, manne.

Mheshimiwa Spika, kwanza nataka uwekezaji huu wenzetu majirani zetu wameanza kupunguza kodi ya makampuni, kwa sababu tunashindania wawekezaji hawa, wanapunguza kodi ya makampuni kutoka 30 kuja asilimia 25. Hiyo ni kivutio ambacho hatuwezi kukibisha hata tungesema tunafanya nini. Pili; kuna perception kwamba gharama za kuanzisha mradi hapa ni kubwa sana kumbe wala si kubwa sana ukilinganisha na kwingine, tatizo la watu kuona gharama hizi za uanzishaji miradi kubwa ni utitiri wa mamlaka zinazotoza tozo hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, utakuta kwamba kama tungeweka lamp sum tukasema kuanzisha kitu hiki ni Shilingi Milioni Moja unaenda kulipa kama ni TRA au mahali pengine lakini mamlaka nyingine zikagawiwa na huyo anayekusanya inakuwa ni rahisi mtu anajua kabisa ok, nataka kuanzisha kampuni ya simu ni Shilingi Milioni Tano basi its transparent and open and no need ushauri wa mtu. Kwa hiyo, mimi naomba hilo lifanyiwe kazi ili tuweze kupata wawekezaji hawa waje upesi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatu; ni suala zima nitalizungumza tena kwa bahati mbaya suala la riba ambalo najua mamlaka imeshatoa amri imeshatoa directive kwamba lishughulikiwe, lakini hatuwezi kupata wawekezaji ambao hawawezi kukopa ndani kwa sababu utakuja na mtaji wako ndiyo mashine na nini, lakini ule mtaji wa working capital lazima utoke kwenye mabenki ya ndani. Hasa huwezi kukopa kwa asilimia 16 wakati kule nje mtu anayezalisha kama huyo anakopa kwa asilimia tano uende ukashindane naye kwenye mauzo ya nje it is impossible! What you need ni kwamba lazima kweli au tuweke special windows na tunajua kwamba kuna watu wanataka kuongeza uzalishaji wao hapa kwa mfano kule NIDA tulikwenda, lakini hawawezi kukopa hapa ndani kwa sababu hiyo tu kwamba riba ni kubwa na wakipeleka kuuza vile vitu nje hawataweza kushindana kwa hiyo inakuwa matatizo, naomba hicho kifanyiwe kazi na tusichukue tu mzaha mzaha kwamba basi tu tuna njia ya kupunguza hizo riba, tunajua zipo! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niongeze kingine ni kwamba mimi naamini pia kwamba miradi mingine kwa mfano Bagamoyo Port, sijui Mchuchuma – Liganga, tunasema kwamba tatizo lililopo ni kwamba wanajadili vitu ambavyo hatuna, wanajadiliana maslahi ya Taifa letu tuyalinde lakini tuangalie maslahi mapana yanatokana au faida nzima zinazotokana na mradi ule kwa muda mrefu, tuangalie tusiangalie kesho utakosa ushuru wa kiasi hiki na hiki, kwa sababu huo ushuru huna anyway haupo kama ile kampuni haitaanzishwa wewe hutapata huo ushuru. Kama Bagamoyo port haitaanzishwa ianze kufanya kazi hutapata hicho kitu, kwa hiyo afadhali tukubali tuangalie tuwe na long term view ya issues badala ya kuwa na short term issues.

SPIKA: Ahsante sana muda wako umeshaisha Mheshimiwa.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana ninaunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana. (Makofi)