Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Ahmed Mabukhut Shabiby

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gairo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii, lakini kabla sijaongea masuala yangu ya bei za mafuta, kwanza nataka nitoe kabisa tahadhari kwa Mawaziri wa Wizara ya Maji kwamba nitachangia kwenye Wizara yake kuhusu habari ya mpango wa maji yale ya kutoka Changongwe kwenda Kata ya Lubeho, Kata ya Msingisi, Kata ya Gairo, Kata ya Kibedia na Kata ya Chakwale. Kwa hiyo najua bajeti iwekwe mapema. Vile vile kwenye TAMISEMI, Mheshimiwa Waziri Mkuu ni shahidi, Mheshimiwa Rais alipita pale Gairo na tulimwambia ile shida yetu ya kuhusu ule mfereji ambao unazuia mafuriko pale Gairo, lakini mpaka leo hatujawekewa bajeti kwa ajili ya ule mfereji ya kuzuia maji pale Gairo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, nataka niseme tu kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mawaziri wanafanya kazi nzuri na tunataka wafanye kazi bila woga ili waweze kumsaidia Mheshimiwa Rais. Nia ya Mheshimiwa Rais ni nzuri na tunaona kwenye majimbo yetu mambo yanavyokwenda, mimi ni Mbunge wa kipindi kirefu kidogo, lakini naona fedha zinazokwenda kwenye majimbo. Tunashuhudia barabara, tunashuhudia minara ya simu, tunashuhudia hospitali, tunashuhudia kila tu, ila nao wasibaki kusema tu mama kaupiga mwingi, huyu mama nilivyomsoma soma mimi hataki sifa sana, anataka kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mama kaupiga mwingi iendane na ufanyaji kazi wenu Mawaziri na kumsaidia kazi, wasije wakajidanganya kwamba mama anaupiga mwingi kwamba mwenzenu anapenda sifa sana mimi nilivyomsoma soma huyu sifa hataki, anataka kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachotaka kusema Watanzania kila kinachofanyika kama kuna wizi sehemu unakuja au wizi unafanyika, Watanzania wa sasa hivi wana akili wanajua kwamba hapa pana wizi umefanyika au wizi unakuja. Pakiwa na chochote kinachopitishwa kikiwa cha deal Watanzania wanajua kabisa, hili hapa ni dea,l si hawa Watanzania wa sasa hivi ni wale Watanzania wa zamani. Hapa niliongea miaka minne nili-spend sana kuongea habari ya mafuta, lakini imebidi tena na leo niongee, lakini miaka minne akina Ole-Sendeka ni mashahidi hawa, nilikuwa nazungumzia habari ya mafuta ya taa kufanywa malighafi kuchanganywa na diesel na petrol, akina mama Kilango wote walikuwepo hapa, miaka minne ndiyo Serikali imekuja kuchukua hatua za kuweka kodi kwenye mafuta ya taa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hapo mmeshuhudia wenyewe robo ya yale mafuta ya taa yaliyokuwa yanatumika hayatumiki, Serikali imepata mapato mengi imefanya vitu vingi sana. Hili suala tumechangia sana kwamba itakuja kuleta athari kubwa sana za kupanda kwa bei ya mafuta. Ule mpango wa bulk procurement wakati unakuja. Kuwa na vita Urusi na Ukraine kwa Tanzania ni fursa na kwa nchi zingine ni fursa ya kupata mafuta kwa bei rahisi, lakini kwetu sisi sasa imekuwa ni moto. Tulishasema na narudia kusema kipindi kile imekuja kampuni ya Li lance ya tajiri mmoja wa India anaitwa Ambani mwaka 2007 ilipokuja hapa Reliance iliponunua GAPCO na GAPWAY kwa ajili ya kuendesha biashara ya mafuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, Reliance ndiyo wenye refine kubwa sana duniani kipindi kile ndiyo ya kwanza hata hao Urusi hata Saudi Arabia hawana. Wao wana meli zao walipokuja hapa wakati wameanza kuleta mafuta, mafuta yalishuka zaidi ya shilingi 400 au 500 kwa lita kwa makampuni mengine yote walikuwa hawapati nafasi ya kuuza mafuta. Haya makampuni makubwa ya kizungu yanashirikiana na baadhi ya Wabunge wengine wapo upande wetu na mwingine alikuwa kiongozi kabisa wa chama fulani kule upinzani naye alikuwemo. Wakapiga deal kule, wale wajamaa wakawaambia bwana hebu sasa tunafanyaje huyu Reliance anashusha bei, na nini wakawaambia nyie hebu anzisheni mgomo hapo, msiuze mafuta hata siku mbili jifanyeni bei ndogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema vile vituo vilivyogoma kidogo wakaja huku, twendeni kule kwenye depots, sijui twendeni wapi, mbwebwe tu, kumbe wenzetu kuna ulaji. Baadaye tukaleta hoja maalum tujadili. Baada ya kujadili tukasema hakuna mtu binafsi kuleta mafuta, tununue kwa bulk procurement, matokeo yake ni nini? Ukishanunua mafuta kwa pamoja, sasa nani maana wote mnanunua bei hii halafu wote mnaleta mnapangiwa bei hii, sasa atakayeshusha nani, wote mnakuwa na bei moja, hakuna tena ushindani wa mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yule bwana akaamua kuuza kabisa, akawauzia TOTAL ile GAPCO na GAPWAY, maana yeye alitegemea ataleta mafuta yake atauza kwa ushindani kama alivyokuwa anafanya atashusha bei, lakini mnamwambia sasa bwana tunaenda kununua wote kwa pamoja, sasa ushindani uko wapi? Hebu kumbukeni angalieni kuanzia ile miaka ile kuna makampuni mpaka ya Watanzania World Oil ni ya Mtanzania, mtu wa Kigoma; hawa akina Vedasto Manyinyi huyu Mbunge wa hapa wa Musoma hawa nao walikuwa na kampuni yao; wako akina Barongo, watu wa Bukoba huko walikuwa na makampuni yao, watu kibao walikuwa na makampuni yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi ninavyokwambia kule deep sea kuna meli zinauza robo ya bei ya dunia yanatoka huko Urusi mengine yanatoka nchi zilizowekewa vikwanzo yako pale yanauza robo ya bei ya dunia, ukimruhusu mfanyabiashara wa binafsi yeye kazi yake anachokwenda pale ship to ship anachukua mafuta, meli kwa meli anapakia mzigo anakuja, ninyi watu wa huku wa EWURA, watu sijui wa Serikali, watu wa TBS, kazi yenu ilikuwa panga bei bwana, mafuta haya kwa bei ya dunia yasizidi hapa na TBS kiwango chetu tunataka hiki, yanatimiza kiwango basi, kwisha lakini unataka tu kupanga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naangalieni kwenye hiyo bulk procurement, watu wanakula pesa siyo mchezo, nchi hii inatumia lita milioni mia nne kwa mwezi. Sasa fanya tu wale kwenye ile Kamati wanachosema kwamba fulani nikupe tender ya kwenda kununua wakiweka dola tano tano wana shilingi ngapi? Hata dola mbili mbili wana bei gani? Tunachokizungumza hatukizungumzi kwa kukisia, lakini ukiongea sana hapa ukishika mishiko ya watu unasikia huyu Shabiby atakuwa mwizi wa mafuta huyu yaani nyie mnajuaga wizi wizi tu. Wakati wezi wako huko huko, ndiyo majambazi halafu wanatengeneza na nataka niseme kwamba kila kitu sasa hivi ni deal na kuna watu wachache ambao kazi yao ni kupanga deal kwenye hii nchi, sisi huku tunapelekeshwa tu, tunapitisha sheria kumbe sheria hakuna. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii mkiruhusu kampuni binafsi ziagize mafuta na kama mtu anaona kuna unafuu kama mnavyodai bulk procurement nayo iwepo, kama ataona kuna nafuu aende huko, kama ataona hamna nafuu alete yeye, Serikali kazi yake iwe kuangalia tu kiwango inachokitaka na bei inayotakiwa, lakini vitu vingine wanatunga tu utasikia ukileta mafuta mtu mmoja mmoja yatakuwa yanakwepa ushuru, meli zote zinashusha kwenye mita, zinashushia wapi? Hii kazi waachieni TRA, TRA ya nchi hii inafanya kazi nzuri, waaminini TRA lakini wao wanawapa kazi TRA wanakula deal. Sasa hivi tukiangalia toka ile bulk procurement mpaka sasa hivi ile mita imekufa mara ngapi? Imekufa mara nyingi kuliko wakati wanaleta watu binafsi ile mita ya bandarini. Naombeni sana turuhusu hayo bei ya mafuta itashuka kuliko tulivyotegemea na wala tusidanganyane na tusiwadanganye watu na watu wengine hata waliopo huko nje wasiwadanganye kwamba Serikali inaweza ikatoa kodi ya kwenye mafuta, ukitoa kodi nchini, hii mishahara haipo wala hakuna madawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunategemea hiyo kodi ya petrol tusidanganyane eti kodi sijui elfu moja na ngapi? Kodi yetu ndiyo inayotulisha sisi Serikali wala tusiwadanganye watu kama tunaweza kutoa kodi, kodi hatuwezi kutoa tunachotakiwa kufanya ni kupata mafuta kwa bei rahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine, dakika yangu moja imepotea kwa ajili ya makofi, naomba uilinde. Serikali imeleta matrekta yale matrekta yapo pale Kibaha yanaitwa Alice sijui Ursus yanaitwa nini? Serikali imewaletea wakulima kuja kuwaua, imeleta matrekta mabovu mimi sijawahi kuona toka nizaliwe, mimi ni mkulima nina trekta zaidi ya ishirini sijawahi kuona trekta inakatika katikati kichwa kinaenda peke yake matairi ya nyuma yanabaki peke yake. Haya matrekta yote ni mabovu, leo wamewatia watu umaskini hawa, huko yalikonunuliwa wapo wapi wale watu, hawajatoa guarantee? Yale matrekta leo wanasumbua wakulima wetu wanawadai wanataka kuwanyang’anya matrekta wao walikuwa hawana guarantee na yule aliyeagiza yale matrekta naye ashtakiwe, huwezi kuleta trekta kwanza ina jina la mama linaitwa Alice, halafu inakuja inasumbua, nenda unakuta dereva yupo mbele matairi yamebaki nyuma, kiuno kimekatika karibu matrekta yote hamna hata moja mikoa yote Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, halafu leo hii wanaandikiwa barua usipolipa tutakunyang’anya trekta. Mtu unamdai milioni 20, ukimnyang’anya trekta unaenda kulipiga mnada kwa milioni mbili kwa hiyo hapa pana kila aina ya njia ya wizi. Serikali iangalie namna ya kuwasaidia kuyatengeneza yale matrekta na wawasaidie namna ya kuwaongeza muda ili waweze kulipa yale madeni wanayodai. Vilevile wachunguze haya matrekta nani kaleta na yana mkataba gani na yana guarantee gani, maana yake trekta haiwezi kuwa na guarantee ya mwaka mmoja kama lori au kama basi au kama gari ndogo, linatakiwa liwe na muda mrefu. Kwa hiyo…

NAIBU SPIKA: Ahsante.

MHE. AHMED M. SHABIBY: Kwa hiyo naomba wayafuatilie hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)