Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutofuata Maelekezo ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia

Hon. Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutofuata Maelekezo ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii ya kuchangia hoja ya Kamati yetu na naishukuru Kamati kwa kazi waliyoifanya na mambo waliyoibua.

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe maelezo kidogo; la kwanza, Kamati inasema kwamba nanukuu kwenye taarifa; “kwamba wakati akitoa maelekezo yake Mheshimiwa Waziri alisema kwamba, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu inamkwamisha.”

Mheshimiwa Spika, niliyosema hapa yapo kwenye Hansard, sikusema maneno hayo nadhani ni kughafirika, naomba iondolewe kwenye taarifa.

Mheshimiwa Spika, nilipokutana na Kamati tulizungumza, niliwaeleza kwamba ile Kamati ya Kupitia Mikopo ilishaanza kazi na kwa kweli ilianza kazi kabla hoja iliyotolewa hapa kuhusu mikopo ya elimu ya juu na mtoa hoja wakati ule Mheshimiwa Ezra alinukuu siku naongea na vyombo vya habari, kwamba atakayekwamisha kazi ya Kamati hii nitakula kichwa. Nilisema vile kwa sababu nilikuwa nataka nione speed ya kazi inaongezeka. Sasa hata ukienda kwa whatever explanation kuanzia tarehe 12 Julai mpaka 31 Oktoba, 2022. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kamati ile ilikuwa tayari kufanya kazi mwezi Septemba, on record na ilipeleka proposal na ilikuwa tayari kufanya kazi mwezi Septemba, haikuanza kufanya kazi na wale watu wameajiriwa sehemu nyingine wakawa wametawanyika. Kamati iliniuliza, wewe Bodi imekukwamisha? Niliwaambia Bodi naimudu, ikinikwamisha mimi nitaishughulikia siji kushtaki Bungeni hapa na sikuishtaki Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakaniuliza ulitumia neno resistance, kwamba resistance uliyoiona inasababisha uamini kwamba huenda kuna madudu, ulikuwa unamaanisha nini na resistance? Kwa sababu sikusema Bodi wala sikuitaja, niliwaambia moja, sikuridhika na speed, nitaeleza kidogo.

Mheshimiwa Spika, pili, nilieleza na nilieleza hapa leakages za taarifa mitandaoni, ya barua zinazotoka kwenye Bodi na maelezo kwamba hapa Mkenda anafanya witch-hunting anataka kuweka Mchaga kuongoza, aache kufuatilia huku, yeye atafute hela ziongezeke zaidi. Sasa ile hisia huwezi kujua na hata sasa hivi siwezi kujua leakage inatoka wapi, lakini fact of the matter is, mimi kazi yangu na CAG ameeleza kwamba oversight ya Wizara kwenye Bodi ya Mikopo si nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kazi yangu ya ku- exercise oversight sio witch-hunting na uzuri clip zipo. Mara ya mwisho nilivyokutana na Bodi tarehe 5 Septemba nadhani, niliwaeleza sina haja ya kumuumbua mtu hii ripoti ni ya Waziri na ni ya Bodi. Tunataka kuangalia wapi tunaweza tuka-improve. Ripoti ni ya Waziri na ni ya Bodi, tunataka kuangalia wapi tunataka…

Mheshimiwa Spika, sasa mtu anapodhani kwamba ni witch-hunting au nataka kumwondoa mtu siwezi kuelewa.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri ngoja nikuongoze kidogo, ukitoa maelezo yale ambayo hayako kwenye hii taarifa na michango ya Waheshimiwa Wabunge kwenye hoja hii, utataka tena tufungue, watu watataka kujibu tena hoja hizo.

Na ile Bodi haitapata tena fursa ya kuanza kujibu haya, kwa hiyo, tutakuwa tunaenda mbele, tunarudi nyuma. Kwa hiyo, nikuombe ufafanuzi umepewa muda, hoja zile zilizotolewa na Wabunge hapa baada ya kuwa Kamati imeleta taarifa na zile za kwenye taarifa ambazo wewe unataka kuzitolea ufafanuzi ili tuwe tumejielekeza kwenye jambo lililo mbele yetu.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante na nitafanya hivyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwanza sikuja kuishtaki Bodi humu, sina haja ya kuishtaki Bodi, ninaimudu na wala sikusema kwamba Bodi inanikwamisha kama ilivyoandikwa hapa. Neno resistance nililieleza vizuri kwenye Kamati na nilieleza mambo ya speed, nilieleza mambo ya mitandao. Vilevile maelezo ambayo nilikuwa nimeyapata ambayo sikuridhika nayo na Kamati niliwaeleza vilevile kwamba waliambiwa na Kamati fulani ya Bunge kwamba Kamati yangu ivunjwe, tulipotafuta maandishi hatukuyapata.

Mheshimiwa Spika, kitu cha muhimu ni kwamba kazi imeanza tarehe 31 na lazima niseme ukweli Kamati inapata ushirikiano mkubwa sana na Bodi na nimeongea nao hata leo kwamba kazi inaendelea vizuri sana, wanaendelea. Watanzania wote wanaosikiliza wajue kwamba tutajaribu kuchambua na kuelewa kwamba tunavyogawa mikopo kama kweli tunagawa kwa haki, mahali ambapo pana upungufu tutaweza kuparekebisha.

Mheshimiwa Spika, lazima niseme vilevile kwamba suala kubwa ambalo hata CAG alizungumza na kila mtu alizungumza hapa ni suala la kugawa mikopo kwa haki. Kamati yenyewe hadidu za rejea kama ulivyouliza ya kwanza, kwa sababu ni wataalam wa mifumo na ni wataalam wa programming ni kwenda kuangalia takwimu na kuzi-program, kuhakikisha kwamba kila aliyeomba mkopo, sio some...

T A A R I F A

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, hii taarifa siipokei na nimeeleza kwamba at some point nilikuwa sijaridhika na speed ya utekelezaji. Ile Kamati ilikuwa tayari kufanya kazi mwezi Septemba…

T A A R I F A

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, nilikuwa sijaridhika na speed ya kazi, nikatoa onyo public, siyo humu Bungeni na kazi ikaanza na ushirikiano ni mkubwa na ndio jukumu langu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilizungumza in public na labda ni-quote maneno; “kwamba atakayekwamisha Kamati hii nitakula kichwa” iko ndani ya uwezo wangu na nilizungumza hivyo…

T A A R I F A

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nimekuelewa na nakushukuru kwa mwongozo wako.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo yako mambo yangu ya kazi yangu niliyasema nje ya Bunge, wakati naongea na press na yale niliyoyasema humu na yale niliyoyasema humu nilijaribu kuyafafanua kwenye Kamati kwamba yalikuwa na maana gani kama nilivyoeleza ni hayo nilikuwa najaribu kuyaeleza. Lakini bado tunarudi tena kwenye hoja ya msingi kwamba, kazi ya ile Kamati ni kujaribu kuhakikisha kwamba mikopo ya wanafunzi inagawanywa kwa haki. Nadhani hata ukiangalia kwenye ripoti ya CAG imesema wako yatima ambao wamekosa mikopo. Kwa hiyo, kazi ile na Waheshimiwa Wabunge wakati tunajadili bajeti yetu hayo mambo yalikuwepo na Wabunge wengi walipenda tuyafanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, cha muhimu sasa hivi ni kwamba kazi inafanyika na ushirikiano upo na ile Kamati imetoa communication strategy, mtu yeyote mwenye taarifa za ziada atapeleka kwenye Kamati. Naamini kazi itakapokamilika tutakuwa na fursa nzuri sana ya kuboresha namna ya kutoa mikopo. Kwa hiyo, hilo ni kubwa na nadhani hatutakiwi kutoka kwenye reli.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, labda nieleze kidogo tu kuhusu TOR ambazo ulikuwa umesema hadidu za rejea, sijui kama ni wakati wake wa kuzieleza hapa, kwa sababu kazi kubwa ile ni compliance, kwamba vigezo ambavyo vimetangazwa, mwombaji anapoomba mkopo anavisoma kwenye tovuti, kwamba nikiwa na hivi naweza nikapata mkopo. Je, ukiomba na unakidhi hivyo vigezo unapata mkopo? Kama nilivyosema wakati ule hata kama vigezo hivyo bado vina mashaka, ni vizuri kwanza tuvitendee haki tufanye hivyo.

Mheshimiwa Spika, la pili, tunahitaji na iko kwenye CAG Report kuangalia taarifa zipi za ziada tunaweza tukazitumia kwa ajili ya ku-improve means testing na hii wanaifanya. Tumefanya kazi na Bodi kama ninavyosema na wenyewe wameongeza TOR zao kwa sababu kuna kazi wanataka kuifanya na niliridhia na nataka kutoa tena taarifa hapa, Kamati ipo kazini, inafanya kazi vizuri, speed nilikuwa sijaridhika nayo, sasa hivi ninaridhika na kazi inavyokwenda na Bodi. Nisiporidhika hatua za kuchukua zipo ndani ya mikono yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. (Makofi)