Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutofuata Maelekezo ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutofuata Maelekezo ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Spika, nakushuru kwa kunipa fursa hii nami nichangie hoja ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimemsikiliza vizuri sana msomaji wa taarifa mbele yetu. Katika taarifa hiyo imeonekana wazi kabisa kwamba Waziri mwenyewe kwa kauli yake kama alivyonukuliwa na muwasilishaji akisema kwamba anajukumu la kuisimamia bodi lakini pili bodi haijakaidi maelekezo yake. Pia on Hansard Waziri huyo huyo hapa mbele ya Bunge lako Tukufu, jambo lililopelekea mpaka ukatoa maelekezo aende kwenye Kamati akahojiwe.

Mheshimiwa Spika, pia on Hansard, Waziri huyo huyo hapa mbele ya Bunge lako tukufu, jambo lililopelekea mpaka ukatoa maelekezo aende kwenye Kamati akahojiwe na Kamati iwasikilize watu wote, iweze kutuletea taarifa ambayo leo tunaijadili hapa; ulimsikia na tulimsikia sote hapa ndani on Hansard akisema kwamba Bodi imeweka resistance kubwa, imekataa maelekezo yake na pengine kuna kitu kilichofichika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hizi ni kauli tata za Waziri huyu huyu mmoja; moja, ndani ya Bunge, ndani ya Kumbukumbu Rasmi za Bunge; pia kauli nyingine kwenye Kamati na kauli zake zinapingana hata saa 72 hazijapita. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa muktadha huo, ni dhahiri kwamba Waziri amelidanganya Bunge lako Tukufu kwa kusema uongo ndani ya Bunge. Pia uongo aliousema Mheshimiwa Waziri hapa Bungeni, umeleta taharuki ndani ya Bunge, ndani ya Umma wa Watanzania na zaidi kwa watoto ambao wanasikiliza Bunge kwa matumaini makubwa juu ya hoja yao ya msingi kwamba ni namna gani Serikali yao itawapatia mikopo waendelee na masomo yao ya elimu ya juu. Kwa hiyo, Waziri hakuwa makini na taarifa ambayo alikuwa anaipeleka kwenye jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika utangulizi huo, naomba Waziri aliombe radhi Bunge lako Tukufu; pili, awaombe radhi wananchi kwa kusababisha taharuki kubwa iliyojitokeza; tatu, nilikuwa naomba Waziri mwenyewe ajitathmini kama anatosha kuwa mwakilishi wa Rais kwenye usimamizi wa sekta hii. Kama hii ndiyo taswira anayoipeleka mbele ya Bunge Tukufu na kwa Umma, ajitathmini kama bado ana hadhi na uhalali wa kuendelea kumsaidia Mheshimiwa Rais kwenye nafasi hiyo. Kama akiona hawezi, ampe fursa Mheshimiwa Rais aweke mtu mwingine anayeweza kumsaidia vizuri kwa sababu yeye ni dhahiri ameshindwa kusimamia sekta yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni jambo la kuiaibisha Serikali kuona kwamba Mheshimiwa Waziri anatamka mbele ya Bunge; kwenye Kumbukumbu Rasmi, ndani ya vyombo vya habari vyote na Umma wote ukimsikiliza kwamba taasisi anayoisimamia imekaidi maelekezo yake. Hata kama ingekuwa imekaidi, nisingetarajia Waziri wa Serikali kuja kulalamika ndani ya Bunge. Kuna machinery za kiutendaji na kiutawala ndani ya Serikali yenyewe za namna ya kuchukua hatua dhidi ya watu wanaokaidi viongozi wao wa juu, watu wanaokaidi maelekezo yanayotolewa na Serikali, kuna namna za kiutawala za kushughulika na mambo hayo na siyo kuja kulalamika Bungeni.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Kigwangalla, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Getere.

T A A R I F A

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri samahani. Nilitaka Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla a-declare interest kwamba alipokuwa Waziri wa Maliasili na Utalii alikuwa na mgogoro na Katibu Mkuu wake ambaye kwa sasa ni Waziri wa Elimu. (Makofi)

MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa mwongozo huo. Kiukweli namshukuru pia Mheshimiwa Getere kwa kulileta hili. Sina maslahi yoyote kwenye jambo hili, lakini kiuhalisia ni kwamba tumefika hapo tulipofika kwa sababu Mheshimiwa Waziri ametumia, yaani kufanya personal attack dhidi ya Bodi ya Mikopo kuja kulidanganya Bunge, kwamba Bodi imemgomea na vitu kama hivyo, badala ya kutafuta suluhu ya tatizo la msingi ambalo ni bajeti ndogo kwenye mikopo ya elimu ya juu.

Mheshimiwa Spika, ni utaratibu huo ambao ulipelekea kwenye hilo ambalo umekuwa ukilisema kwamba yeye anapenda migogoro, ugomvi na ku- attack watu binafsi badala ya kufanya kazi.