Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Elly Marko Macha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DKT. ELLY M. MACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha tena kuwa na afya njema ya kuchangia hoja ambayo inachangiwa sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda kukupongeza, kwanza kwa kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii ambayo mimi ni Mjumbe na pia kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bunge. Hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, napenda kuwapongeza Waziri wa Afya, Naibu Waziri pamoja na timu yake yote kwa kazi njema wanayoifanya na kwa hotuba walioiwasilisha mbele yetu ambayo sasa tunaijadili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita katika masuala matatu; suala la kwanza, ni kwamba jana na leo Waheshimiwa Wabunge mbalimbali wamezungumzia suala la watu wenye ulemavu mbalimbali katika Wizara hii. Sipendi kurudia ambayo yameshazungumzwa, nina imani kwamba Mawaziri wanaohusika wame-take note ya hayo yote, lakini napenda kwenda mbele zaidi kuwasilisha ombi kwa Wizara hii kwamba kuna umuhimu sana Waziri anayehusika Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Naibu wake baada ya Bunge hili kwenda kuanzisha desk ama focal point kwa masuala ya watu wenye ulemavu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ulemavu ni cross-cutting na japokuwa mambo ya walemavu yako chini ya Waziri Mkuu, lakini Wizara zote na critically ni Wizara ya Afya, inatakiwa kuwa na department au kuwa na desk au focal point kwa ajili ya masuala ya watu wenye ulemavu. Ni kwa nini? Kwanza tukumbuke kwamba ulemavu unasababishwa aidha kwa kuzaliwa nao ama unapatikana kutokana na magonjwa mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba Waziri na Wizara yake amelipa kipaumbele suala la kinga, kwa sababu kunapokuwa hakuna kinga, ndipo magonjwa mengi yanasababisha ulemavu. Kwa hiyo, ni critical hii Wizara iwe na professional advice kwamba masuala ya walemavu yawe katika muundo wa Wizara. Mambo ya Waziri Mkuu kule yaliko ni mambo ya sera, mambo ya sheria, mambo ya ushauri, lakini mambo ya huduma, mambo ya matibabu, mambo ya kinga, yanatakiwa yashughulikiwe kikamilifu na Wizara ya Afya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ulemavu nimesema ni profession, kwa hiyo, naomba Wizara inayohusika iwe na kitengo au department ambayo itakuwa inashauri kuhusu mambo ya ulemavu, kwa sababu kuna watoto wenye ulemavu, wanapokuwa na matatizo itakuwa vipi? Kuna wazee wenye ulemavu, kuna masuala ya jinsia; mambo ya wanawake wenye ulemavu. Kwa hiyo, ni muhimu sana Wizara hii ikiwa na idara ama kitengo ambacho kitashughulikia masuala ya ulemavu ili kumshauri Waziri pamoja na timu yake jinsi gani ya ku-deal na masuala haya yanayotokana na ulemavu kutokana na jinsi Wabunge walivyochangia hapa tangu jana na leo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo napenda kupata ufafanuzi kutoka kwa Waziri ni suala la watu wa Ustawi wa Jamii. Sijui watu wa Ustawi wa Jamii wako wapi! Sijui kama wameunganishwa na Maendeleo ya Jamii; lakini nina imani kwamba bado wako katika Wizara hii. Kuna Maafisa Ustawi wa Jamii Mikoani, Wilayani na mpaka kwenye ngazi za Mitaa. Sasa hawa wana-belong katika Wizara gani? Kama wana-belong katika Wizara hii, role yao ni ipi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kugusia suala la watoto, kuna vituo mbalimbali hapa nchini kwetu ambavyo vimeanzishwa kwa ajili ya kuhudumia watoto yatima na suala la watoto yatima linahudumiwa na Mashirika ya Serikali na pia yasiyokuwa ya Serikali. Kuna NGOs nyingi ambazo zimeanzisha vituo na centre za watoto yatima, lakini katika vituo hivi, pamoja na kwamba kuna wengi wana nia nzuri ya kusaidia watoto yatima, lakini pia kuna mambo mengine ambayo hayastahili, yanaendelea kwenye hivyo vituo vya watoto yatima. Kuna vituo vingine vya watoto yatima ambapo kuna child abuse sana inaendelea na vingi pia viko chini ya wafadhili wengine kutoka nje ya Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wafadhili wengine wamekuja hapa wakianzisha vituo hivyo, wana nia njema, lakini kuna wengine wana agenda zao katika hivyo vituo. Wanakuwa wanapiga picha wale watoto, wanawapeleka kwao kwenda kufanya fundraising na wanapata pesa nyingi; na wanapokuja na pesa hizo utakuta wanawaleta watu wa kwao wengi in the name of volunteers; na wale Watanzania ambao wameajiriwa katika hivi vituo wanalipwa pesa kidogo sana na pesa nyingi walizo-fundraise wanawalipa wale watu wa kwao waliokuja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naishauri Wizara kwamba kuna haja ya kuwa na monitoring mechanism ya kuhakikisha kwamba wale wanaoendesha hivi vituo vya watoto yatima kweli wahakikishe vinaendeshwa katika misingi inayokubalika na wale watoto wasitumike katika ku-fundraise kwa ajili ya faida yao, bali ile fundraising inayofanyika itumike katika kuendeleza watoto hao na katika kuwalipa Watanzania vizuri wanaofanya kazi katika hivyo vituo vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo lingine pia katika vituo hivi nilivyosema. Kwa mfano, kule Arusha kuna kituo kimoja kiko chini ya Wamarekani, wale Wamarekani wanaoendesha kile kituo cha watoto yatima, watoto wanapougua pale hawawapeleki hospitali, wanasema tuwaombee. Ilitokea hata mwaka 2015 mtoto mwingine alikufa. Kwa hiyo, kuna hizo imani kwamba watoto tuwaombee na hakuna kuwapeleka hospitali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni child abuse na kama Wizara haita-monitor mambo kama hayo tutakuta watoto wetu wengine ambao ni yatima wanafanyiwa vitu ambavyo havistahili. Kwa hiyo, kuna haja ya kuwa na monitoring system ambayo inaeleweka ku-control hawa ambao wanaendesha hivi vituo, ambao wana nia nzuri waeleweke na wale ambao wana nia mbaya pia waweze kugundulika ili vitendo kama hivyo vikomeshwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kuzungumzia suala la Benki ya Wanawake. Naiomba Wizara na Waziri, Mheshimiwa Ummy, kwamba hii Benki ya Wanawake kuna affirmative action gani ambayo imechukuliwa kuhakikisha kwamba wanawake wenye ulemavu nao wanafaidika na mikopo na huduma za hiyo Benki. Kama hakuna affirmative action tutaendelea labda kusema hapa. Lilionekana hili ni suala la Wabunge wenye ulemavu, lakini hili ni suala la kila mwanamke na Waziri pia na aliweke katika mikakati yake awe na affirmative action ya kuhakikisha kwamba wanawake wenye ulemavu nao wanafaidika na mikopo ya hiyo ya Benki ya Wanawake iliyopo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo napenda kuchangia ni kama nilivyosema, jinsi gani watu wanapata matatizo katika hizi bodaboda. Mheshimiwa Waziri alieleza katika hotuba yake kwamba kuna pesa zimetengwa katika kuimarisha kile kituo cha MOI pale Muhimbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuimarisha kituo cha MOI, lakini pia kuna haja kuwepo na mikakati madhubuti kwa ajili ya kuelimisha hawa waendesha bodaboda ambao kwa kweli kwa upande mmoja ni ajira ambayo wamepata vijana wengi lakini kwa vile hakuna mafunzo yanayotolewa, ajali ni nyingi na ulemavu unasababishwa siku hadi siku, watu wengi wanavunjika, watu wengi wanazidi kulemaa kutokana na hizi bodaboda.
Kwa hiyo, nafikiri kuna haja ya kuwa na mkakati wa kutoa elimu kwa hawa wanaofanya hii biashara ya bodaboda ili kupunguza wale watu wanaoathirika katika kulemaa kwa ajili ya ajali mbalimbali zinazosababishwa na hizi bodaboda, ni tatizo kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumalizia hapo. Nashukuru sana.