Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kushukuru sana kwa fursa hii ili kuchangia taarifa hizi za Kamati tatu. Napenda kupongeza sana Kamati zote tatu, Wenyeviti na Wajumbe kwa ripoti zao nzuri sana ambazo kwa kwa kweli kama nitakavyoeleza baadaye maazimio yao, recommendations zao tunazikubali kwa Wizara ya Elimu na nyingine tumeanza kuzitekeleza. Napenda vilevile kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote ambao wamechangia mjadala huu na maoni yao ambayo yamegusa Sekta ya Elimu hasa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia tumeyabeba na mengine nitajaribu kuyatolea maelezo kidogo. Kwa hiyo mchango wangu pengine utakuwa nia mfupi kidogo.

Mheshimiwa Spika, naomba niungane na wenzangu vilevile kumpongeza sana Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan hasa katika Wizara yetu ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mambo makubwa sana ambayo yamefanyika kwa kipindi kifupi ambacho amekuwa Rais wa Nchi yetu, ujenzi wa shule nyingi wote tunauona, ujenzi wa vyuo kwa mfano sasa hivi najua kila Mbunge tukiongea naye anaulizia kuhusu VETA, lakini makubaliano tumeshafanya na Hazina kwa maelekezo ya Rais wetu ni kwamba fedha tuliozonazo za VETA zitajenga VETA katika kila wilaya ambayo sasa hivi haina VETA mradi tupate ardhi. Vilevile ujenzi wa campus ya Vyuo Vikuu katika mikoa 14 ambayo ilikuwa haina campus ya Vyuo vikuu. Kwa hiyo mafanikio haya na yenyewe ni mazuri sana yanaleta vilevile changamoto kwa sababu tunaongeza idadi ya wanafunzi ambao wanahitaji fursa ya kusoma na kazi yetu kubwa ni kupambana na hizo changamoto. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala kubwa ambalo limezungumzwa hapa ni kuhusu Bodi ya Mikopo kwa Elimu ya juu na nitajaribu kuelezea kwa kifupi yale ambayo yameelezwa na Kamati na yale ambayo tunakusudia kuyafanya. CAG mwenyewe ametoa recommendation kubwa kwamba tufanye maboresho ya Sera na Sheria ya Bodi hii na vilevile tuhakikishe kwamba Wizara inaongeza usimamizi na kuimarisha mfumo wa kitaasisi kwa ajili ya kuimarisha bodi hii. Mambo mengine ambayo yametajwa na CAG ambayo yamerudiwa na PAC ni masuala kama vile kugundua yatima ambao waliomba mikopo ambapo kwa vigezo ambavyo vilitakiwa vitumike, walitakiwa wapate mikopo, vilevile kasi ya kushughulikia rufaa kwa mtu ambaye ameomba mikopo, lakini hakuweza kupata na nadhani kwamba kwa vigezo ambavyo vimetangazwa angeweza akapata na vilevile kuangalia wale wanaostahili.

Mheshimiwa Spika, CAG vilevile amezungumzia kuhusu endapo mini testing yaani mfumo tunaotumia kutambua nani apewe mkopo na apate kiasi gani kama kweli tunatumia taarifa za kutosha kuweza kuhakikisha kwamba kweli tunawalenga wale ambao tunahitaji kuwapata.

Mheshimiwa Spika, taarifa vilevile ya PAC imepitia humo humo na maazimio ambayo wameyapendekeza yapo katika mfumo huo huo. Mambo kwa mfano ya sera na sheria, vilevile mfumo wa usimamizi na kwa sababu taarifa zote mbili zinazungumzia umuhimu wa Wizara kuhakikisha kwamba inafanya usimamizi wa bodi na kusimamia vilevile mfumo wa kitaasisi na PAC ina- recommend vilevile Msajili wa Hazina naye a-play role yake katika kuimarisha suala hili.

Mheshimiwa Spika, mengine ambayo yamezunguzwa na PAC ni pamoja na hilohilo la mini testing ambayo inatumika wanaona kwamba pengine inahitaji taarifa nyingi zaidi na imetambua kwamba mahitaji ya mikopo kwa kweli yanaongezeka sana na yameongezeka zaidi baada ya nyongeza kubwa ya bajeti ambayo ilifanyika mwaka jana.

Mheshimiwa Spika, kuna lingine moja hapa ningependa nilizungumzie kidogo, kwenye taarifa ya PAC nili-clarify kidogo tu, kwa sababu katika ripoti pameelezwa kwamba mini testing inaangalia needs kwa ajili ya kujua nani anaweza akapata mkopo na haiangalii aina ya shahada mtu anayeisoma na tutahitaji kuweka maelezo vizuri zaidi kwa sababu ziko cluster tatu. Cluster ya kwanza inapewa upendeleo zaidi; ya pili upendeleo wa pili; na ya tatu. Kwa hiyo inaangalia mahitaji ya kaya na mtoto anakotoka na vilevile ni masomo gani anaenda kuyasoma? Hivyo ndiyo vigezo vinavyotumika, tunahitaji pengine kuweka ufafanuzi ili viweze kueleweka vizuri zaidi hapa.

Mheshimiwa Spika, wakati wa mjadala huku kumekuwa na masuala mengi vilevile ya kuelezea umuhimu wa kuhakikisha kwamba kuna haki katika kugawa mikopo. Kwanza nianze kusema kwamba tangu tuanzishe Bodi ya Mikopo kumekuwa na uboreshaji wa namna ya kugawa mikopo na nitatoa mfano.

Mheshimiwa Spika, hapo mwanzo taarifa zilizokuwa zinatumika zilikuwa haziingizi taarifa kwa mfano ya TASAF, sasa hivi Bodi ya Mikopo inaruhusu kuchukua taarifa moja kwa moja kwa mwombaji wa mkopo ambaye anatoka kwenye kaya ambayo imeonekana ina mahitaji ya kusaidiwa na TASAF moja kwa moja achukuliwe kama ni anatoka kwenye kaya yenye uhitaji mkubwa kwa hiyo, anapewa upendeleo hivyo hiyo ni taarifa ya ziada ambayo inatumika sasa hivi. Pia Bodi ya Mikopo sasa hivi imefungamana na RITA kwa mfano kwa ajili ya kutambua watoto ambao ni yatima kwa hiyo, ukitoa taarifa yako inaweza ikawa verified mara moja na hali ikaenda vizuri. Hivyo, kumekuwa na improvement mwaka hadi mwaka ikiwa ni pamoja na jitihada za kuongeza makusanyo kwa wale ambao walinufaika na mikopo kuhakikisha kwamba wanarudisha mikopo yao.

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

T A A R I F A

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa Taarifa Mheshimiwa Waziri kwamba, katika hicho anachoongelea kuhusu uboreshaji wa utoaji mikopo na amesema moja ya improvement yao ni kuingiza taarifa za TASAF. TASAF bado yenyewe kule kuna shida kubwa kwamba mpaka hata hao wanaopewa hiyo fedha au ule unafuu wa kusaidia kaya maskini kule kwenye TASAF kwamba, wapo wanaopewa ambao siyo wenyewe ama wanapewa ambao siyo walengwa. Wapo ambao wanao uwezo na bado wanaingizwa kwenye TASAF. Tunayo malalamiko hayo mengi, kwa hiyo, nadhani pia taarifa za TASAF haziwezi kufanya improvement kubwa kwenye mikopo. Ahsante. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, unaipokea taarifa hiyo?

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba niipokee taarifa hiyo kwa maana kwamba, Serikali tuna haja ya kuboresha maeneo yote kuhakikisha kwamba, taarifa ambazo zinakusanywa ziko sahihi, lakini hii hatua ya bodi ya kuanza kutumia Taarifa ya TASAF ni attempt ya kuhakikisha kwamba tunapata taarifa nyingi zaidi kumtambua mtoto mwenye mahitaji, lakini kwa kweli mfumo mzima unahitaji kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, sasa nizungumzie suala lile la sera ambalo naona liko katika mapendekezo ama maazimio hapa. Kweli, kwamba, kuna haja ya kupitia sera na matokeo ya kisheria ya higher education financing hapa nchini pamoja na mfumo wa kitaasisi. Sasa hivi tunapitia sera ya elimu na ninapenda kutoa taarifa kwamba ni kama tumeshamaliza mapitio ya sera sasa hivi, tunasubiri tu mfumo wa approval ndani ya Serikali halafu tutatoa almost like a white paper kwa ajili ya majadiliano ya mwisho kabla ya kwenda kufanya maamuzi kupitia Serikali nzima na suala hili la namna ya ku-finance higher education ni suala ambalo limezingatiwa katika mapitio ya sera na kwa hiyo, liko kwenye azimio hapa nasi tayari tumeshatangulia tunakwenda hukohuko. Hiyo, itaendana vilevile na kupitia mapitio ya Sheria ya Elimu pamoja na sheria nyingine ambazo zinahusiana na utoaji wa mikopo kwa elimu ya juu.

Mheshimiwa Spika, vilevile suala la Wizara kuongeza oversight kwenye Bodi. Progress imekuwa ikiongezeka lakini sasa hivi tutazingatia zaidi, vilevile kupitia mfumo wa kitaasisi ambao utatuhakikishia kwamba kwa kweli tuna- improve kwa sababu kila siku kuna room ya ku-improve. Suala moja kubwa ambalo ningependa nilizungumzie kama ambavyo limezungumzwa na Waheshimiwa Wabunge wengi hapa ni suala la kuhakikisha kwamba mikopo inagawanywa kwa haki.

Mheshimiwa Spika, wengi wamelizungumza na kwenye taarifa ya CAG ameeleza, watu ambao wanapewa mikopo ambao yeye alivyowaangalia kama sample ameona kwamba hawakustahili kupata mikopo, wengine wamepata mikopo zaidi kuliko walivyostahili, hili ni suala ambalo na sisi tunalitilia umakini sana. Wakati nilipozungumza hapa mara ya mwisho, nilizungumza kwamba tumeweka Kamati ya wataalam wa mifumo na takwimu, wanaweza wakafanya programming kuweza kuchukua takwimu zote na kuzichakata na kuzi-cluster kuangalia vigezo na kuhakikisha kwamba, tunahakiki kweli wale waliopata mikopo kama wanakidhi vigezo ambavyo vilitangazwa. Inawezekana vigezo hivyo tusiridhike navyo, lakini madhali ndiyo vilivyotangazwa tunataka kuangalia compliance yake ikoje.

Mheshimiwa Spika, Pili, Kamati hii itaangalia vilevile ni taarifa zipi za ziada ambazo tukizitumia zitaongeza ubora wa mini-testing kama ambavyo CAG mwenyewe amesema tunahitaji kuboresha taarifa hizi.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa taarifa hapa kwamba Kamati imeshaanza kazi, inaendelea na kazi kwa bidii kabisa na itafanya kazi hiyo itamaliza. Kamati hii kwa sababu ina wataalam wa mifumo, takwimu na programing, siyo watu wa kwenda kufanya sampling, ni watu ambao wanaweza wakakaa kuandika program na kuchakata takwimu zote za watu ambao wameomba mikopo na kuhakikisha kwamba, wanajua kama tumekuwa tukizingatia vigezo ili tuweze kupata recommendations tujue tunakwendaje.

Mheshimiwa Spika, sote wote kama Serikali tunajua umuhimu kwamba fedha zilizopo kwa ajili ya mikopo kila mtu anasema hazitoshi, zitaongezwa zitakuwa hazitoshi, zitaongezwa hazitoshi, basi kile ambacho tunacho kigawanywe kwa haki, anayepata mkopo awe kweli yule anayestahili na ambaye kwa kweli anajiwezaweza kama fedha hazitoshi asije akaingia kule.

Mheshimiwa Spika, suala hili tusipolizingatia malalamiko yatakuwa makubwa sana. Kwa hiyo, napenda kusema Kamati iko kazini na imeongezewa nguvu leo, vilevile itakuwa na fursa ya kutangaza kwa watu wenye taarifa za kupeleka kwenye Kamati, nje ya takwimu zilizopo kule watazipeleka kwenye Kamati tutapata taarifa hatimae tutajua tuweze kuongeza nini katika yale tunayofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mambo mengine ya ziada ni pamoja na kama nilivyosema pale kwamba, mikopo ya elimu ya juu kama CAG alivyosema ni kweli tunahitaji kutafuta vyanzo vingi zaidi. Kulikuwa na recommendations huko mwanzo kwamba tuweze kutoa mikopo hata kwa wale wanaofanya Diploma. Kwa sasa hivi tumeznza na NMB tumepata Bilioni 200 na masharti yake, ingawaje masharti nafuu sana kwa mikopo ya elimu, lakini tutaendelea kufanya hivyo kuhakikisha kwamba, tunaboresha education financing hapa nchini, hasa higher education financing na financing hasa kwa hivi vyuo vya kati kama VETA na vingine vya ufundi.

Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana kwa muda. (Makofi)