Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi; na niungane na Wabunge wengine kukupongeza kwa unavyouendesha mjadala huu. Kwa kweli kama kuna mjadala ambao umefanyika kwa ufanisi sana. Ni mjadala huu wa ripoti ya CAG; na si kwa bahati mbaya, kwa sababu hii ndiyo imebeba kila kitu cha nchi hii, kwa hiyo nikupongeze sana, I am very proud, as your student, I am very proud. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwapongeze sana Wajumbe wa Kamati hizi zote tatu, LAAC, PIC na PAC, kwa kweli wamefanya kazi nzuri sana, na ni kazi ngumu kwelikweli. Mimi nadhani mwaka mmoja uliopita halmashauri yangu iliitwa kwa hiyo nilishuhudia mahojiano kati ya Kamati yetu ya LAAC na halmashauri; inafanana kabisa na process zile za cross-examination za mahakama, ni nzuri sana. Kwa hiyo kwa kweli tuwapongeze sana.

Mheshimiwa Spika, nimejaribu kuangalia zile ripoti zota za CAG, takriban repoti 17, kama zote tutazifuatilia, pages 3,632. Hii maana yake nini? Ni kwamba, huko mbele ili tuweze kupata muda mzuri wa kuchangia vizuri, labda pengine tuangalie pia muda ili Wabunge waweze kuchangia. Niwapongeze Wabunge wale wote ambao wamepitia ripoti hizi, kwa kweli kazi nzuri sana wamefanya.

Mheshimiwa Spika, mimi nazipongeza pia halmashauri zilizofanya vizuri. Wale ambao wamefanya vibaya tuweze kuwasema sana. Tusipo shughulika na wale wanaofanya vibaya inaondoa uzalenda wa wale wanaofanya vizuri, kama alivyokuwa anasema Mheshimiwa Shigongo. Lazima wanaofanya vibaya waadhibiwe.

Mheshimiwa Spika, Jaji mstaafu wa Kenya aliwahi kusema hivi, “the greatness of any nation lies in its fidelity to the its constitution and adherence to the rule of law but above all respect to God”.

Mheshimiwa Spika, CAG ameshafanya kazi yake ya kikatiba na ameonesha madudu ambayo yamefanyika kila mahala. Kazi iliyobaki ni ya Bunge. Bunge liko kwenye trial wanasubiri sasa kuona Bunge litachukua maamuzi gani. Kwa hiyo, kwa kweli tufanye maamuzi ambayo yatasaidia nchi hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama walivyosema Wajumbe wengine hapa, Mheshimiwa Rais anafanya kazi nyingi sana, anahangaika kila mahala kutafuta pesa kwaajili ya miradi ya Tanzania. Lakini ukisoma ripoti hizi, na ukaangalia mfano tu wa zile fedha alizotafuta kwaajili ya miradi ya UVIKO, ilivyoleta heshima kila mahala nchi hii, halafu unaambiwa ni TirionI 1.3 tu; lakini ukisoma ripoti hii unaambiwa kuna zaidi ya Tirioni 1.8 zimepotea. Maana yake kwamba, kama hizi fedha tungeweza kupeleka kwenye miradi mingine heshima yetu ingekuwa kubwa zaidi na zaidi.

Mheshimiwa Spika, hakuna kitu kimenisikitisha sana kama unakuta unaambiwa eti kuna halmashauri 47 wamenunua dawa zimeharibika. Fedha zimetumika na maisha ya Watanzania tunayaweka kwenye wakati mgumu wa kuwa na dawa ambazo zimeharibika, this is shame. Kwa hiyo si tu kwamba fedha zao zimepotea lakini wanaweza pia wakapata madhara ya afya kutokana na dawa ambazo zimeharibika.

Mheshimiwa Spika, nilitaka pia kupata clarification kwa ripoti hii ya CAG, ukurasa wa tano. Kwenye ku- summarize zile recommendation, wanazosema 10,824 kwenye jedwali namba mbili wanasema utekelezaji unaendelea kwa recommendation 10,864.Lakini paragraph iliyopo juu hapo, wanasema mapendekezo 1,864 sawa na asilimia 17 hayajatekelezwa, lakini ukiangalia kwenye chati ambayo hayajatekelezwa ni 3,637, nadhani hiyo confussion lazima iwe clarified ili tujue. Kwa sababu hapa ni kama ime swap kidogo.

Mheshimiwa Spika, habari za halmashauri zimezungumzwa hapa na sisi tunakutana hapa kama wawakilishi wa wananchi, na kila mahala tunakokwenda hakuna maji, hakuna barabara, hakuna zahanati hakuna vituo vya afya, madarasa, madawati halafu ukiambiwa kuna fedha zinapotea na watu wapo na Sheria zipo ni hatari kidogo.

Mheshimiwa Spika, ukisoma ripoti hii, Mheshimiwa Attorney General ambaye kwa kweli namheshimu sana, I think is the only man, amekuwa DPP amekwenda judicial na Sasa ni Attorney General na is the most qualified, by the way. Naomba ulisaidie Bunge hili, next ripoti tusipate ripoti inayo tokana na mikataba ambayo inafungwa fungwa kwa ajabu ajabu. Bunge hili lilifanya mapinduzi ya sheria kwa kufanya wanasheria wote kuwa chini yako, hata wale wa halmashauri, nadhani nia ilikuwa ni mfanye quality assurance ili walau basi yale yanayotokana na mikataba mmusaidie CAG ili ripoti ijayo isiwepo.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la TAMISEMI, na ripoti imezungumzwa hapa, kwamba hamrejeshi fedha, na sijui kama Waziri wa TAMISEMI yuko hapa. Nakushukuru na nakupongeza sana, ulisema unataka kuweka misingi ili wanao kufuata wakutane na misingi hiyo. Sasa, kuna suala linatusumbua kila wakati, kutorejeshwa kutoka hazina pesa mnazochukua kwa kigezo kwamba mwaka umeisha. Tumeshazungumza hapa, mnapeleka fedha na hamrudishi. Kwa mfano Kiteto imechukuliwa fedha milioni nane ya mfuko wa jimbo ambayo ilitakuwa iwe imejenga darasa Zambia Kata ya Lengateu, hamtaki kuleta milioni 32 za Basket Fund. Mheshimiwa Waziri kama unanisikiliza hizi pesa Monday, Tuesday Wednesday or next week hizi fedha zije tena. Haiwezekani mnatutengenezea hoja, kesho ripoti za CAG zije halafu mnatuambia kwamba miradi imechelewa, kumbe ni ninyi. Tulishasema hapa mzipeleke hizo fedha. Mheshimiwa Waziri hiyo ndiyo test yako ya Kwanza.

Mheshimiwa Spika, yamezungumzwa mambo mengi hapa, wizi takriban kila mahala, eti mpaka kwenye Balozi zetu; that is how desperate we area, mpaka kwenye Balozi. Sasa ukiona madudu yanafanyika mpaka kwenye Ubalozi basi ujue kwamba tuko desperate sana.

Mheshimiwa Spika, ripoti ya CAG inatuambia, kati ya maagizo ya Bunge hili 619 kwa mamlaka 99 eti kuna maagizo 264 ya Bunge lako hili hayajatekelezwa. Sasa ndiyo tutashangaa zile za Waziri wa Elimu na Bodi ya Mikopo, honestly kama maagizo 264 ya Bunge hili hayatekelezwi!

Mheshimiwa Spika, nimesoma ripoti ya Bodi ya Mikopo inasikitisha sana, kwamba wananchi masikini hata wale wanaotokana na familia za TASAF ambao kimsingi walitakiwa kuwa na dirisha maalum, wanakosa mikopo. Watoto wa wakulima, watoto wa single parent eti wanakosa mikopo. Mwalimu Nyerere alishasema hapa, ukitaka kumsaidia mtoto wa masikini, mpe elimu. Elimu haizuii umasikini, lakini ni silaha ya kupambana na umasikini. Sasa tusipoweka fedha kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wetu, watapambanaje na umasikini?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kweli hili la Bodi ya Mikopo, nashukuru sana kwa maazimio ya Bunge yaliyofanyika juzi. Wanafunzi wanahangaika kila mahali, wanatusumbua sisi Wabunge; “napiga simu hapa niangalie kama nitapata mkopo.” Wanafunzi ambao hali zao wanatoka kwenye familia ambayo ni masikini sana. Inasikitisha sana.

Mheshimiwa Spika, kwa maneno yangu ya mwisho kabisa, kwa sababu ni lazima tutengeneze majawabu. Nilikuwa nasoma kitabu fulani hapa. Institute inaitwa, Wajibu Institute of Public Accountability, wanasema hivi, naomba ninukuu, kwa sababu inaweza ikatusaidia mbele huko.

“Naombeni ushauri, Serikali kuiwezesha Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa ndani kuwa na fungu au Vote ili kumjengea uwezo na kufanya kazi zake kwa uhuru zaidi. Aidha, wajibu wa kumshauri Mkaguzi Mkuu wa ndani awe anapeleka taarifa hizi kwa Katibu Mkuu Ikulu ili taarifa zake zimfikie kwenye Baraza la Mawaziri ambalo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Mwenyekiti wake. Ripoti hii ikimfikia Rais kabla ya Septemba, tarehe 30, ambapo itakuwa ni miezi tisa baada ya mwaka wa fedha wa Serikali kumalizika, hii itampa fursa Mheshimiwa Rais kujua hali ya utendaji wa Serikali kabla ya ripoti ya CAG.”

Mheshimiwa Spika, nadhani hili likichuliwa pengine linaweza likasaidia ku-improve ripoti huko mbele. Nakubaliana na maagizo yote na ripoti zote mbili, naomba Bunge hili sasa lionyeshe kazi yake.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.