Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia taarifa iliyowasilishwa mbele ya Bunge lako Tukufu kuhusiana na Kamati za PAC, PIC pamoja na LAAC.

Mheshimiwa Spika, nitajikita zaidi kwenye hoja ya KADCO. Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumzia suala la KADCO, lakini wengi hawajaingia kwa ndani sana. Binafsi naomba niweze kuelezea kwamba KADCO ni mtoto mmoja aliyezaliwa tarehe 11 Machi, 1998 akiwa na wazazi wawili ambao ni, Mott McDonald aliyekuwa na hisa asilimia 99 na mtu mwingine anaitwa Inter-Consult Tanzania Limited akiwa na hisa asilimia moja. Kampuni hii ilisajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni, Sura ya 212 kama shirika binafsi.

Mheshimiwa Spika, tarehe 17 Julai, 1998, KADCO waliingia makubaliano na Serikali pamoja na McDonald lakini alikuja kujiunga mtu mwingine anaitwa South African Infrastructure Fund wakagawana shareholders kati ya Serikali na wale wamiliki wengine. Serikali ikachukua asilimia 24 ya hisa, McDonald wakawa na asilimia 41.4 ya hisa. South African Infrastructure Fund wakawa na asilimia 30 ya hisa, Inter-consult wakawa na asilimia 4.6.

Mheshimiwa Spika, tarehe 10 Novemba, 1998, KADCO na Serikali wakaingia mkataba wa uendeshaji kwa ajili ya kuhakikisha kwamba miundombinu kwenye uwanja wa KIA inaendelezwa kwa miaka 25. Mwaka 2006 baada ya miaka hiyo yote, Serikali ilikuja ikafanya tathmni ya KADCO kama inafanya kazi ipasavyo kulingana na concession agreement lakini baada ya tathmini Serikali ikasema kwamba tuangalie masuala yafuatayo: -

Je, KADCO inafanya kazi kama ilivyokubaliwa? Serikali ikagundua kwamba wanahisa wenzake ambao ni Mott McDonald waliokuwa na asilimia 41.4, South Africa Infrastructure Fund waliokuwa na asilimia 30 ya hisa, Serikali ambayo ilikuwa na asilimia 24 na Inter-Consult Tanzania Limited waliokuwa na asilimia 4.6. Serikali ikaja kuona kwamba hao wenzake wanahisa hawafanyi kazi vizuri. Serikali ikaamua kwamba, sasa umefika wakati wa kuchukua KADCO moja kwa moja na kununua hisa zote kwa asilimia 100.

Mheshimiwa Spika, kinachotushangaza, kinachonishangaza mimi kama Mjumbe wa Kamati ya PAC, tumemwita Afisa Masuuli Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, tumemuuliza kuhusiana na hawa watu McDonald, South Africa Infrastructure Fund pamoja na Inter-Consult Limited hizo hisa zao zilikuwa na value kiasi gani? Hakuna jibu mpaka leo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kinachoshangaza tena, baada ya Serikali kuchukua hisa zote kwa asilimia mia moja, Serikali kupitia TAA ikaenda kukopa fedha kutoka CRDB USD million 5.3 kwa ajili ya kuwalipa wanahisa wenzake ambao wameshindwa kazi. Hata hivyo, tunachojiuliza hizo fedha zimelipwa kwa kigezo gani? Tumechukua mkopo ambao utalipwa na Serikali kupitia fedha za walipakodi shilingi milioni 5.3 USD kwa ajili ya kuwalipa watu ambao hatukujua hizo hisa zao zina value kiasi gani.

Mheshimiwa Spika, kinachoshangaza vile vile, leo bado Serikali baada ya kununua hisa zote bado tuna concession agreement na KADCO. Huyu KADCO ni nani? Ni swali la kujiuliza huyu KADCO ni nani ambaye bado tuna concession agreement ya miaka 25 ambayo huuhishaji wake utaisha tarehe 16 Julai, 2025. Kama Serikali imesajili kwa mujibu wa mashirika ya umma huyu KADCO ni nani ambaye bado tuna concession agreement na yeye? fedha za walipakodi bado zinapotea kwa sababu hiyo.

Mheshimiwa Spika, ninachojiuliza, kama ni TAA ilichukua mkopo kutoka CRDB shilingi milioni 5.3 Dola za Marekani, maana yake wao ndio wangetakiwa kusimamia Uwanja wa KIA na siyo mtu mwingine tena. Kwa hiyo nitoe pendekezo kama kweli tupo tayari kwa ajili ya kuisaidia nchi hii hatuhitaji kumsikia mtu anaitwa KADCO, labda waje watupe jibu hapa ndani kwamba KADCO ni nani ambaye sisi Wabunge wengine hatumjui. Kwa hiyo Uwanja wa KIA ukabidhiwe kwa TAA ili waweze kuendesha kwa manufaa ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, suala lingine katika kupitia ripoti za CAG kuna mtu anaitwa DUWASA hapa Dodoma, ambao wanatusaidia kusimamia miradi ya maji, kwenye ripoti ya CAG tumeona kwamba DUWASA walichimba visima viwili Kongwa vyenye thamani ya Shilingi Billion1.5. Kitu cha kushangaza kisima kimoja baada ya Miezi Mitano hakitoi maji, kisima kingine hakijawahi kutumika kwa sababu maji yana chumvi, kuwauliza kwa nini? Wanasema tulikuja kuona kwamba yale maji yana chumvi. Kinachoshangaza kwani watalam wetu wanapochimba maji, tuna maabara ya maji, kabla ya maji kutumika ni lazima tupeleke kwenye maabara ya maji yakaangaliwe ubora wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo tumepoteza Fedha za wananchi kwa kuchimba visima, kisima kingine baada ya miezi mitano hakifanyi kazi, tumeishapoteza fedha na naamini ni fedha za walipa kodi. Suala lingine la kusangaza kwenye mradi huohuo ulikabidhiwa mitambo na kibanda ambacho kilikuwa na pampu lakini haijawahi kutumika hata siku moja.

Mheshimiwa Spika, nishauri fedha hizi za walipa kodi zinalipwa na Watanzania nasi kama Wabunge tulipewa nafasi hii kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunazilinda hizo fedha ili zilete manufaa kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, naomba pia nigusie suala la TRA kwenye ripoti ya CAG kutoka Mwaka 2018/2019 mpaka 2020/2021, TRA imeshindwa kukusanya Shilingi Trilioni 6.78, lakini tunajua kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania tumewakabidhi jukumu la kuhakikisha kwamba wanatukusanyia fedha kwa ajili ya kufadhili miradi ya maendeleo. Kila Mbunge yupo kwenye Bunge hili na anataka maendeleo yaende kwenye Jimbo lake, lakini TRA Watumishi waliopo wamekuwa wanashindwa kukusanya mapato yaliyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, ninaomba nishauri Bunge lako Tukufu, kuna mianya mingi ya rushwa kwa sababu ya TRA, ukijaribu kuangalia kuna makadirio ya chini ya kodi nyingi in value inaweza ikafika zaidi ya Billion 30 lakini kuna maeneo mengine wanashindwa kukusanya kodi. Kwa mfano, kwa Mwaka wa Fedha wa 2020/2021 wameshindwa kukusanya Shilingi Billion 8.5 kwa mafuta yanayotumiwa ndani ya nchi. Kwa hiyo TRA wanatakiwa nao kusimamiwa kwa ajili ya kukusanya mapato.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naomba niunge mkono hoja kwa Kamati zote. (Makofi)