Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nianze na ada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba mbingu na ardhi ambaye kwa utashi wake ametuchagua mimi na nyote mliomo humu ndani kuwa na afya njema na kuwa hapa kwa wakati huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naomba nichangie kwa kiasi Mwenyezi Mungu atakachoniwezesha kwenye mjadala huu wa Wizara hii muhimu sana. Nianze kwa kuwaombea dua au kuwatakia kheri wale waliopewa jukumu hili na kuwapa nasaha kwamba walichukue hili kama ibada, wanalifanya kumridhisha muumba wao lakini pia wanalifanya kama wajibu wao wa kijamii ambao wamekabidhiwa na wamekabidhiwa kwa sababu wameonekana wanaliweza. Mimi na wengine wengi tunawaombea Mwenyezi Mungu awawezeshe katika kutekeleza jukumu hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wengi wamechangia nami kila nikifuatilia nazidi kupata wasiwasi. Nikasema labda tuna haja ya kubadili hata hii approach ya kufanya hizi budgeting. Nilikuwa nimesema labda ianzie kule mwanzo kabisa, kuna need ya some sort of brainstorming session ya hawa Mawaziri wetu na watendaji wao wakuu, ile tuliyokuwa tunaita semina elekezi lakini wakae pamoja wakaja na kitu kuna wataalam wanakiita mind map, inakuwa huge thing ambayo inatoa matawi chungu nzima, katikati pale ipo Tanzania halafu kuna hizi Wizara sasa, kila Wizara ipo peke yake inatoa mkia mmoja halafu kila Wizara ina nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoona hapa tukifanya hili zoezi, mwisho wa yote hayo iwe kwamba, lile jambo linatutengenezea system ambayo itakuwa inafanya kazi in a very integrated way yaani iunganeungane. Isiwe kama sasa hivi nahisi kama vile afya wako wenyewe wakija na bajeti yao inaanza upya, elimu wapo wenyewe wakija hapa na bajeti yao inaanza upya kama yenyewe isolated thing siyo kama party of the whole thing. Nadhani tuna haja ya kufanya hicho na vilevile iendane na periodic assessment. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, inanisikitisha hii na bahati mbaya ndiyo nimeingia kwa mara ya kwanza, bajeti inakuja hapa halafu tunaambiwa katika maelezo mwaka jana tulipangiwa shilingi bilioni kadhaa, Bunge likaidhinisha shilingi bilioni kadhaa, lakini tulichopewa ni shilingi milioni kadhaa. Halafu mwakani tukija tunaacha yote yale tunaanza upya, mwaka huu tunaomba kadhaa, sasa hivi hatuendi. Lazima tukishajenga hii system inapokuwa na input process, output na feedback, feedback itumiwe tena kama input tunapoanza second round ya ile process. Isiwe kila mwaka kama tunaanza upya mambo ambayo kwa kweli nadhani hayatatufikisha mahali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tuliangalie hilo kwa upana zaidi na tuone namna gani tunaifanya hii system yote ifanye kazi kwa pamoja, kwa sababu mwisho wa yote ni Serikali hii moja ambayo ndiyo inatakiwa ihudumie wananchi hawa wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yamesemwa mengi masuala mahsusi nami naomba nianze kwa lile suala la kuwa na mahitaji ya ma-specialist wetu. Niwapongeze kwanza wafadhili wetu, they are really friends in need and they are friends indeed kwa sababu kama wanatusaidia kwenye program kama hizi ambazo Dkt. Othman na timu yake wanafanya sasa hivi katika Kanda mbalimbali za kuhudumia watoto wetu wenye vichwa vikubwa. Kwa kweli ni msaada mkubwa na hawa watumishi wetu pia tunawapongeza na tungependa kuwe na mifano kama hii mingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wale ma-specialist wetu wa maeneo mbalimbali waje na some sort of a proposal kwamba wanawezaje wakafanya kazi, labda Serikali na wapenzi wetu wengine watusaidie kutafuta funds ili hawa wataalam wetu, ma-specialist watakuwa wana-move. Kwa kweli ni msaada mkubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, imagine watoto hawa wote wabebwe na mama hawa kutoka mikoa mbalimbali wakajazane pale MOI - Muhimbili hali ingekuwa vipi? Tunawapongeza na tunawaombea Mwenyezi Mungu awalipe kwa hayo mnayoyafanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea Taasisi ya Saratani Ocean Road. Nimeangalia kwenye bajeti yao kwenye hili book kama ndiyo liko sahihi, kuna zero zero, eneo la preventive and cure, actually hata sehemu ya cure pale kwa Ocean Road kuna zero bajeti. Ukiangalia pia kwenye zero budgeting issue nyingine iliyotajwa ni ya HIV/AIDS na kwenyewe kuna zero, sasa nikasema hii kidogo inaleta wasiwasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taasisi hii ya saratani ni moja ya maeneo yale very sensitive. Niliwahi kuzungumza na mtu ambaye yeye aliishi Ujerumani akasema Ujerumani ndiyo mabingwa sana wa haya mambo ya saratani. Hata hivyo, kuna marafiki zake walitutembelea, walipokwenda kwenye taasisi yetu ile wakasema hata vile vifaa vyenyewe havifai kufanyia hiyo tiba tunayofanyia sasa hivi. Nikapata wasiwasi kwamba kama hiyo ndiyo taasisi tunayoitegemea countrywide kuhudumia wagonjwa wetu hawa, halafu na bajeti yenyewe inakwenda hivi, kwa kweli ni hali ya hatari sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye taarifa ya Kamati pia wameeleza vizuri mambo haya. Sidhani kama inaleta maana sana kusema vinahitajika vifaa vya shilingi bilioni sita lakini tumewapa shilingi bilioni mbili. Nina imagine lidude kama X-ray machine kama ni ya shilingi bilioni nne umewapa shilingi mbili sasa wanunue kipande au inakuwa vipi? Kama tumepewa hizi shilingi bilioni mbili mara hii, kwa hiyo tuziweke na je mwakani bei inakuwa ile ile au vipi? Nadhani tunatengeneza environment ambayo tunaji-defeat sisi wenyewe pamoja na kuwa na mipango mingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kabisa Taasisi ya Saratani iangaliwe upya. Iangaliwe upya pia hata kuwasaidia kujipanga wenyewe namna wanavyotoa huduma. Nimesikia vilio vya wagonjwa au wasindikizaji wao wanasema eti wanaamka alfajiri makwao wanakwenda kusubiria pale kupimwa au kupata huduma na inaweza ikafika saa tatu ya usiku hawajahudumiwa, jamani tuwaangalie hawa wenzetu. Kwa kweli ni hali mbaya na tuwasaidie hawa watendaji wetu wawe kwenye environment ambayo kidogo ni rafiki isijekuwa mwisho wa siku na wao pia tukawa tunawadhuru kwa sababu ya kufanya kazi kwenye mazingira ambayo siyo sahihi. Kwa hiyo, naomba sana taasisi hii iangaliwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niseme kwa uchache kuhusu ndoa za utotoni. Kwa sababu niliwahi kujiwa siku moja yaani watu wana jambo linawakera kweli kweli, nini mwalimu tukasaidiane, kitu gani kuna ndoa za utotoni. Kwa nini mimi, aah kwa sababu Waislam tumeonekana ndoa ziko nyingi. Nikamwambia kama ndoa Waislam wanafanya ndiyo ibada kwa sababu ndoa ni nusu ya dini yao lakini ni sunna. Sasa nikasema kama ni Waislam hawatokimbilia kwanza kwenye ndoa watakimbilia kwenye elimu kwa sababu elimu ni faradhi yaani jambo la lazima, sasa wanapataje matatizo haya Waislam? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tatizo linarudi pale pale kwamba kila kitu tunachukua in isolation. Kama tungekuwa na mfumo ambao watoto wetu watasoma pamoja na wasichana wetu mpaka form four, a minimum atakuwa tayari ana miaka 17 akija kuolewa mwakani ana miaka 18 mpaka akipata ujauzito ana miaka 19 ndiyo amewahi huyo. Sasa tutazungumza lini haya mambo ya ndoa za utotoni. Kwa hiyo, hili jambo linakuja kwa sababu approach na mambo yetu tunafanya kwa namna ambayo siyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna waliowahi kusema hapa, tutengeneze mifumo ambayo watoto wetu wote watapata hizi huduma za lazima katika ule umri wao na tunawakuza hivi watakapofikia mahali wanapoanza utu uzima ndiyo haya majukumu mengine ya kiutu uzima na wao yanaendana nao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, siyo suala tu kwamba kuna ndoa za utotoni lakini naona zaidi tatizo ni mimba za utotoni kwa sababu nilikwenda Muhimbili siku moja, Manesi tena wanawachekea hasa, wanasema wapisheni hao chekechea, nawauliza chekechea ni akina nani? Wasichana wale ambao wamejifungua wote wapo kwenye wodi, watoto wao wako huko chini sijui kwenye incubators lakini majority of them wala hawakuolewa. Kwa hiyo, tatizo ni mimba hizi na wala siyo ndoa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia twende mbali zaidi tu-define huyo mtoto ni nani kwa umri wake ambao sikuona humu kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri. Tukimsema huyo mtoto ni nani, halafu tujipange sasa kuhakikisha huyu mtoto tuliyem-define tunamuwekea mazingira mpaka amalize utoto wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.