Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nami naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Ezra. Kwanza napenda kutumia nafasi hii kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuwa na scholarship maalum kwa ajili ya watoto ambao wanaenda kusoma sayansi.

Mheshimiwa Spika, kuna scholarship zimetolewa kwa ajili ya watoto zaidi ya 600, ni jambo jema nami kwa mawazo yangu na uelewa wangu nimeona kwamba kama Taifa tuna miradi mingi inayoendelea. Tuna mradi wa SGR, tuna mradi wa Bwawa la Umeme na juzi tumeona uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanja kikubwa sana cha Kimataifa cha Msalato na viwanja vingi vinaendelea kujengwa kikiwemo kiwanja cha Iringa pale ambacho kitapanua wigo sana wa utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hivi vitu vyote ambavyo tunavijenga, hii miundombinu yote baada ya kuwa imekamilika, itahitaji huduma katika kuiendesha miundombinu hii. Vile vile itahitaji wataalamu na utaalamu na nadhani kwa sababu hiyo ndiyo maana Mheshimiwa Rais akaona atoe scholarship kwa ajili ya watoto ambao baadaye watakuja kutumika katika kusimamia miundombinu na miradi mbalimbali ambayo tunaijenga sasa hivi kwa fedha nyingi ambazo ni za Watanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu hiyo basi, suala la mikopo ni suala ambalo siyo la hiari tena kwa Taifa letu, ni suala la lazima. Tukitoka huko nje kwa wananchi sisi kama Serikali ya Chama cha Mapinduzi, katika mikutano yetu ya hadhara, katika vikao vyetu vya ndani tumekuwa tukijinasibu kwamba tumeongeza fedha kwa ajili ya mikopo ya watoto wetu. Sasa inapotokea kwamba watoto na waliokuwa na ufaulu wamekosa, maana yake ni kwamba tunajichanganya sisi wenyewe na wananchi, kwamba tumeongeza fedha kama alivyosema Mheshimiwa Kanyasu, kijana anauliza hiyo shilingi milioni 570 sasa iko wapi?

Mheshimiwa Spika, sasa kama tumeongeza fedha na watoto hawapati, kwa kadri ya matarajio na kwa kadri ambavyo tumewaaminisha kwamba tumeongeza fedha, maana yake ni kwamba tunakuwa tunawachanganya wananchi.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi niseme jambo moja, maana tayari hii ni crisis, hili ni tatizo. Sasa je, tatizo hili ni namba moja, ni tatizo kama hivyo walivyokuwa wanasema wenzangu namna ya kuwatambua wanaostahili mikopo au tatizo ni ufinyu wa bajeti?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, baada ya kuwa tumetambua shida ni nini, tatizo ni nini, basi kama Bunge ambao tunaishauri na kuisimamia Serikali, ni wajibu wetu kuona tunatoka na suluhisho gani?

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, tulipokuwa tuna shida ya ongezeko la bei ya mafuta kutokana na ongezeko la bei ya mafuta duniani, Serikali yetu tunaipongeza sana ilikaa chini, ikaona kuna umuhimu wa kutoa ruzuku kupunguza makali ya bei ya mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulipokuwa na kilio hapa cha mbolea, Serikali yetu ikafuata ushauri wa Wabunge, imekuja imetoa ruzuku ya mbolea. Mwaka 2021 au mwaka 2020 wakati tulipokuwa na crisis ya bei ya mahindi, tulikaa na Serikali; Wabunge wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, Serikali ikatafuta fedha ikawezesha hifadhi ya chakula, ikatoa fedha mahindi yakanunuliwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ushauri wangu, kama hili ni tatizo basi kama ni la kibajeti, hebu tukae chini tuone tunafanyeje, fedha ipatikane watoto wapate mikopo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)