Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

Hon. Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ili nami niweze kuchangia hoja ambayo iko Mezani.

Mheshimiwa Spika, suala la elimu kwa nchi yoyote ama kwa jamii yoyote ndiyo mkombozi wa mtoto wa masikini yeyote katika taifa lolote. Elimu ndiyo imani ambayo mzazi anaweza kuiweka kwa mtoto wake, ndio urithi pekee ambao mzazi wa kimasikini wa Kitanzania anaweza kumpatia mtoto wake.

Mheshimiwa Spika, napenda kwanza kuipongeza Serikali. Sasa hivi elimu msingi katika nchi yetu ni bure. Mtoto anaanza darasa la kwanza mpaka darasa la saba, anafuata form one mpaka form four, form five mpaka form six. Mazingira ni wezeshi kwa mtoto wa Kitanzania kuweza kupata elimu yake kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha sita. Kwa kweli napenda kuipongeza Serikali kwa jitihada kubwa ambazo imefanya kwa ajili ya haya mazingira wezeshi.

Mheshimiwa Spika, elimu yetu ya Kitanzania mtoto yupo katika elimu kwa miaka takribani 16 hadi 17. Baada ya hapo mtoto huyu anategemewa kwenda elimu ya juu. Pale kwenye elimu ya juu kama atapata nafasi, au kama mkopo atapata ama asipopata, baada ya hapo anaenda mtaani. Tayari tuna-frustration kubwa ya changamoto ya ajira mtaani.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba mtoto anakaa kwa takribani miaka 14 katika elimu, ile miaka mitatu ambayo inabidi amalizie, bado inakuwa kizungumkuti. Kwa hiyo tunakuwa tunavunja imani kwa watoto wetu kuweza kumalizia.

Mheshimiwa Spika, kwa Afrika Mashariki, ukitoa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo imejiunga sasa hivi, Tanzania ni mojawapo ya nchi ambayo ina-population kubwa ya watu. Ukilinganisha na nchi kama Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, Tanzania iko hapo juu lakini kwa kipindi kirefu Tanzania siyo amabayo inaongoza kwa idadi ya wanafunzi ambao wanamaliza katika elimu ya juu. Inaongoza kwa idadi ya population lakini haiongozi kwa idadi ya wanafunzi ambao wanamaliza katika vyuo vikuu vyetu.

Mheshimiwa Spika, nchi zetu jirani kwa mfano, idadi ambazo zinamaliza ni laki moja mpaka laki na ishirini; nchi ambazo zina-population ndogo, lakini sisi idadi zetu ni sixty thousand, elfu hamsini, elfu arobaini na tano, hatuvuki hapo. Sababu ni nyingi lakini sababu mojawapo ni uwezeshaji wa wanafunzi kuweza kujiunga na elimu ya vyuo vikuu. Mikopo imekuwa changamoto kwa kipindi kirefu sana.

Mheshimiwa Spika, elimu ndiyo advantage ambayo tunaweza tukaitumia tukiwa tuna-population. Ukiwa na idadi kubwa ya watu walioelimika, ndipo hapo unaweza ku-explore opportunities nyingi kwa wananchi wa taifa lako. Sasa tukiwa tuna namna ambazo zinasababisha watoto kupata vizingiti vya kuendelea na elimu ya juu hapo kunakuwa kizungumkuti, na hapo ndipo ambapo tunajitahidi huku ngazi za chini tunakuwa na idadi kubwa ya wanafunzi ambao sasa wanakaa mtaani, wanakuwa frustrated, wanajiunga na wale ambao tayari wanachangamoto ya ajira, tunakuwa na taifa la vijana ambaao wako frustrated kwelikweli.

Mheshimiwa Spika, elimu kwenye Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni haki ya msingi kabisa. Kwa hiyo ni jukumu la Serikali kuhakikisha fedha inapatikana kwa ajili ya wanafunzi kusoma, hususani masuala ya sayansi. Sayansi ndiyo ambayp inakomboa taifa lolote duniani kwa sasa masomo ya sayansi ndiyo msingi wa maendeleo ya sayansi na teknolojia kwenye taifa lolote lile; na hapa ndipo ambapo vijana wengi wataweza kuajiriwa. Hatuwezi kutatua changamoto ya ajira taifa hili kwa kazi physical. Changamoto za ajira zinatatuliwa kwa uvumbuzi unaotokea kwenye maendeleo ya sayansi na teknolojia. Sasa tusipoweka mikopo watoto wakasoma kwenye masomo ya sayansi mpaka ngazi ya juu, sasa ubunifu tutatoa wapi?

Mheshimiwa Spika, ni lazima Serikali i-dedicate kwenye kuhakikisha fedha zinapatikana. Ukiangalia bajeti yetu ya Wizara ya Elimu 60% ni Bodi ya Mikopo. Hata hiyo Bodi ya Mikopo imewekwa kwenye list ya miradi ya maendeleo, lakini si mradi halisi wa maendeleo huu. Ilitakiwa iwe ina-vote yake tofauti, peke yake. Ndiyo maana ukiangalia Wizara ya Elimu unaona Bodi ya Mikopo inafedha kubwa lakini haina fedha kubwa. Imekaa kwenye bajeti ya Wizara, ilitakiwa iwe na vote peke yake. Ndiyo maana tukiona bajeti hapa tunaona bajeti ya Wizara ya Elimu ni Bodi ya Mikopo ina fedha kubwa lakini siyo fedha kubwa, ni 60% ya bajeti ya Wizara ya Elimu; lakini sio fedha kubwa. Tunashauri iwe na vote peke yake ili tuweze kui-monitor.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)