Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Sita na Mkutano wa Saba wa Bunge pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa kwenye Mkutano wa Tatu na Mkutano wa Nne wa Bunge

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Sita na Mkutano wa Saba wa Bunge pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa kwenye Mkutano wa Tatu na Mkutano wa Nne wa Bunge

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa nafasi hii ambayo umenipatia na mimi niweze kuchangia hii taarifa ya Kamati ya Sheria Ndogo na mwanzo kabisa nimeshindwa kujizuia kuwapongeza sana Kamati hii ya Sheria Ndogo kwa uchambuzi wao mzuri sana wa hizi sheria na kasoro zilizokuwepo pamoja na mapendekezo ambayo wameyapendekeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo imeelezwa hapa na Kamati kwamba hili suala la sheria ndogo ni suala ambalo ni muhimu sana, ni suala ambalo kama lisiposimamiwa vizuri linaweza kwenda kupoteza hata maana ya sheria zenyewe ambazo zilitungwa na kupitishwa na Bunge hili tukufu. Sasa tusipoliwekea maanani na msimamo mzuri kuanzia kwenye mfumo wa utungaji wake na mpaka utekelezaji wake, tunaweza tukawa tunapiga mark time kila wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri sana kamati hapa imefanya uchambuzi na imefanya uchumbuzi wa sheria wa kanuni kama 14 lakini ukweli ni kwamba sheria ambazo zina changamoto nyingi, ni nyingi sana kwa hiyo hizo ni 14 ni sehemu ndogo sana ya kanuni ambazo zina kasoro na zinazohitaji marekebisho. Kwa hiyo, ina maana kwamba hii Kamati ya Sheria Ndogo pamoja na kazi nzuri sana ya kufanya uchambuzi wa kanuni 14 katika taarifa hii lakini bado wana kazi kubwa sana ya kuhakikisha kwamba zile kanuni zote zenye changamoto ambazo zinaleta mkanganyiko mkubwa kwa wananchi katika utekelezaji wake zinashughulikiwa na zenyewe zinafanyiwa uchambuzi na kuletwa hapa Bungeni kwa ajili ya kufanyiwa uamuzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nakubaliana nao, kwa mfano wametolea mfano kukinzana na masharti ya sheria inayotoa mamlaka ya kutunga sheria ndogo na sheria nyingine za nchi. Hizi tunazo nyingi sana na bahati mbaya sana Kamati wao wamezungumzia suala la sheria ndogo tu lakini kuna waraka nao ambao ukiandikwa na Katibu Mkuu, kuna waraka nao ukiandikwa na Waziri unaenda kutumika na wenyewe kama sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hizi sheria ndogo pamoja na waraka zinapoenda kule zinaenda kwenda ku-distort au kuharibu kabisa hata mifumo ya sheria ambayo ilishawekwa na zingine zimekuwa zikienda hata tofauti kabisa na sheria zenyewe zilizopo sasa kwa mfano kipindi cha UVIKO - 19 tunatekeleza miradi ya UVIKO-19 kuna baadhi ya taasisi hapa ziliandikia taasisi nunuzi barua za kuwataka wakafanye manunuzi kwenye viwanda fulani kwa kuvitaja kwa jina na hayo yalifanyika huku wakijua Sheria ya Manunuzi hairuhusu hilo hayo yalifanyika huku wakijua Sheria ya Ushindani Na. 8 ya mwaka 2003 hairuhusu hilo, lakini yalifanyika na sheria zipo, kuja huku kwenye waraka wakaandikiwa barua ya waraka wahusika wafanye manunuzi katika maeneo hayo, kuja huku ikatekelezwa hivyo hivyo ilivyotekelezwa kinyume cha sheria na kinyume cha utaratibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pale Mvomero kuna kijiji kimoja katika Wilaya ya Mvomero wametunga sheria kwamba mifugo hairuhusiwi kuwepo kwenye kijiji hicho huku wakijua wananchi wanayo ruksa kwa mujibu wa Katiba ya nchi kufanya shughuli za kiuchumi zozote wanazozitaka. Sasa unatunga sheria inasema kwenye kijiji husika hakuna mfugaji kuingia, inatungwa, kanuni inafanya kazi ya muda mrefu na watu wamekuwa wakipigwa faini ya mamilioni ya fedha wakiingiza mifugo kwenye eneo hilo, jambo ambalo linakiuka Katiba, jambo ambalo ni uonevu na manyanyaso kwa wananchi wasiokuwa na hatia.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kanuni hizi ndogo ndio zimetufikisha kwenye kasoro nyingi, mrundikano wa tozo na kodi nyingi katika eneo moja zinatungwa kila taasisi inatunga, TBS anatunga, TMDA anatunga na taasisi zingine zenyewe zinatunga kwenda kusimamia jambo moja, kijiji kina kodi eneo husika, halmashauri ina kodi kwenye eneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, mamlaka zingine zinazosimamia NEMC mlolongo huu wote umetufikisha hapa katika mfumo mzima wa utungwaji wa hizi kanuni na sheria zetu ndogo.

Sasa nasema nini; mfumo wa utungaji wa hizi sheria ni bora tuanzie pale, mfumo wa utungaji wa kanuni za hizi sheria ndogo ukoje utaratibu wa sasa sheria hizi kanuni ndogo hizi zinatungwa na taasisi kwa mfano Serikali ya Kijiji, Halmashauri ya Kijiji, lakini na Waziri kutunga sheria ya utekelezaji wa baadhi wa sheria, na anapomaliza kutunga na ana-gazette kwenye Gazeti la Serikali na baada ya kuwa gazetted kwenye Gazeti ya Serikali ndio Kamati yetu ndogo inarudi kuzipitia na kubaini kasoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mimi nauliza leo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Bunge hili na wewe mwenyewe Naibu Spika, kwani kuna shida gani hizi kanuni ndogo zikafanyiwa mapitio na Kamati yetu ndogo ya Sheria Ndogo kabla hazijaenda kuwa gazetted kwenye Gazeti la Serikali ili changamoto leo tunazojiuliza leo ziwe zimeshapata oversight mapema kabla hazijaenda kwenye utekelezaji wa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati hapa imezungumza na sisi wote ni mashahidi kwamba hizi sheria ndogo zimeenda ku-distort hata sheria yenyewe iliyotungwa, zimeenda kufifisha sheria yenyewe, nguvu ya sheria imeenda kufifishwa kwa kutunga sheria ndogo, lakini pia zimeenda kutungwa hata sheria ndogo ambazo ni kinzani na hata ile sheria mama, na kwa kufanya hivyo wananchi wengi wamepata mateso makubwa kwa sababu wameenda kuadhibiwa kwa kosa ambalo hata linakinzana na sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia inazuia hata utekelezaji wa sheria yenyewe lakini Serikali tumekuwa tukishindwa kesi nyingi sana Mahakamani kutokana na haya, ukienda kutafsiriwa sheria Mahakamani vs hatua iliyochukuliwa kwa kanuni kwa sheria ndogo Serikali inatangazwa kushindwa wakati mwingine tunafidia mabilioni ya fedha kwa hizo technical zilizofanyika katika utungaji na uchukuaji wa hatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hali hiyo lakini pia tumeelezwa hapa hata inapotekea kasoro kurekebishwa hazirekebishwi kwa wakati, sheria ndogo ina kasoro, Kamati imeita mamlaka husika, wamekaa nayo, wamezungumza na wamekubaliana, lakini miezi minne tunaambiwa na Kamati hakuna marekebisho, hayafanyiki, inachukua muda mrefu kufanya marekebisho. Sasa kama haya yote yanafanyika na tunaenda kuwaadhibu wananchi wasiokuwa na hatia na tunaenda kuiingiza Serikali hasara kubwa kwa nini hizi sheria ndogo Bunge hili likakasimu madaraka, kwa hiyo Kamati ya Sheria Ndogo kushughulika na hizi sheria ndogo kabla hazijaenda kwenye utekelezaji ili kuweza kuepuka hizi hasara ambazo tunawezakuwa tunazipitia za kunyika haki watu, lakini pia za kuleta mkanganyiko hata tafsiri ya sheria Mahakamani na kusababisha wakati mwingine watu wengine kukosa haki na kusababisha hata Serikali yenyewe kushindwa baadhi ya kesi mahakamani.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili tusipofanya maamuzi ya namna hiyo ninajua kwamba sheria ndogo hizi hata wakati mwingine kwa mfano kuna mambo tunapitisha humu kama Bunge na mnayapitisha mpaka kwenye bajeti, mnayaweka mpaka kwenye bajeti, halafu baadaye inaamuriwa kwamba kuna maeneo ya sheria ambayo yanarusu Waziri ataenda kutunga sheria ndogo kule, mwisho wa siku Waziri huyo huyo anaenda kufuta baadhi ya hata ya tozo ambazo mlikubaliana humu Bungeni kwa mamlaka hayo aliyonayo kupitia hiyo sheria ndogo bila hata consultation ya Bunge mambo ambayo yanaenda hata kuathiri bajeti yenyewe iliyopitishwa na Bunge, mambo ambayo yanaenda kuleta hasara kubwa kwenye Taifa na mkanganyiko mkubwa wa mhimili wa Bunge pamoja na Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala lingine ambalo ninaomba Kamati ya Sheria Ndogo ikaliangalie ni utekelezaji wa force account. Suala hili la utekelezaji wa force account sasa hivi lina changamoto kubwa, leo hii mradi unapelekwa kwenye shule husika wa madarasa, mwalimu mkuu wa shule hiyo na mwalimu mwingine kila leo mguu na njia kwenda kufanya manunuzi, hawafundishi watoto wapo safari na njia kwenda kufanya manunuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii kwa madaktari zahanati ni moja, mnajenga pale nyumba ya mtumishi, daktari wa eneo hilo kila siku anaenda kwenye manunuzi, akileta mbao leo anaambiwa rangi imeisha, akimaliza kuleta rangi anaambiwa cement imeisha, kila leo yuko safari. Madaktari wetu wagonjwa wetu awatibiwi kwa sababu madaktari wameshapewa kazi nyingine ya manunuzi, kazi nyingine ya kusimamia ujenzi badala ya kazi ambazo husika walizopewa kuzisimamia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kanuni ya sheria ya manunuzi ambayo ndio ina utekelezaji wa force account ni muhimu sana iende ikatizamwe upya, lakini hili suala la force account linatuletea hasara nyingi. Leo hii mradi ukiwa unatekelezwa kwa sababu unasimamiwa na watumishi wa umma maana yake kama ni kwenye halmashauri Mkurugenzi mguu na njia anaenda kuukagua mradi huo, engineer mguu na njia anaenda kukagua mradi huo, Afisa Elimu kama ni wa elimu mguu na njia kila siku anaenda kukuagua mradi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo watumishi karibu halmashauri nzima yote wako barabarani na jana Waziri wa Fedha ametuthibitishia hapa kwamba sasa hivi kuna gharama kubwa sana ya matumizi ya force account kwa sababu ina involve usimamizi wa watu wengi mno.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninyi mnasema mmepunguza gharama, lakini ukweli kwamba hakuna miradi yenye gharama kubwa kama ya force account na inakwepa vitu vingi kwenye force account tunajinyima sisi wenyewe kwa sababu hata VAT hatulipi, kama angekuwa contractor pale hata kama ni mdogo namna gani angelipa VAT. Lakini sisi tunajidanganya, mradi umetekelezwa kwa fedha ndogo kwa sababu tumekwepa kulipa kodi sisi tunajidanganya mradi umetekelezwa kwa fedha ndogo lakini ukichukulia fedha ya mafuta, ya madiwani kwenda kukagua mradi huo, Mkurugenzi Injinia, Afisa Elimu sijui nani gharama zake ni kubwa mno.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini na hasara nyingine pale inapotokea sasa mradi umejengwa chini ya viwango, nani anakamatwa sasa, nani analipia kama ni mkandarasi tungeweza kumwambia mkandarasi kwamba mradi huu aurudie, abomoe na ajenge upya. Sasa leo umejengwa kwa force account, baada ya mwaka mmoja jengo limebomoka, tunaenda kumkamata nani?

Mheshimiwa Naibu Spika, tukamkamate Mkurugenzi Mtendaji, tukamkamate Mganga, tukamkamate nani inahusisha mlolongo mkubwa wa watumishi wa Serikali inahusisha mlolongo mkubwa wa wananchi katika jamii husika. Tunaenda kumkamata nani?

Sasa mimi niombe sana hizi kanuni zilianzishwa kwanza Kamati yetu ya Sheria Ndogo ikajiridhishe na matakwa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)