Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki

Hon. Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kutuwezesha tukae hapa leo na kulijadili jambo hili muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuishukuru Kamati kwa kutoa mwelekeo ambao mawazo yao ni chanya sana katika kukubaliana na wazo la kuridhia Itifaki ya Kuwaongezea Majukumu Mahakama yetu ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wote waliotoa mawazo yao wametoa msukumo kwamba jambo hili kwanza lilichelewa, na ni kweli kabisa kwamba lilichelewa kwa sababu wale waliokuja na wazo la kuanzisha chombo hiki walikuwa na maana yake. Nasi kama Tanzania katika ile Mihimili mitatu ya nchi kubwa zilizoanzisha Jumuiya hii nasi ni mmojawao. Kwa hiyo, nadhani lilikuwa linasubiri wakati na sasa wakati umefika, nami nikubaliane na mawazo ya Waheshimiwa Wabunge waliochangia, kuwashawishi Wabunge wote mliopo katika ukumbi huu kuiridhia hii Itifaki ya kuwaongezea majukumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, actually siyo kuwaongezea majukumu ile Mahakama ni kutufungulia milango sisi Watanzania, kwa sababu kuchelewa kote huku kunaweza kukawa kumesababisha vitu vingi sana ambavyo watu wetu wameshindwa kunufaika kwa wakati juu ya matumizi ya Mahakama hii. Kwa sababu wakati mwingine unaweza ukapata hofu ya kitu chenye msaada kwako mwenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyabiashara wengi sana wanafanya biashara na hizi nchi, lakini inapotokea migogoro unaona kabisa uhitaji wa chombo cha marekebisho ya migogoro ile ni mkubwa kuliko wakati wowote ule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini wazi tunapokwenda kuridhia Itifaki hii ya kuwaongeza Majukumu hii Mahakama ya Afrika Mashariki, itatusaidia sana, hasa katika haya maeneo matatu ambayo yanatufanya tuwe pamoja zaidi. Kuendelea kutoridhia kutasababisha tubaki nyuma sana kwa sababu huwezi kukaa nje ya competition halafu ukasema na wewe ni mmojawapo. Ni lazima tuingie huko ndani tuendelee kunufaika na uwepo wa vyombo hivi, kimsingi kama tulikuwa na mashaka yalishaondolewa na waliokuwa watungulizi wetu, wameonesha kwamba ardhi iendelee kubaki chini ya milki za Serikali husika. Kwa hiyo, hatuna mashaka makubwa sana ambayo unasema hapa hili ndilo linaloweza likasababisha tusi-ratify haya makubaliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika mazingira ya kawaida ninashukuru sana mapokeo ya Waheshimiwa Wabunge kwa sababu katika wale wachangiaji, pamoja na kwamba walikuwa kama Sita tu, lakini unaona ile message walioiwasilisha kwenye Bunge lako Tukufu, ni message nzito sana ya kushawishi ili wananchi wetu waende wakanufaike na hizo opportunities zinazotokana na haya masoko huria, matumizi ya shilingi moja na ile free movement ya vitu katika ukanda wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ninaamini wazi kwamba ikiridhiwa hii inakwenda kufungua miliango. Kwa sababu tukisharidhia tukamalizika katika Jumuiya yetu hii, maana yake vitu vingine ambavyo havijafanyika, kwa mfano kuwa na hiyo one currency haiwezi kwenda kuanza mchakato wa aina yoyote mpaka turidhie sisi wote wanachama ili tukaunde mawazo mapya, kwamba, okay, kutoka hapa sasa hela gani tunaweza tukai- formulate pale iweze kutembea katika huu muungano wetu wa jumuiya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake nchi kama zile za Eurozone unaona wanatumia Euro, siyo hela ya nchi moja katika zile. Na advantage ni kubwa sana kwa sababu biashara inakuwa miongoni mwa wanachama, haikui kwa mtu mmoja mmoja. Kwa hiyo, unaona faida ambayo tunategemea itakwenda kupatikana huko ni kubwa sana. Hivyo basi, mimi nisiwe msemaji sana kwa sababu hakuna ambacho unaweza ukasema unajibu hoja ambazo labda zinataka ufafanuzi. Katika watoa hoja, wote wamekubaliana na wazo la kuridhia mkataba huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, kwanza naunga mkono hoja, vilevile nimalize kwa kusema twendeni kwenye maendeleo ya kweli kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ahsante sana. (Makofi)