Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nakushukuru kwa kunipa nafasi. Niseme tu kwa niaba ya Serikali, maoni ya kamati hizi mbili ambazo ni muhimu sana, ambazo zinafanya kazi ya kufuatilia (over site function) zimefanya kazi zao vizuri sana na ninawapongeza sana. Nampongeza sana Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Mheshimiwa Kaboyoka, taarifa yake nzuri na Wajumbe wote wa Kamati hiyo. Kipekee sana nimpongeze dada yangu Mheshimiwa Grace Tendega kwa ripoti nzuri sana. Nawapongeza pia Makatibu wa Kamati, wamefanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yamesemwa mambo mengi makubwa yenye nia ya kuishauri Serikali, kama ambavyo wajibu wa Bunge umesemwa kwa mujibu wa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nasi kama Serikali, kazi yetu kwa muktadha huu ni kupokea taarifa hizi ambazo baadaye kupitia kiti chako zitapitishwa na kuwa maazimio ya Bunge; kwa hiyo, Serikali kazi yake itakuwa ni kwenda kuyapitia na kuyatekeleza kwa kadri kanuni za Bunge zinavyotaka, ambapo huko tutakutana Serikali pamoja na Kamati na kujaribu kutekeleza na kuteta taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge kwa mujibu wa utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wangekuwepo Mawaziri wote na pengine wangepata fursa ya kusema hapa, wangeweza kupunguza mzigo ambao umesemwa, lakini tunafahamu ziko taratibu. Nakushukuru na kukupongeza pia wewe kwamba umetuongoza vizuri na Serikali tumepata kusikia, lakini kwa michango ya Waheshimiwa Wabunge, unazo Kamati makini. Kwa kweli ni watu makini na wamefanya kazi yao vizuri; nasi upande wa Serikali tutajitahidi kufanya nao kazi vizuri ili tuhakikishe kwamba tunamsaidia Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Rais wa Awamu ya Sita hayuko tayari kuona fedha za Serikali zinachezewa, hayuko tayari kuona Serikali inaingia mikataba mibovu. Amesema ukitaka kujua true colors zake, chezea fedha ya umma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tutafanya kazi hii kwa uaminifu mkubwa upande wetu wa Serikali kwa kadri kila sekta ilivyoguswa ili kuhakikisha kwamba ripoti hizi za Kamati zinatendewa haki ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nirudie tena kuwapongeza Kamati zote mbili kwa kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naunga mkono hoja. (Makofi)