Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa sababu ya muda shukrani zote zimeshakutosha. Nashukuru kupata nafasi hii ya kuchangia katika Kamati yangu ya LAAC.

Mheshimiwa Spika, uhai na uchumi wa nchi yetu umelalia kwenye halmashauri zetu na Ushahidi ni fedha zinazopelekwa huko ni mabilioni ya fedha za watanzania zinapelekwa kwenye halmashauri. Kwa sababu, fedha nyingi zinakwenda huko tunategemea kwamba, usimamizi mkubwa wa fedha na wa makini sana ufanyike huko na watu wanaohusika na usimamizi huu ni maafisa masuuli wakuu katika halmashauri zetu ambao ni wakurugenzi.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, tumehoji wakurugenzi wengi takribani 40 kwa mfano, lakini wakurugenzi hawa wanatofautiana kwa kiasi kikubwa sana katika uwezo wao pale wanapojibu maswali yetu na wanapowakilisha halmashauri zao. Sitaki kuwa na mashaka na uteuzi na mchakato wa jinsi wanavyopatikana, lakini ningependa kushauri kwa sababu, ya umuhimu sana wa watu hawa wanaoitwa wakurugenzi wa halmashauri, maafisa masuuli wa fedha nyingi za watanzania, ningeshauri kwamba, uteuzi wao uanzie kwenye usaili.

Mheshimiwa Spika, wako watanzania wengi sana wana uwezo mkubwa, wafanyiwe usaili wa kutosha, wafanyiwe vetting, baada ya hapo Mheshimiwa Rais sasa akabidhiwe kundi kubwa la watu kama 300 hivi afanye mamlaka yake ya uteuzi ndani ya watu ambao wamefanyiwa usaili, ili tupate watu watakaosimamia fedha hizi. Watu ambao ni makini kwa sababu uhai wa Watanzania uko kule kwenye halmashauri ambako kuna fedha nyingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, upungufu wa watumishi kwenye halmashauri. Kama nilivyosema fedha nyingi ziko kule, lakini watumishi ni wachache sana, watu wanakaimu nafasi wanapewa fedha za acting allowance, kuna watumishi wanadai mpaka bilioni 80 tumewahoji kwa ajili tu ya ku-act, fedha hizi ni sawa na pension ya mtu mwingine. Kwa nini watu wasiajiriwe na watu wenye uwezo wapo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama Serikali inadhani inaepuka mzigo wa ajira ikumbuke kwamba, inapoteza fedha nyingi zaidi kwa kutokuajiri watu ambao wana uwezo na kuweka watu wanao-act kwa kufanya maamuzi ya mabilioni ya watanzania ambayo yako kule. Kwa hiyo, niishauri Serikali, fedha nyingi inapeleka, isikwepe mzigo wa kuajiri watu wenye uwezo ili wasimamie fedha hizi tuweze kuona tija ambayo ya fedha hizi Mheshimiwa Rais anazipeleka kila siku kule katika halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la watumishi pia kukaa maeneo, sehemu moja. Unakuta mkuu wa idara ana miaka kumi katika eneo moja; ameshakuwa sawa na wakulima, ameshakuwa saw ana wafanyabiashara wa eneo husika, amejisahau kabisa kwamba, yeye ni mtumishi wa umma kwa sababu, ameshakaa muda mrefu. Matokeo yake anaingia kwenye migogoro ya ardhi, anaingia kwenye migogoro mingine, matokeo yake kunakuwa kuna matatizo mengi kwenye halmashauri ambayo yanakuja kama hoja kwa CAG. Kwa hiyo, ningeomba tatizo hili Serikali pia, iliangalie kwa macho mawili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya hoja zangu hizi sasa nikupongeze kwa sababu, muda bado ninao, kwa kuchaguliwa. Na tunakushukuru ni Spika wa viwango, taratibu na kanuni zimejaa kwenye kichwa chako. Tuna hakika mambo yatakwenda vizuri katika Bunge letu. Ahsante sana, naunga mkono hoja hii, ahsante sana. (Makofi)