Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili nami niweze kuchangia Hoja hii ya Taarifa ya Kamati ya CAG.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nikupe pongezi wewe binafsi kwa kuchaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Zungu kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda kuunga mkono Taarifa ya Kamati yetu ya LAAC kwa asilimia 100. Kamati yetu imetoa mapendekezo, maoni na ushauri ambao tunaitaka Serikali izingatie; na lengo kuu la mapendekezo, maoni na ushauri wetu kwa Serikali ni kutaka kupunguza idadi ya hoja za ukaguzi ambazo kila mwaka zinaibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Mheshimiwa Spika, baada ya uchambuzi wa Taarifa ya CAG na mahojiano ya baadhi ya Maafisa Masuuli wa Halmashauri, Kamati yetu tumebaini kwamba eneo moja ambalo linazalisha hoja nyingi za ukaguzi ni udhaifu mkubwa kwenye mifumo ya udhibiti wa ndani (internal control system) katika Halmashauri zetu; ziko very weak na ndizo zinazozalisha hoja nyingi za ukaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mifumo ya udhibiti wa ndani (internal control system) ni mifumo ya ki-TEHAMA, kiutawala, taratibu zinazoongoza namna gani malipo yafanyike, namna gani makusanyo yafanyike ambapo Kamati yetu baada ya uchambuzi tumebaini kwamba kuna uwepo wa udhaifu mkubwa katika mifumo hii ya udhibiti wa ndani ambavyo ndivyo vinazalisha hoja nyingi za ukaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukifuatilia hoja nyingi za ukaguzi ambazo zimeibuliwa na CAG ambaye ni Mkaguzi wa Nje; na jambo moja ambalo ni la kufahamu ili tuwekane sawa ni kwamba Mkaguzi wa Nje (CAG) anafanya ukaguzi wa fedha mara moja kwa mwaka, na mara nyingi anafanya ukaguzi wa mahesabu baada ya mwaka mzima wa fedha kuwa umeshapita. Katika Halmashauri zetu tunao watu tunawaita Wakaguzi wa Ndani ambao ndio sehemu ya mifumo ya udhibiti wa ndani ambapo wao wanafanya ukaguzi kila siku katika ile Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, hoja ambazo zinaibuliwa na huyu Mkaguzi wa Nje ambaye anakagua mara moja kwa mwaka, zinadhihirisha wazi uwepo wa udhaifu mkubwa katika mifumo ya udhibiti wa ndani; uwepo wa weaknesses kubwa mno katika internal control systems zetu.

Mheshimiwa Spika, nitaeleza baadhi ya hoja ambazo Mkaguzi wa Nje ameibua ambazo dhahiri zinaonesha wazi kwamba Halmashauri zetu mifumo yake ya udhibiti wa ndani ni very weak, yaani ina udhaifu mkubwa sana. Tulikwenda kukagua miradi katika Halmashauri ya Chemba, huu ni mfano mmojawapo.

Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri ya Chemba tulibaini kuwa Halmashauri imemlipa mkandarasi zaidi ya shilingi milioni 72 kwa kazi ambayo Halmashauri kwa kutumia idara yake ya ma-engineer hawakuikagua wala hawakuipima. Kwa hiyo, hii dhahiri inaonesha kwamba mifumo ya udhibiti wa ndani katika Halmashauri ama haipo au ni makusudi ambayo yamefanyika ili kufanya ubadhirifu wa fedha hizo.

Mheshimiwa Spika, mkandarasi akifanya kazi, ana- raise certificate. Kabla ya kulipwa ni lazima Engineer wa Halmashauri aende site, aipime kazi, aione kama imefanyika kwa specifications zilizokubalika, aseme ndiyo, asaini, ndipo taratibu za kifedha zianze kufuatwa na huyu mkandarasi alipwe. Ila pale ambapo mkandarasi analipwa, kazi haijapimwa wala kukaguliwa, maana yake ni kwamba internal control system ni very weak.

Mheshimiwa Spika, pia tumekuta Halmashauri nyingi kazi zinatolewa bila idhini ya Bodi ya Zabuni. Hii dhahiri ni kwamba internal control systems hazipo. Unawezaje kumpa kazi mkandarasi au mzabuni bila idhini ya bodi ya zabuni kama mahali pale mifumo ya udhibiti wa ndani ipo na inafanya kazi ipasavyo?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono taarifa ya Kamati kwa asilimia mia moja. (Makofi)