Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. JERRY W. SILAA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kuwashukuru wote, tumepata wachangiaji 20 ambao wamechangia hoja zote mbili lakini katika hoja ya Kamati ya Bajeti wametaja mashirika ambayo na sisi tunasimamia kwa haraka haraka Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile, Mheshimiwa Christine Mnzava, Mheshimiwa Subira Mgalu, Mheshimiwa Hyuma, Mheshimiwa Esther Bulaya, Mheshimiwa Joseph Kandege, Mheshimiwa George Malima, Mheshimiwa Issa Mtemvu, Mheshimiwa Dkt. Oscar Kikoyo, Mheshimiwa ShallyRaymond, Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mheshimiwa Esther Matiko, Mheshimiwa Kwagilwa Reuben, Mheshimiwa Stansalaus Mabula, Mheshimiwa Luhanga Mpina, DKT. John Pallangyo, Mheshimiwa Ally Hassan King, Mheshimiwa Abbas Tarimba na Naibu Mawaziri wawili; Naibu wa Viwanda na Biashara - Mheshimiwa Kigahe na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango - Mheshimiwa Chande. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na maoni na mapendekezo yaliyoko kwenye taarifa ya kamati naomba kama walivyosema wachangiaji wengi niseme mambo machache yafuatayo; niombe tuipongeze sana Serikali na tumpongeze kipekee Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuweka mtaji mkubwa kwenye benki yetu ya kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye taarifa yetu tumeelezea mwezi disemba Serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 208 kama mtaji kwa benki hii na juzi tumeona ufaransa benki hii imesaini euro milioni 80 sawa na shililingi bilioni 210 tunaamini fedha hizi zitaenda kuleta tija kubwa kwenye sekta ya kilimo kupitia benki yetu ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru wewe binafsi kwa mwongozo wako kwenye kikao cha leo lakini nimshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Tulia Acskon, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tumshukuru Katibu wetu ndugu Nenelwa Mwihambi, Mkurugenzi wa Idara ndugu Athumani Hussein, Kaimu Mkurugenzi msaidizi ndugu Bisile, makatibu wa kamati yetu wakiongozwa na Zainabu Mkamba, washauri wetu wa mambo ya sheria na wataalamu wengine kwa ushirikiano mzuri wanaotupa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kamati yetu inafanya kazi na Msajili wa Hazina ndugu Mgonya Benedict, tunamshukuru sana kwa kazi kubwa anayotusaidia na wataalamu wake ambao anafanya nao kazi, tuwataje ndugu Lightness Mauki, Mkurugenzi wekezaji wa umma, na Linus Kwakesigabo, Mhasibu Msaidizi wambao wamekuwa wakitusaidia sana kwenye kazi zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wachangiaji wengi wamezungumza mambo yale tuliyoyatoa kwenye maoni na mapendekezo itoshekusema tu maeneo yote mlioyataja ya APZA, NHIF, MSB, TARURA, NHC, TPA, kwenye maeneo ya TICTS
na kule kwenye uyejushaji wa mafuta, RUWASA, yote tutayafanyia kazi kwa mashirika yale tunayoyasimamia na tunaamini Msajili wa Hazina atatengeneza utaratibu mzuri wa kamati yetu kuweza kufanya kazi ya kusimamia uwekezaji wa mitaji ya umma na mashirika haya yaweze kuleta tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumesema kwenye taarifa yetu kwamba gawiwo la mashirika haya ni moja kati ya chanzo kikubwa cha mapato kwenye mfuko wa Taifa, Kamati yetu itaendelea kufanya kazi kwa moyo na uwadilifu wa hali ya juu katika kuishauri Serikali kuweza kuwezesha mashirika haya yaweze kufanya kazi vyema katika kuleta tija na ufanisi wa hali ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho siyo kwa umuhimu niwashukuru sana wajumbe wa kamati Makamu mwenyekiti, Mheshimiwa George Malima na wajumbe wote kwa ufinyu wa muda naomba majina yao yaliyokwenye kamati yaingie kwenye Kumbu kumbu za Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa kutoa hoja.

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.